Ni kweli Makamba natumia Biblia kwa ufinyu sana. Ukisoma Biblia utakuta Manabii wengi sana walikuwa wakitumia muda mwingi kuwakosoa watawala wa Israel/Yuda na wengi wao walipata misukosuko sana. Nabii Elisha, Nabii Isaya na Yeremia ni mifano mojawapo. Ilifikia Nabii Yeremia akatumbukizwa kwenye kisima kwa kumkosoa na kumkemea Mfalme. Kazi wa watu wa dini ni pamoja na kukosoa watawala.