Mwana JF,
Nape amezidi kusasibu kuwa zoezi la kujivua gamba linarudisha imani ya wananchi kwa CCM.
[h=2]Maamuzi ya CCM yanarudisha imani kwa wananchi[/h]Thursday, 04 August 2011 19:55 newsroom
NA BASHIR NKOROMO
HATUA ya kuwataka watuhumiwa wa ufisadi wapime na kuchukua uamuzi wa kuondoka katika vikao vya maamuzi ya CCM, kutakifanya Chama kuaminiwa zaidi na wananchi. Hayo yalisemwa jana mjini Dar es Salaam na Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, alipokuwa akizungumza na viongozi wa Kampuni ya Africa Media Group, inayomiliki vyombo kadhaa vya habari, kikiwemo kituo cha Televisheni cha Chanel Ten. Alisema, maamuzi ya CCM yanalenga zaidi maslahi ya nchi na wananchi wake na si maslahi ya mtu mmoja mmoja. Alisema, kutokana na misingi iliyowekwa na waasisi wake, CCM bado ina kila sababu ya kuendelea kuongoza nchi kwa kutekeleza yale yote ambayo yamo ndani ya Ilani ya Chama hicho.
Nape alisema, mazingira yaliyokuwapo ndani ya Chama hivi sasa, yamekilazimu kufanya mabadiliko ili kukabiliana na changamoto mbali mbali. Alisema, mabadiliko hayo ambayo yalipitisha maamuzi zaidi ya 20, ni miongoni mwa mengi ambayo CCM imekuwa ikiyafanya tangu wakati wa TANU na hivyo watu wasichukue muda mwingi kuyashangaa bali washiriki katika kuyaenzi kwa kufanya utekelezaji. Hata hivyo, alikiri kuwa mabadiliko hayo yanaweza kuwaathiri baadhi ya watu, lakini hilo halitakuwa jambo la ajabu kwa sababu mabadiliko yoyote yanapotokea, wapo watakaoathirika katika kipindi kifupi, lakini wakafaidika kwa muda mrefu. "Siwezi kusema hakuna watakaoathiriwa na mabadiliko haya, wale waliokuwa wananufaika na mfumo holela uliokuwa unawapa mwanya kufanya mambo kwa manufaa yao hata kama yanaathiri taifa, lazima wataguna na kujaribu kufanya sarakasi za kupinga mabadiliko haya," alisema Nape. Alisema kutokana na sababu hizo, ndio maana zimetokea changamoto za hapa na pale katika mapokeo ya mabadiliko yaliyofanywa na CCM, ikiwemo baadhi kujaribu kujitokeza na kusema hadharani kwamba mabadiliko haya hayana maana.
Nape aliwataka Watanzania na hasa vyombo vya habari, kuacha kuyafanyia kazi maneno ya mitaani, hasa yanayokihusu Chama cha Mapinduzi. Alisema CCM inaendeshwa kwa vikao na hata wanahabari wanapaswa kuripoti kile kilichozungumzwa ndani ya vikao.
Alisema milango ipo wazi kwa kila mwenye hoja mbadala inayohusu maamuzi yanayofanyika hivi sasa. Ziara hiyo ya kutembelea vyombo vya habari, ni mwendelezo wa ziara za Mwenezi huyo alizoanza kuzifanya mwezi uliopita.
Source: Uhuru Newspaper 4/8/2011
Nape amezidi kusasibu kuwa zoezi la kujivua gamba linarudisha imani ya wananchi kwa CCM.
[h=2]Maamuzi ya CCM yanarudisha imani kwa wananchi[/h]Thursday, 04 August 2011 19:55 newsroom
NA BASHIR NKOROMO
HATUA ya kuwataka watuhumiwa wa ufisadi wapime na kuchukua uamuzi wa kuondoka katika vikao vya maamuzi ya CCM, kutakifanya Chama kuaminiwa zaidi na wananchi. Hayo yalisemwa jana mjini Dar es Salaam na Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, alipokuwa akizungumza na viongozi wa Kampuni ya Africa Media Group, inayomiliki vyombo kadhaa vya habari, kikiwemo kituo cha Televisheni cha Chanel Ten. Alisema, maamuzi ya CCM yanalenga zaidi maslahi ya nchi na wananchi wake na si maslahi ya mtu mmoja mmoja. Alisema, kutokana na misingi iliyowekwa na waasisi wake, CCM bado ina kila sababu ya kuendelea kuongoza nchi kwa kutekeleza yale yote ambayo yamo ndani ya Ilani ya Chama hicho.
Nape alisema, mazingira yaliyokuwapo ndani ya Chama hivi sasa, yamekilazimu kufanya mabadiliko ili kukabiliana na changamoto mbali mbali. Alisema, mabadiliko hayo ambayo yalipitisha maamuzi zaidi ya 20, ni miongoni mwa mengi ambayo CCM imekuwa ikiyafanya tangu wakati wa TANU na hivyo watu wasichukue muda mwingi kuyashangaa bali washiriki katika kuyaenzi kwa kufanya utekelezaji. Hata hivyo, alikiri kuwa mabadiliko hayo yanaweza kuwaathiri baadhi ya watu, lakini hilo halitakuwa jambo la ajabu kwa sababu mabadiliko yoyote yanapotokea, wapo watakaoathirika katika kipindi kifupi, lakini wakafaidika kwa muda mrefu. "Siwezi kusema hakuna watakaoathiriwa na mabadiliko haya, wale waliokuwa wananufaika na mfumo holela uliokuwa unawapa mwanya kufanya mambo kwa manufaa yao hata kama yanaathiri taifa, lazima wataguna na kujaribu kufanya sarakasi za kupinga mabadiliko haya," alisema Nape. Alisema kutokana na sababu hizo, ndio maana zimetokea changamoto za hapa na pale katika mapokeo ya mabadiliko yaliyofanywa na CCM, ikiwemo baadhi kujaribu kujitokeza na kusema hadharani kwamba mabadiliko haya hayana maana.
Nape aliwataka Watanzania na hasa vyombo vya habari, kuacha kuyafanyia kazi maneno ya mitaani, hasa yanayokihusu Chama cha Mapinduzi. Alisema CCM inaendeshwa kwa vikao na hata wanahabari wanapaswa kuripoti kile kilichozungumzwa ndani ya vikao.
Alisema milango ipo wazi kwa kila mwenye hoja mbadala inayohusu maamuzi yanayofanyika hivi sasa. Ziara hiyo ya kutembelea vyombo vya habari, ni mwendelezo wa ziara za Mwenezi huyo alizoanza kuzifanya mwezi uliopita.
Source: Uhuru Newspaper 4/8/2011