Lipumba kukutana na wanachuo Dodoma..kuzungumzia uchumi wa Taifa na Dunia karibuni wote

Topical

JF-Expert Member
Dec 3, 2010
5,173
935

Wanafunzi wa vyuo vikuu vya Dodoma wameomba kukutana na Mwenyekiti wa Chama cha wananchi (CUF), Prof Ibrahimu Lipumba ili kujadili kuyumba kwa uchumi wa taifa na kulitafutia ufumbuzi suala hilo.
Hayo yalibainishwa juzi na Naibu Katibu Mkuu wa CUF, Julius Mtatiro alipokuwa akizungumza na wanafunzi kutoka katika chuo kikuu cha Dodoma (Udom), Chuo cha biashara (Cbe), Chuo cha Mipango pamoja na Chuo cha Mtakatifu John.Naibu Katibu Mkuu huyo alisema baada ya kuzungumza na wanafunzi hao wa vyuo vikuu na kutambua umuhimu wa uchumi wa taifa maombi hayo wameyapokea na kwamba Prof Lipumba atafanya kongamano na wanafunzi hao kujadili masuala ya kuyumba kwa uchumi na mfumuko wa bei uliopo sasa.“Baada ya kusikiliza maombi ya wanafunzi wa vyuo vikuu na kwa kuona jinsi hali ya uchumi ilivyo mbaya kwa sasa tumeamua kuandaa kongamano ambalo Prof Lipumba atazungumza na wanafunzi hawa ili kulitafutia ufumbuzi suala hili,” alisema Mtatilo na kuongeza “Suala hilo linatarajiwa kufanyika hivi karibuni baada ya mtaalamu huyo wa uchumi kulejea nchini hivi karibuni kutoka Marekani,” alisema.Mtatilo alisema kwa sasa hali ya uchumi inazidi kuwa mbaya baada ya kuongezeka kwa mfumuko wa bei jambo ambalo linazidi kufanya maisha ya watanzania kwa magumu.“Kiukweli suala la uchumi na mfumuko wa bei linatakiwa kutafutiwa ufumbuzi kwani jinsi hali ilivyo sasa inatisha ndio maana hata wasomi wameliona jambo hili na kutaka kutafutiwa ufumbuzi wa haraka,” alisemaKatika hatua nyingine Naibu Katibu Mkuu huyo alisema wanafunzi hao pia wameomba kukutana na Makamo wa kwanza wa Rais wa Zanzibar ilikuwapa mafunzo ya siasa na utawala bora.“Wanafunzi hao pia wameoma kukutana na Makamo wa kwanza wa Rais wa Zanzibar ili kuwapa mafunzo ya siasa na utwala bora jambo ambalo ni la msingi kwa maendeleo ya Taifa,” alisemaKatika Mkutano huo ambao ulihuhuliwa na wanafunzi 60, wanafunzi 23 walichukua kadi za chama hicho.20 february,2012
 
tunahitaji kujikita kwenye ujasiriamali kabla ya kuingia kwenye macro economics

michicha na kisamvu vimekosa masoko
 
Vizuri lakini liwe kongamano la uchumi na siyo la siasa za kibongo zinazoishia vurugu na maandamano yasiyo na tija na kupoteza dhana nzima ya kongamano. Hivi prof amekuwa mpya au ni yuleyule tunaemjua aliyemshauri Mzee mwinyi na kushindwa kabisa katika nyanja ya uchumi kwa kuingia katika trade liberalization pasipo kuwa na control ys inflation uchumi wenye udalali?
 
Akajenge chama chake asituletee lecture hapa! Of course ni Prof wa uchumi na anajua kuelezea uchumi kweli! Lakini ukombozi tunaoutaka si lecture zake za uchumi!
 
Eti wamemuomba!!!!!!!!! makamu wa pili wa rais nchi jirani ya zanzibar@ kwiii kwiiii kwii kwiii
 
huo ndo wajibu wake kwenye siasa alijichanganya..ubovu ni kwamba kwenye siasa hatumii hata robo ya utalamu wake zaidi ya kuwarubuni wananchi...
 
Sisi hatutaki u prof wakuandika vitabu na ku publish paper ambao utekelezaji wake ni zero kama lipumba ndiye aliyekuwa anamshauri mzee mwinyi na wote tuliyaona madudu ya kipindi kile hali ilivyokuwa mbaya kwa serikali huo uchumi wake wa kwenye vitabu hauna maana bora aende akafundishe vijana wetu hafai kuwa hata mjumbe wa nyumba kumi pamoja na hayo ma gpa yake yeye ni kilaza tu kwenye implementation
 
Back
Top Bottom