Lulu sasa abadilishiwa mashtaka

Haina haja ya kuchezea watu akili wamuachie tuu ...hata mie napenda wamuachie maana kesi yake inahusiana na issue za mapenzi sasa mungu ndio anajua ukumu ya hilo sio mahalama za kwetu duniani.

Asante.
 
DUH
hii nayo ni kali ya mwaka na pengine ndiyo ya kufungia mwaka na kama ikiendelea hali hii kuna wakati bastora zitalia nje nje
 
Kwani kwenye criminal case burden of proof iko upande upi??? Ukishajua hilo utajua kwanini dpp kajishtukia mapema maana ilikuwa ile kwao mapema........
 
Kikao kijacho cha mahakama lazima nikutoe kwa dhamana. Mapumziko yetu China. Nikupe pole kwa kutenganishwa na sisi kwa siku zote hizo. Mzee wako tutapita kumsalimia. Hii itakusaidia kuwaepuka paparazi wa bongo kwa muda mpaka wazoee kuwa kwako nje ya gereaza. Pole honey kwa yooote. Maisha ni hatua.

sawa mkuu wewe mtoroshee mbali hakisha kuwa huru, make mapapaladhi wa Dar noma watamfuata hata nyumbani so itakuwaq kama bado tu yuko gerezani
 
Sawa kabisa DPP amechelewa sana kufanya maamuzi, tatizo ninaloliona hapo ni kwamba kesi nyingine a aina hiyo ina cheleweshwa sana
 
Mimi sioni kama kuna ukiukwaji wa sheria uliofanywa na Mkurugenzi wa Mashtaka, mshtakiwa hufunguliwa shtaka kulingana na ushahidi uliopo, kama DPP hana ushahidi unaoweza kuthibitisha kwamba Lulu ameua kwa makusudi na aliua bila ya kukusudia kuna haja gani ya kuendelea kumshtaki Lulu kwa mauaji ya kukusudia. Ukiangalia jinsi tukio lenyewe lilivyotokea ni wazi kwamba kuna ugumu kwa DPP kuweza kuthibitisha mauaji ya kukusudia. Ni mamlaka yake na nakubaliana nae kwa kitendo hichi cha kubadilisha shtaka. Hakuna mamlaka yoyote ya Mahkama yaliyoingiliwa hapo.

1. Mkuu umeelewa muanzisha maada alichomaanisha?
2. Umesoma post yako na kuelewa ulichoandika?

I doubt neither of the above:D
 
Tujadili ya maana wana board.... wakwale nawaona macho njeeeeeeee, Chezea pesa na WAKUBWA WEWEEE....
 
Akitoka, akina Shigongo, Ruge na Kusaga watamdaka na kutulipisha viingilio Dar live kumwona tu.

Washajua lini atatoka na booking tayari.
 
UKWELI KIFO CHA KANUMBA: ACP. Charles Kenyela athibitisha kifo cha Steven Kanumba


a. songeayetu.blogspot.com
Kamanda wa polisi wa mkoa wa kipolisi wa Kinondoni leo mapema asubuhi ameweza kuthibitisha kutokea kwa kifo cha msanii maarufu wa filamu nchini Tanzania Steven Kanumba (Uncle JJ). Kamanda Kenyela alisema kuwa tukio la kifo cha Kanumba limetokea usiku wa kuamkia leo tarehe 7 Aprili 2012. Kutokana kifo hicho cha ghafla cha msanii huyo jeshi la polisi linamshikilia mtu mmoja ambaye inasadikika kuwa alikuwa ni mpenzi wake na marehemu.


Kamanda Kenyela alisema kuwa taarifa za awali zilizopatikana ni kwamba marehemu alimpiga mpenzi wake kutokana na wivu wa kimapenzi ambapo taarifa hizo zilipatikana kutoka kwa ndugu yake marehemu ambaye walikuwa wakiishi pamoja. Baadaye ndugu yake huyo alipofuatilia zaidi alimwona marehemu akiwa katika hali mbaya, na kwenda kutoa taarifa polisi. Kamanda huyo amedai kuwa Polisi walipofika katika eneo la tukio walimkuta Kanumba tayari ameshakata roho.


Polisi waliweza kuuchukua mwili na kuupeleka hospitali kwa ajili uchunguzi zaidi kuhusiana na tukio hilo. Kuhusiana na undani wa kifo hicho Kamanda ameomba kupewa nafasi zaidi kuhusiana na uchunguzi, kwani taarifa nzuri za kifo hicho zitatolewa na wataalam (madaktari) ambao wanaendelea na uchunguzi na baada ya uchunguzi ataweza kutoa jina la mwanamke ambaye anashikiliwa na jeshi la polisi ambaye ataweza kusaidia kueleza mazingira ya kutokea kwa kifo hicho.


Mwisho, Kamanda Kenyela aliweza kuwapa pole Watanzania wote kwa ujumla na nje ya Tanzania kwa watu wote kutokana na kifo cha msanii ambaye alikuwa kioo cha jamii.
images
 
Ameepuka mustakabali wa kunyongwa.

Sijui kama kuna kutanabahisha tofauti ya mustakabali na adhabu katika uandishi wetu.
Mkuu, "mustakabali" nadhani maana yake ni "future," sio? Kama ndivyo badi sidhani kama unaweza hata kusema "ameepuka future ya kunyongwa" kwa sababu hakuna anaejua kwamba asingefutiwa mashitaka angekutana na future ya kunyongwa.

Lulu ameepuka uwezekano wa kuhukumiwa kunyongwa. Simple as that.

Na sidhani kama mwandishi wa kawaida wa gazeti kama la MWANANCHI anaelewa tofauti yake, au whether wanajali.
 
Naona umehamaki kutoa lalamiko ambalo ujalifanyia uchunguzi!!Ebu tafuta kwanza historia ya marehemu kwa undani yeye binafsi kiafya kabla ajafa kisha, kisha chuku evidence za tukio umganisha na taarifa za marehemu za kiafya kabla ya tukio binafsi ninekuwa mimi NAMFUNGULIA LILY MLANGO KWAHERI BINTI KAWASALIMIE KWENU!!ONYO KWANGU INGEKUWA ACHANA NA MAHUSIANO NA WATU WAZIMA SANA KUKUZIDI UMRI MARA 30 YAKE.

Najua Serikali ya Jamhuri ya Muungano inafanya kazi zake kwa umakini,na atimae sheria itachukua mkondo wake na KUMUACHIA huyo binti,akaendelee na maisha yake!!!
 
Hii nayo habari ya kisiasa?

Au kuna wanasiasa wanahusika na haya maamuzi....?!?
 
kanumba angekuwa ndugu yenu mngejadili kwa utulivu huu,hapa hakuna hata mmoja anayejua ukweli,lulu aweza kuwa na hatia au asiwe nayo.
 
Mimi sioni kama kuna ukiukwaji wa sheria uliofanywa na Mkurugenzi wa Mashtaka, mshtakiwa hufunguliwa shtaka kulingana na ushahidi uliopo, kama DPP hana ushahidi unaoweza kuthibitisha kwamba Lulu ameua kwa makusudi na aliua bila ya kukusudia kuna haja gani ya kuendelea kumshtaki Lulu kwa mauaji ya kukusudia. Ukiangalia jinsi tukio lenyewe lilivyotokea ni wazi kwamba kuna ugumu kwa DPP kuweza kuthibitisha mauaji ya kukusudia. Ni mamlaka yake na nakubaliana nae kwa kitendo hichi cha kubadilisha shtaka. Hakuna mamlaka yoyote ya Mahkama yaliyoingiliwa hapo.

LET'S DO AS FOLLOWS:

1. Mwanzo wa mashtaka ni tuhuma za mauaji(murder).

2. Tuhuma hizo zinatakiwa zithibitishwe beyond reasonable doubt mbele ya mahakama.

3. Ili kuprove and disprove allegations za murder,must be done in court.

4. After proof of beyond reasonable doubt (or disproof), the court has to convict the accused of the guilty of murder, otherwise the court may rest itself to manslaughter....(ask why manslaughter).
 
Mkuu, "mustakabali" nadhani maana yake ni "future," sio? Kama ndivyo badi sidhani kama unaweza hata kusema "ameepuka future ya kunyongwa" kwa sababu hakuna anaejua kwamba asingefutiwa mashitaka angekutana na future ya kunyongwa.

Lulu ameepuka uwezekano wa kuhukumiwa kunyongwa. Simple as that.

Na sidhani kama mwandishi wa kawaida wa gazeti kama la MWANANCHI anaelewa tofauti yake, au whether wanajali.

Uwezekano wa kuhukumiwa kunyongwa ulikuwa katika past au future yake?
 
Back
Top Bottom