LOWASSA kila akisimama Bungeni kuongea,BUNGE huzizima kwa Nderemo hii inashiria nini?

sokoinei

JF-Expert Member
Feb 27, 2012
1,832
566
Mbunge wa Monduli na Waziri mkuu aliejiuzulu kwa kashfa ya Richmond Edward Lowassa ni miongoni mwa wabunge wachache ambao ni nadra sana kumsikia au kumuona akizungumza au kuchangia hoja bungeni.
Tangia kujiuzulu kuwa Waziri mkuu mwaka 2007 Mh Lowassa hajawahi kuchangia kwa kuongea hoja bungeni zaidi ya mara mbili.

Lowassa km tumjuavyo sio mtu muongeaji sana na hata hoja nyingi bungeni huchangia kwa maandishi,lakini amekuwa akiongea kwa kupitia media mbalimbali na ktk matamasha na harambee huku akijiita kuwa yeye sio mtu wa maneno ila ni wa vitendo.
Sijajua kwanini mh Lowassa hukwepa kuongea Bungeni lakini hupenda kuongea na waandishi wa habari. Km ktk kile kipindi cha Semenyu wa ITV kinachorushwa kila Jumatatu saa 3:00 usiku.

Tangia kujiuzulu kwa Mh Lowassa binafsi niliwahi kumsikia akiongea bungeni mara mbili. Na mara zote baada tu ya kusimama utasikia baadhi ya Wabunge wakimshangilia. Mara ya kwanza ni pale alipotoa kauli akiishauri serikali ichukuwe MAAMUZI MAGUMU.
Mara ya pili ni jana wakati akimuunga mkono waziri LUKUVI ktk hoja iliyoibuka baada ya Mbunge wa Cdm Susan Liymo kuuliza swali kuwa ni lini serikali itawaleta nchini wataalamu wa kutengeneza na kuzuia mvua nchini km ilivyoahidi?
Akijibu swali hilo waziri Huviza aliwataka wananchi wasidanganyike kwa kuwa hakuna mwarobaini wa kuzuia na kutengeneza mvua isipokuwa ni kutunza mazingira.

Kauli hiyo ilimfanya Lukuvi kusimama na kusema,ni kweli Waziri mkuu aliejiuzulu(Lowassa) aliwahi kufanya ziara nchini Thailand na sio Malesia km Waziri Huviza na Susan walivyodai.

Lukuvi alisema kuna utaalamu huo na Lowassa aliwaomba wataalamu hao waje kufundisha wataalamu wa Tanzania teknolojia hiyo lakini ilishindikana kutokana na Tanzania kutokuwa na fedha.
Hata hivyo Mwenyekiti wa bunge Jenister Muhagama aliwataka mawaziri hao kukutana kupata jibu sahihi maana wananchi hawajui nani anasema ukweli.

Wakati Muhagama akitoa maelekezo hayo ndipo aliposimama Mh LOWASSA na kusababisha Bunge kulipuka kwa shangwe. Lowassa alisema; "Alichokisema Waziri William Lukuvi ndicho sahihi" akamaliza na kukaa.

Kushangiliwa kwa Lowassa kila mara anaposimama kuzungumza bungeni je inaashiria nini? Au kwa kuwa sio kawaida yake kuzungumza kwa hiyo kila mbunge anataka kusikia atakachozungumza?
 
Anashangiliwa na Beatrice Shelukindo tu mbunge wa Hanadeni na aliwahi kwenda kwake (lowassa) huko monduli akala na chakula , huyu mwanamke ana kihelehele sana utafikiri mmewe hamtoshelezi
 
Mbunge wa Monduli na Waziri mkuu aliejiuzulu kwa kashfa ya Richmond Edward Lowassa ni miongoni mwa wabunge wachache ambao ni nadra sana kumsikia au kumuona akizungumza au kuchangia hoja bungeni.
Tangia kujiuzulu kuwa Waziri mkuu mwaka 2007 Mh Lowassa hajawahi kuchangia kwa kuongea hoja bungeni zaidi ya mara mbili.

Lowassa km tumjuavyo sio mtu muongeaji sana na hata hoja nyingi bungeni huchangia kwa maandishi,lakini amekuwa akiongea kwa kupitia media mbalimbali na ktk matamasha na harambee huku akijiita kuwa yeye sio mtu wa maneno ila ni wa vitendo.
Sijajua kwanini mh Lowassa hukwepa kuongea Bungeni lakini hupenda kuongea na waandishi wa habari. Km ktk kile kipindi cha Semenyu wa ITV kinachorushwa kila Jumatatu saa 3:00 usiku.

Tangia kujiuzulu kwa Mh Lowassa binafsi niliwahi kumsikia akiongea bungeni mara mbili. Na mara zote baada tu ya kusimama utasikia baadhi ya Wabunge wakimshangilia. Mara ya kwanza ni pale alipotoa kauli akiishauri serikali ichukuwe MAAMUZI MAGUMU.
Mara ya pili ni jana wakati akimuunga mkono waziri LUKUVI ktk hoja iliyoibuka baada ya Mbunge wa Cdm Susan Liymo kuuliza swali kuwa ni lini serikali itawaleta nchini wataalamu wa kutengeneza na kuzuia mvua nchini km ilivyoahidi?
Akijibu swali hilo waziri Huviza aliwataka wananchi wasidanganyike kwa kuwa hakuna mwarobaini wa kuzuia na kutengeneza mvua isipokuwa ni kutunza mazingira.

Kauli hiyo ilimfanya Lukuvi kusimama na kusema,ni kweli Waziri mkuu aliejiuzulu(Lowassa) aliwahi kufanya ziara nchini Thailand na sio Malesia km Waziri Huviza na Susan walivyodai.

Lukuvi alisema kuna utaalamu huo na Lowassa aliwaomba wataalamu hao waje kufundisha wataalamu wa Tanzania teknolojia hiyo lakini ilishindikana kutokana na Tanzania kutokuwa na fedha.
Hata hivyo Mwenyekiti wa bunge Jenister Muhagama aliwataka mawaziri hao kukutana kupata jibu sahihi maana wananchi hawajui nani anasema ukweli.

Wakati Muhagama akitoa maelekezo hayo ndipo aliposimama Mh LOWASSA na kusababisha Bunge kulipuka kwa shangwe. Lowassa alisema; "Alichokisema Waziri William Lukuvi ndicho sahihi" akamaliza na kukaa.

Kushangiliwa kwa Lowassa kila mara anaposimama kuzungumza bungeni je inaashiria nini? Au kwa kuwa sio kawaida yake kuzungumza kwa hiyo kila mbunge anataka kusikia atakachozungumza?

Wote wanaomshangilia wamelipwa tayari....
 
Anashangiliwa na Beatrice Shelukindo tu mbunge wa Hanadeni na aliwahi kwenda kwake (lowassa) huko monduli akala na chakula , huyu mwanamke ana kihelehele sana utafikiri mmewe hamtoshelezi
kifungu alichoambiwa Adamu na Eva kinamtetea kisemacho: zaeni muongezeke mkaijaze nchi yote!!!
 
inaashiria kuwa huyo ndio chanzo cha umasikini wetu katika kipindi cha miaka hii 8
 
hii inashiria kwa jinsi gani bungeni mna watu wasiojua kujenga uchumi wala kuitangaza nchi yetu kidiplomasia. humo bungeni sijawahi kabisaa kusikia wabunge wakilalamikia kuwa kuna shule za msingi zilizoezekwa kwa Nyasi na vyoo vya kuchimba vinukavyo!! sijawahi kuwasikia wakilalamikia ukosefu wa ajira! wao bado wana ule moyo wa ukomunisti wa kuitikia ndiyoooooooo, juuuu, juuuu, juuuuuuzaidi!! wabongo hapo tumeliwa kweli kweli!!!!
 
Ukiwa mwanasiasa mtaji wako ni watu/wapiga kura. Ndoto ya kila mwanasiasa ni kuwa top leader,hata makazini kila mfanyakazi anataka siku moja aje kuwa mkurugenzi etc, kwahiyo hao wanaoshangilia ni mtaji wake kisiasa wala sio dhambi.
 
SIIPENDI CCM ILA WAKIMSIMAMISHA LOWASA 2015 KAMA MGOMBEA URAISI BASI KURA YANGU WAMEPATA.NINA IMANI LOWASA NI BONGE LA KIONGOZI NA ANAWEZA KUKEMEA NA KUKATAZA HATA KUFANYA MAAMUZI MAGUMU.NCHI YETU KWASASA ILIPOFIKIA INAHITAJI VIONGOZI WAKALI WATENDAJI NA WAFUATILIAJI.WENGINE WANAOWEZA KUPATA KURA YNG PALE CCMAGAMBA NI MAGUFULI NA MZEE WA MADAWA!! aka(mwakyembe) NJE NA HAO MM NI CDM WALA C MLIBERALI
 
Back
Top Bottom