Maajabu ya Kisiwa cha Bermuda

Socratic

JF-Expert Member
Dec 18, 2014
568
308
Uko ndani ya ndege. Kukiwa na utulivu mkubwa ambapo watu wengi wanaonekana kusinzia. Umejiegemea kwenye seat yako ukitafakari hili na lile.. Ghafla unaskia sauti ya kilio cha mtoto mchanga kwa mbali.. unageuka huku na kule na unajiridhisha sauti ile unayoiskia haitoki ndani ya ndege bali nje.

Unajiuliza mara mbili mbili.. unashangaa . Ghafla unajiskia ulazima wa kwenda haja ndogo, unapokaribia mlango wa choo unaanza kuhisi mle ndani ya choo kuna nyoka kibao. Unajipa ujasiri na kufungua mlango, mlango haufunguki. Unasukuma tena kwa nguvu mlango bado haufunguki.

Unapata hisia kuna nyoka mkubwa yuko mlangoni ndio maana mlango haufunguki.Unaamua kuahirisha tukio unarudi kukaa kwenye kiti chako, ile kukaa tu unakutana na boonge la mtikisiko (turbulent). unaanza kuhisi ndege inadondoka&[HASHTAG]#8230[/HASHTAG];unaangalia saa..ni saa 5 usiku na bado kuna kama masaa matano kabla ya ndege kutua.

Unafungua dirisha kuangalia nje ni giza totoro, unachokishuhudia nje ni mvua kubwa na radi, pia sauti ya kilio cha kitoto kichanga inasikika zaidi. Isitoshe unaskia mshindo mkubwa kwa mbali. Haraka unafunga dirisha.Unaamua kupambana na hofu kwa kujiimbisha,&[HASHTAG]#8230[/HASHTAG];Mbinguni..kuna makao mazuri sana.

unaangalia pembeni unajistukia umekuwa ukiimba kwa sauti kiasi cha kuwaamsha baadhi ya abiria wenzako ambao wanakuangalia kwa jicho la kukushutumu na pia unajistukia ni kama wimbo wenyewe unakusuta vile kwa mazingira uliyonayo. Unajaribu kupotezea kwa kujichekesha lakini sauti inayotoka inakuwa ya ajabu kutokana na hofu uliyonayo.

Unaacha kuimba na kuiruhusu hofu iliyokushika itawale. Unawasha kitv unaangalia geographical location ulipo&[HASHTAG]#8230[/HASHTAG]; ramani inakuonesha unapita kisiwa cha Bermuda.Kijasho chembamba kinakutiririka japo kuna AC. Unatamani ushuke.
Bermuda Triangle, ambayo pia inajulikana kama Devil's Triangle, ni eneo la magharibi wa bahari ya Atlantiki ya kaskazini ambapo idadi kumbwa ya ndege na vyombo vya baharini vinanadaiwa kutoweka katika hali isiyojulikana ambayo haiwezi kuelezewa kama makosa ya binadamu, uharamia, hitilafu ya vifaa, au au maafa ya kiasili. Tamaduni maalufu zinahusisha kutoweka huku na jambo lisilo la kawaida ambalo haliwezi kuelezewa kwa njia za kisayansi, kutanguliwa kwa sheria za fizikia, au shughuli za viumbe visivyo vya kawaida.Jisomee hapa chini baadhi ya maajabu ya eneo hili

1. Bermuda triangle ni eneo katika uso wa Dunia ambalo linahusishwa na masuala mbalimbali ya nguvu za maajabu, ni eneo ambalo maelfu ya watu wamepoteza maisha, ndege na meli nyingi sana zimezama katika eneo hilo pasipo kujulikana zinaelekea wapi. Wanasayansi wengi wamepoteza pesa zao pasipo kutoa majibu kuhusu maajabu ya eneo hilo na kila aliyeenda hajafanikiwa kutoka na inasemekana Zaidi ya ndege na meli 1000 zimepotea kwa mud wa miaka 500.

2. Bermuda Triangle inapatikana pwani ya kusini mashariki ya marekani na iko katika bahari ya Atlantic. Kona zake huunda pembe tatu ambazo ni Miami huko marekani, San Juan Nchini Puerto Rico na Buermuda katika kisiwa kaskazini mwa kisiwa cha Atlantic.

3. Ajali/mgongano kati ya kimondo na dunia
Inasemekana kuwa Bermuda triangle ilitokea baada ya Dunia kugongana na kimondo huko angani miaka 11,000 iliyopita. Mgongano huo ulitokea katika eneo la bahari la Dunia na kusababisha bahari kuzama kwa futi 10,000 chini ya usawa wa bahari. Kimondo hicho kiliacha mionzi ambayo ambayo husababisha ndege kupoteza uelekeo inapofika katika eneo hilo na kuzamsha meli, ndege pamoja na binadamu.

4. Viumbe vigeni viishivyo sayari nyingine (aliens).
Inasemekana kuwa viumbe viishivyo angani, huwa vinakaa aktika eneo hilo la Bermuda triangle na hilo ni kama Mecca yao. Viumbe hao wana teknolojia ambayo hukinzana na teknolojia yetu ya Duniani, kwahiyo basi ndege, meli pamoja na binadamu wanapopita pale huvutwa na kani ya uvutano ambayo ni kubwa sana toka kwa wale viumbe waishio katika ilo eneo hilo la bermuda.

5. Kituo cha majaribio ya silaha.
Inasemekana serikali huwa zinajaribia silaha ambazo zinakuwa zimetengenezwa na uangalizi wa silaha hizo, pia inasemekana kwamba serikali ikishirikiana na viumbe watokao sayari (Aliens) zingine huhusika katika majaribio hayo. Na hiyo teknolojia ni kubwa kiasi cha kukinzana na teknolojia ya duniani na hatimaye kusababisha madhara kwa meli na ndege pia.

6. Mji uliopotea
Inasemekana katika eneo hilo kulikuwa na mjia wa kale chini ya maji katika bahari ya Atlantic, ulioitwa Atlantis, mji huo ulikuwa umejengeka kwa barafu ambazo zilikuwa kama kioo ambazo pia zilikuwa ni chanzo cha nishati. Na huo mji ulisahaulika milele kwahiyo basi Bermuda iko kwenye huo mji uliozikwa kitambo ambapo kuna kani kubwa ambayo huharibu meli na ndege

7. Kituo cha Maharamia
Inasemekana Bermuda ni eneo kwa ajili ya maharamia kufanya kazi zao, maharamia hao ni wale wanaojulikana kwa bendera nyeusi zenye picha ya fuvu. Lakini dhana hii imeshindwa kuelezea ni kwanini ndege na meli huwa zunapotea katika eneo hilo kwani wachunguzi wa mambo wamehusisha na utekaji nyara wa meli baharini ambao hufanywa na maharamia hao.

8. Volkano.
Inasemekana Volkano pamoja na gesi ya methane katika eneo la Bermuda hupunguza mgandamizo wa maji katika eneo hilo na kufanya meli kupoteza uwezo wa kuelea na hatimaye kuzama. Eneo hilo mlimekuwa likitoa gesi hiyo ya Methane tangu miaka 15,000 iliyopita.

9. Ukungu wenye hali ya ki-electronic na sumaku
Ukungu wenye nguvu ya kuzalisha umeme ambapo husababisha dira hupoteza uelekeo na kuwachanganya marubani pamoja na manahodha. Na hatimaye ndege pamoja na Meli hizo hupotelea katika ilo eneo la Bermuda.

10. Mawimbi na hali ya hewa kubadilika kwa kasi.
Eneo la bahari ya Atlantic hasa upande wa Caribbean hukumbwa na kimbunga kikali pamoja na mawingu mazito, Bermuda ni eneo ambalo limepakana sana na Caribbean na hukabiliwa na upepo na wingu zito ambavyo husababisha mushkeli kwa ndege, meli pamoja na binadamu.
 
Kuna watoto wakali sana pale, ngoja mvua iishe niende tcra kuomba ruhusa/kibali cha kuwawekea hii video na hizi jpeg
 
Uko ndani ya ndege. Kukiwa na utulivu mkubwa ambapo watu wengi wanaonekana kusinzia. Umejiegemea kwenye seat yako ukitafakari hili na lile.. Ghafla unaskia sauti ya kilio cha mtoto mchanga kwa mbali.. unageuka huku na kule na unajiridhisha sauti ile unayoiskia haitoki ndani ya ndege bali nje.

Unajiuliza mara mbili mbili.. unashangaa . Ghafla unajiskia ulazima wa kwenda haja ndogo, unapokaribia mlango wa choo unaanza kuhisi mle ndani ya choo kuna nyoka kibao. Unajipa ujasiri na kufungua mlango, mlango haufunguki. Unasukuma tena kwa nguvu mlango bado haufunguki.

Unapata hisia kuna nyoka mkubwa yuko mlangoni ndio maana mlango haufunguki.Unaamua kuahirisha tukio unarudi kukaa kwenye kiti chako, ile kukaa tu unakutana na boonge la mtikisiko (turbulent). unaanza kuhisi ndege inadondoka…unaangalia saa..ni saa 5 usiku na bado kuna kama masaa matano kabla ya ndege kutua.

Unafungua dirisha kuangalia nje ni giza totoro, unachokishuhudia nje ni mvua kubwa na radi, pia sauti ya kilio cha kitoto kichanga inasikika zaidi. Isitoshe unaskia mshindo mkubwa kwa mbali. Haraka unafunga dirisha.Unaamua kupambana na hofu kwa kujiimbisha,…Mbinguni..kuna makao mazuri sana.

unaangalia pembeni unajistukia umekuwa ukiimba kwa sauti kiasi cha kuwaamsha baadhi ya abiria wenzako ambao wanakuangalia kwa jicho la kukushutumu na pia unajistukia ni kama wimbo wenyewe unakusuta vile kwa mazingira uliyonayo. Unajaribu kupotezea kwa kujichekesha lakini sauti inayotoka inakuwa ya ajabu kutokana na hofu uliyonayo.

Unaacha kuimba na kuiruhusu hofu iliyokushika itawale. Unawasha kitv unaangalia geographical location ulipo… ramani inakuonesha unapita kisiwa cha Bermuda.Kijasho chembamba kinakutiririka japo kuna AC. Unatamani ushuke.

nasikia ndege hazipiti hapo. Je ni kweli?
 
nasikia ndege hazipiti hapo. Je ni kweli?
nope.. its just a myth.. hizi stori nilisikia nikaamua kufanya uchukunzi kwa kusoma kwenye sites kadhaa na vitabu.. ni uwongo tu unakuzwa/unatengenezwa na watu na kuna watu/wazungu wametengeneza fedha nyingi kwa hii stori..
kwenye data za ajali za ndege na meli za marekani kuna ajali moja tu ya ndege tena ni eneo pembeni kidogo imewahi kuripotiwa na hakuna pengine popote imewahi kurekodiwa kuwa kuna ndege/meli imewahi kupotea maeneo hayo..
so ni uwongo tu..
 
nope.. its just a myth.. hizi stori nilisikia nikaamua kufanya uchukunzi kwa kusoma kwenye sites kadhaa na vitabu.. ni uwongo tu unakuzwa/unatengenezwa na watu na kuna watu/wazungu wametengeneza fedha nyingi kwa hii stori..
kwenye data za ajali za ndege na meli za marekani kuna ajali moja tu ya ndege tena ni eneo pembeni kidogo imewahi kuripotiwa na hakuna pengine popote imewahi kurekodiwa kuwa kuna ndege/meli imewahi kupotea maeneo hayo..
so ni uwongo tu..

Mkuu napenda sana kuckia habar ya ile triangle ambako ndege uvutwa
 
Mkuu napenda sana kuckia habar ya ile triangle ambako ndege uvutwa

ndo hiyo inaitwa bermunda triangle.. ni uzushi tu.. wazungu wameuza vitabu, wamecheza muvi nk. they make a lot of money out of that myth.. si kweli.. ni kama hadithi za nguva (samaki mtu)
 
ndo hiyo inaitwa bermunda triangle.. ni uzushi tu.. wazungu wameuza vitabu, wamecheza muvi nk. they make a lot of money out of that myth.. si kweli.. ni kama hadithi za nguva (samaki mtu)

Eti ndo kama nungwi hvi maji yanaingiia hapo
cjui mkipita ukiwa macho unapotea.
 
Sasa mbona hadithi yako haisemi kama na hao abiria wenzako hiyo hali walikuwa wanaiona au ni ww tu???????
 
Conciparancy iliyopo hapo inaaminika kuna Allien station hapo chini kwani miaka mingi iliyopita evidence inaonyesha kuna meteorite ilianguka hapo lakini mpaka leo haijapatikana so watu wanahusisha na alliens activities
 
Uko ndani ya ndege. Kukiwa na utulivu mkubwa ambapo watu wengi wanaonekana kusinzia. Umejiegemea kwenye seat yako ukitafakari hili na lile.. Ghafla unaskia sauti ya kilio cha mtoto mchanga kwa mbali.. unageuka huku na kule na unajiridhisha sauti ile unayoiskia haitoki ndani ya ndege bali nje.

Unajiuliza mara mbili mbili.. unashangaa . Ghafla unajiskia ulazima wa kwenda haja ndogo, unapokaribia mlango wa choo unaanza kuhisi mle ndani ya choo kuna nyoka kibao. Unajipa ujasiri na kufungua mlango, mlango haufunguki. Unasukuma tena kwa nguvu mlango bado haufunguki.

Unapata hisia kuna nyoka mkubwa yuko mlangoni ndio maana mlango haufunguki.Unaamua kuahirisha tukio unarudi kukaa kwenye kiti chako, ile kukaa tu unakutana na boonge la mtikisiko (turbulent). unaanza kuhisi ndege inadondoka…unaangalia saa..ni saa 5 usiku na bado kuna kama masaa matano kabla ya ndege kutua.

Unafungua dirisha kuangalia nje ni giza totoro, unachokishuhudia nje ni mvua kubwa na radi, pia sauti ya kilio cha kitoto kichanga inasikika zaidi. Isitoshe unaskia mshindo mkubwa kwa mbali. Haraka unafunga dirisha.Unaamua kupambana na hofu kwa kujiimbisha,…Mbinguni..kuna makao mazuri sana.

unaangalia pembeni unajistukia umekuwa ukiimba kwa sauti kiasi cha kuwaamsha baadhi ya abiria wenzako ambao wanakuangalia kwa jicho la kukushutumu na pia unajistukia ni kama wimbo wenyewe unakusuta vile kwa mazingira uliyonayo. Unajaribu kupotezea kwa kujichekesha lakini sauti inayotoka inakuwa ya ajabu kutokana na hofu uliyonayo.

Unaacha kuimba na kuiruhusu hofu iliyokushika itawale. Unawasha kitv unaangalia geographical location ulipo… ramani inakuonesha unapita kisiwa cha Bermuda.Kijasho chembamba kinakutiririka japo kuna AC. Unatamani ushuke.

Uongo mtupu.
 
Kuna documentaries zinazoelezea juu ya Bermuda triangle na visiwa vyake kwa undani zaidi.
Kama ukiweza kuzipata utapata majibu yote juu ya Bermuda
 
Back
Top Bottom