Regia Mtema
R I P
- Nov 21, 2009
- 2,970
- 864
Wakuu.
Leo tulitembelea Kaburi la Hayati Baba wa taifa na kufanikiwa kukutana na Mama Maria pamoja na watoto wake wawili,Magige na Makongoro. Walitupokea vizuri sana.Pamoja na mambo yote yaliyofanyika kuna jambo moja tu nililolipenda zaidi.Maneno mazuri ya Magige kwa chama cha CHADEMA kuhusu maandamano. Amesema hivi ukiwa huna taarifa utapinga sana wanachokifanya CHADEMA kama ambavyo yeye alikuwa akipinga mwanzoni hasa Wabunge wa CHADEMA walivyotoka nje ya Bunge kutomsikiliza Rais Kikwete lakini baadaye amejifunza kwamba CHADEMA wanafanya kitu chema na akatoa mfano wa maandamano yanayoendelea sasa kuwa yanaumuhimu mkubwa sana hivyo akatoa rai kuwa kila mwenye kuipenda nchi hii basi lazima aunge mkono harakati hizi za CHADEMA.Amekiri kuwa yeye ni CCM damu lakini anaunga mkono harakati hizi za CHADEMA.
Vile Vile ameitakia CHADEMA ushindi wa Urais mwaka 2015 kwa kutaka wajitokeza wapiga kura Milioni Kumi na Mbili halafu CHADEMA ipate Kura Milioni Sita na CCM Milioni Nne.
Nawasilisha
Kutoka Kitangiri Mwanza
Reagia E Mtema
Waziri Kivuli-Kazi na Ajira
Leo tulitembelea Kaburi la Hayati Baba wa taifa na kufanikiwa kukutana na Mama Maria pamoja na watoto wake wawili,Magige na Makongoro. Walitupokea vizuri sana.Pamoja na mambo yote yaliyofanyika kuna jambo moja tu nililolipenda zaidi.Maneno mazuri ya Magige kwa chama cha CHADEMA kuhusu maandamano. Amesema hivi ukiwa huna taarifa utapinga sana wanachokifanya CHADEMA kama ambavyo yeye alikuwa akipinga mwanzoni hasa Wabunge wa CHADEMA walivyotoka nje ya Bunge kutomsikiliza Rais Kikwete lakini baadaye amejifunza kwamba CHADEMA wanafanya kitu chema na akatoa mfano wa maandamano yanayoendelea sasa kuwa yanaumuhimu mkubwa sana hivyo akatoa rai kuwa kila mwenye kuipenda nchi hii basi lazima aunge mkono harakati hizi za CHADEMA.Amekiri kuwa yeye ni CCM damu lakini anaunga mkono harakati hizi za CHADEMA.
Vile Vile ameitakia CHADEMA ushindi wa Urais mwaka 2015 kwa kutaka wajitokeza wapiga kura Milioni Kumi na Mbili halafu CHADEMA ipate Kura Milioni Sita na CCM Milioni Nne.
Nawasilisha
Kutoka Kitangiri Mwanza
Reagia E Mtema
Waziri Kivuli-Kazi na Ajira