Lowassa azingirwa na polisi nyumbani kwake Monduli ashindwa kwenda kumnadi mgombea

Status
Not open for further replies.

Jembe Jembe

JF-Expert Member
Jun 9, 2016
749
1,797
Katika kuonyesha kuwa CCM inahofu katika uchaguzi mdogo wa madiwani, magari zaidi ya 10 ya jeshi la Polisi mkoa wa Arusha yamezunguka nyumba ya Lowasa ambae ni waziri Mkuu mstaafu na kuzuia msafara wa Magari na pikipiki kuelekea kata ya Musa wilaya ya Arumeru kumnadi mgombea udiwani.

Tukio hilo limejiri Leo j3 kuanzia majira ya SAA 9 alasiri ambapo Polisi wenye silaha na mabomu walitanda nyumbani kwa Lowassa Monduli, kwa lengo la kumzuia asiende kwenye Mkutano wa kampeni kumnadi mgombea udiwani.

Aidha wafuasi wa CHADEMA waliomfuata kumpokea wakiwemo viongozi walizuiwa na Polisi huku Katibu mwenezi wa jimbo John Seneu au Jombii akitiwa mbaroni na Polisi.

Hatua hiyo inaelezwa kuwa ni hofu kwa CCM zinazopelekea kutumia vyombo vya dola vibaya
f8775fb7044eab05cc17dfd84f699c7a.jpg
Kudhibiti siasa za CHADEMA kwa maslahi ya wagombea wa CCM, huu ni uonevu mkubwa kwa mustakabali wa taifa letu na unapashwa kukemewa na kulaaniwa.
 
Hivi hawa pimbi wana nini jamani na hao raia?
Edo keshawakimbia, wanataka nini...
Hizi siasa za wakati huu ni pasua kichwa sana!
Sitokaa niipende na wala kuichagua hii kijani katika maisha yangu...
Nakichukia sana hiki chama, nimetokea kuwachukia sana hata wanachama wake kwa haya mambo ya kibozozo yanayofanywa na dola yake!
Halafu linatokea jinga huko lumumba linajidai lina uzalendo...
Malabuku .....
 
Katika kuonyesha kuwa Ccm inahofu katika uchaguzi mdogo wa madiwani ,magari zaidi ya 10 ya jeshi la Polisi mkoa wa Aeusha yamezunguka nyumba ya Lowasa ambae ni waziri Mkuu mstaafu na kuzuia msafara wa Magari na pikioiki kuelekea kata ya musa wilaya ya Arumeru kumnadi mgombea udiwani.

Tukio hilo limejiri Leo j3 kuanzia majira ya SAA 9 alasiri ambapo Polisi wenye silaha na mabomu walitanda nyumbani kwa Lowasa Monduli, kwa lengo la kumzuia asiende kwenye Mkutano wa kampeni kumnadi mgombea udiwani.

Aidha wafuasi wa chadema waliomfuata kumpokea wakiwemo viongozi walizuiwa na Polisi huku Katibu mwenezi wa jimbo John Seneu au Jombii akitiwa mbaroni na Polisi.

Hatua hiyo inaelezwa kuwa ni hofu kwa Ccm zinazopelekea kutumia vyombo vya dola vibaya
f8775fb7044eab05cc17dfd84f699c7a.jpg
kudhibiti siasa za chadema kwa maslahi ya wagombea wa Ccm ,huu ni uonevu mkubwa kwa mustakabali wa taifa letu na unapashwa kukemewa na kulaaniwa.
kama hii ni kweli wengi watamhurumia Lowasa kwa njia tofauti
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom