Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,956
- 22,148
Wakati huohuo, Mchungaji Mtikila amewacharukia wachungaji na maaskofu wanaodaiwa kupanda mbegu kwenye taasisi ya Deci na kwenda kuzivuna kinyemela baada ya serikali kuizuia kufanya kazi, akidai hao si wachungaji wa watu bali ni wachunaji.
Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika juzi Jumamosi kwenye viwanja vya Jangwani jijini Dar es Salaam uliokutanisha wapandaji na kamati ya dharura ya wanachama hao, Mtikila alisema habari za kuwapo watu wakubwa kungoa fedha zao ni za kusikitisha.
"Nimepigiwa simu na baadhi ya watu wakinieleza wazi kuwa kuna baadhi ya maaskofu na wachungaji waliokuwa wamepanda mbegu zao Deci eti wameng'oa mbegu hizo kinyemela, hizi ni habari mbaya kuona mchungaji anayetakiwa kuchunga kondoo anamshawishi kondoo wake kuweka fedha Deci na baadaye anakwenda kuchukua kimya kimya na kumuacha kondoo huyo akihangaika, huyu si mchungaji wa kweli bali ni mchunaji," alisema.
Mtikila alisema kitendo cha watumishi hao wa Mungu kuchukua fedha zao kimya kimya na kuwaacha waumini wao wakihangaika, kinampa mashaka juu ya ushiriki wao katika taasisi hiyo.
Katika hatua nyingine mwenyekiti wa kamati ya dharura ya wanachama wa Deci, Mchungaji Isaack Kalenge ameeleza kufurahishwa na uamuzi wa serikali kuzuia Deci kutoa fedha kwa wanachama waliotakiwa kuanza juzi, akisema utoaji fedha hizo ungesababisha watu kupoteza haki zao.
Alisema yeye kama mtetezi wa wanachama anapingana na kitendo cha uongozi wa Deci kinachodai watu watakaolipwa ni wale ambao hawajawahi kuvuna, akisema kufanya hivyo ni kuonea wanyonge.
Kalenge alisema yeye na kamati yake wameamua kujitolea kushughulikia suala la wanachama wa Deci hadi wanahakikisha wanapata haki zao ili kusiwe hata na mmoja anayedhulumiwa.
Wakati huohuo leo katika ofisi za Deci zoezi la kuorodhesha majina ya wanachama kwa ajili ya kuja kungoa mbegu zao linaendelea baada ya mapumziko ya siku ya Jumapili.
Kwa mjibu wa ratiba iliyotolewa na uongozi wa Deci zoezi hilo litaanza saa za kawaida za kazi na utaratibu wa kawaida wa kuorodhesha majina kwa kutumia namba unaendelea kutumika.
Katika hatua nyingine Fidelis Butahe anaripoti kuwa wastaafu wa iliyokuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) wameibuka na kuitupia lawama serikali kwa kuifungia taasisi ya Deci.
Mwenyekiti wa jumuiya hiyo, Nathaniel Mlaki alisema uamuzi huo wa serikali unaonyesha ni jinsi gani isivyojali maendeleo ya wananchi.
"Tangu uhuru mpaka hivi leo hakuna chombo chochote kilichowekwa na serikali kwa ajili ya kusaidia wananchi wenye kipato cha chini, lakini Deci ilifanya hivyo na hakuna mtu aliyelalamika kutapeliwa na taasisi hii sasa kwa nini ifungiwe.
"Wastaafu tumedai fedha zetu tumeishia kufunguliwa kesi, washiriki wa Deci ambao wengi ni walalahoi wamepanda mbegu, lakini sasa taasisi hiyo imefungiwa. Kwa nini kila mwananchi wa kipato cha chini anapokuwa katika utaratibu wa kujikwamua, serikali inaingilia kati; hivi hiyo ndio demokrasia?"
Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika juzi Jumamosi kwenye viwanja vya Jangwani jijini Dar es Salaam uliokutanisha wapandaji na kamati ya dharura ya wanachama hao, Mtikila alisema habari za kuwapo watu wakubwa kungoa fedha zao ni za kusikitisha.
"Nimepigiwa simu na baadhi ya watu wakinieleza wazi kuwa kuna baadhi ya maaskofu na wachungaji waliokuwa wamepanda mbegu zao Deci eti wameng'oa mbegu hizo kinyemela, hizi ni habari mbaya kuona mchungaji anayetakiwa kuchunga kondoo anamshawishi kondoo wake kuweka fedha Deci na baadaye anakwenda kuchukua kimya kimya na kumuacha kondoo huyo akihangaika, huyu si mchungaji wa kweli bali ni mchunaji," alisema.
Mtikila alisema kitendo cha watumishi hao wa Mungu kuchukua fedha zao kimya kimya na kuwaacha waumini wao wakihangaika, kinampa mashaka juu ya ushiriki wao katika taasisi hiyo.
Katika hatua nyingine mwenyekiti wa kamati ya dharura ya wanachama wa Deci, Mchungaji Isaack Kalenge ameeleza kufurahishwa na uamuzi wa serikali kuzuia Deci kutoa fedha kwa wanachama waliotakiwa kuanza juzi, akisema utoaji fedha hizo ungesababisha watu kupoteza haki zao.
Alisema yeye kama mtetezi wa wanachama anapingana na kitendo cha uongozi wa Deci kinachodai watu watakaolipwa ni wale ambao hawajawahi kuvuna, akisema kufanya hivyo ni kuonea wanyonge.
Kalenge alisema yeye na kamati yake wameamua kujitolea kushughulikia suala la wanachama wa Deci hadi wanahakikisha wanapata haki zao ili kusiwe hata na mmoja anayedhulumiwa.
Wakati huohuo leo katika ofisi za Deci zoezi la kuorodhesha majina ya wanachama kwa ajili ya kuja kungoa mbegu zao linaendelea baada ya mapumziko ya siku ya Jumapili.
Kwa mjibu wa ratiba iliyotolewa na uongozi wa Deci zoezi hilo litaanza saa za kawaida za kazi na utaratibu wa kawaida wa kuorodhesha majina kwa kutumia namba unaendelea kutumika.
Katika hatua nyingine Fidelis Butahe anaripoti kuwa wastaafu wa iliyokuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) wameibuka na kuitupia lawama serikali kwa kuifungia taasisi ya Deci.
Mwenyekiti wa jumuiya hiyo, Nathaniel Mlaki alisema uamuzi huo wa serikali unaonyesha ni jinsi gani isivyojali maendeleo ya wananchi.
"Tangu uhuru mpaka hivi leo hakuna chombo chochote kilichowekwa na serikali kwa ajili ya kusaidia wananchi wenye kipato cha chini, lakini Deci ilifanya hivyo na hakuna mtu aliyelalamika kutapeliwa na taasisi hii sasa kwa nini ifungiwe.
"Wastaafu tumedai fedha zetu tumeishia kufunguliwa kesi, washiriki wa Deci ambao wengi ni walalahoi wamepanda mbegu, lakini sasa taasisi hiyo imefungiwa. Kwa nini kila mwananchi wa kipato cha chini anapokuwa katika utaratibu wa kujikwamua, serikali inaingilia kati; hivi hiyo ndio demokrasia?"