Lazima tukazikwe "nyumbani"?

ngoshwe

JF-Expert Member
Mar 31, 2009
4,131
931
Kwa wale tunaofuata imani ya kristo , tunasoma na kuamini kuwa:

“Mwanadamu aliyezaliwa na mwanamke siku zake za kuishi si nyingi, naye hujaa taabu. Yeye huchanua kama vile ua, kasha hukatwa; Hukimbia kama kivuli, wala hakai kamwe… (Ayubu 14:1-2,14).

Mistari hii inatukumbusha kila machweo na pambazuko kuwa pamoja na taabu na mashaka mengi, au raha nk hapa duniani, ijapo siku tutakufa, tutakufa kwa kupenda au tusipopenda. Kifo kimeandikwa , iwe ni wa imani ya dini au mpagani (mtu asieamini katika dini yeyote ile).

Pamoja na kujua kuwa kifo kipo na kinatokea siku tusioijua, kuna badhii ya watu katika jamiii wanaimani pia katika mila za kuwa ukifa ni sharti ukazikwe katika udongo wa eneo la asili ya kizazi chako ( wanaita "nyummbani").

Kwa kuweka msisitizo wa kauli zao, baadhi yao wanadiriki hata kuacha wosia kwa ndugu na familia kuwa " tafadhali sana mimi nikifa, ni lazima nikazikwe nyumbani"


Pengine unakuta mtu huyu amekuwa akiishi mbali sana na huko "nyumbani "katika maisha yake yote na kabla ya umauti haujamfika alikuwa na mali na kipato kizuri sana cha kumwezesha kujenga mazingira ya yeye siku akifa "akazikwe nyumbani" lakini hakutunza hata sehemu moja ya mali zake za kuwezesha safari hiyo ya nyumbani.

Inapofika siku ya kifo cha mtu wa jinsi hii, na kwa kuzingatia baadhi ya imani za kimila na desturi za baadhi ya makabila yetu (...), inakuwa ni "lazima kutekeleza kauli ya marehemu" kwani marehemu huwa inaaminika ana nguvu kuu hata za kusambaratisha milima iwapo kauli alizohusia hazitatekelezwa (ni imani!!).,

Ikiwa familia ni maskini, na haiwezi kabisa hata kukamuana kuweza kusafirisha msiba kwenda huko "nyumbani", hali inakuwa ngumu zaidi na kama itawezekana, basi pengine inaishia kwa kuiweka katika umaskini mkubwa mno labda hata kwa kuuza mali zote ambazo zingeweza kuisaidia familia iliyoachwa na marehemu ili kutimiza "agano" na marehemu...la kumfikisha huko "nyumbani".

Ikiwa tunaamini kifo kipo na tunataka tukazikwe huko "nyumbani" ambapo pengine hata hatukuishi wala kujenga huko katika uhai wetu, kwa nini basi tusijiandae kwa hilo ili kuwatokuwaongezea umasikini na majonzi zaidi kwa wale ambao tunawaacha hapa duniani baada ya sisi kuondoka???.
 
Actually , this is a very pressing matter all over the world!

Imani hizo zipo na nina imani wengi wetu (hapa JF) tuna mawazo hayo na tunaamini kabisa kwamba tukipelekwa kuzikwa kwetu tunaungana na ndugu zetu waliozikwa tangu kale!..Kwa makabila makubwa kama Wahaya,Wachaga na Wanyakyusa, mtu hazikwi mbali na kwao, regardless ya umbali wa mtu huyo anapofia!

Ni wachache sana (kama wapo)wanaokumbuka kufacilitate ishu ya kuufikisha mwili wake makwao pindi atakapokufa!...

Kama mtu alikuwa na uwezo, basi kiasi cha mali zake kinaweza kusaidia hilo, lakini, asilimia 95 huwa ni kushikana mashati na kukamuana kama ulivyosema...Angalau kama marehemu alikuwa mtumishi wa mahali fulani inasaidia, maana mara nyingi organisation zinakuwa na sera ya kumrudisha mtu 'place of Domicile.

Kuna mtu kijijini kwangu alichonga sanduku ambalo alidai azikwe humo pindi akifa, watu walimwona kama mchuro, wazee wakamwita ajibu shauri hilo, na hatimaye sanduku hilo lilivunjwavunjwa!
 
nimeona kuna jukwaa la dini hapa, kwa nini usipeleki hii kitu huko?
 
Kwa vile hakuna aijue siri ya kifo mie sidhani kama ni lazima ..ila tunafanya yote haya kudumisha mila
 
Kwa vile hakuna aijue siri ya kifo mie sidhani kama ni lazima ..ila tunafanya yote haya kudumisha mila

Hapo nimekuelewa mama wa kwanza.

Wazee wa kudumisha mila lazima tudumishe mila.

Jamani mimi nikiresti in piis mkanizike kwetu.........................
 
Hapo nimekuelewa mama wa kwanza.

Wazee wa kudumisha mila lazima tudumishe mila.

Jamani mimi nikiresti in piis mkanizike kwetu.........................

Kama huna fungu mzee yu might leave others in troubles while ur resting in Piis.
 
Actually , this is a very pressing matter all over the world!

Imani hizo zipo na nina imani wengi wetu (hapa JF) tuna mawazo hayo na tunaamini kabisa kwamba tukipelekwa kuzikwa kwetu tunaungana na ndugu zetu waliozikwa tangu kale!..Kwa makabila makubwa kama Wahaya,Wachaga na Wanyakyusa, mtu hazikwi mbali na kwao, regardless ya umbali wa mtu huyo anapofia!

Ni wachache sana (kama wapo)wanaokumbuka kufacilitate ishu ya kuufikisha mwili wake makwao pindi atakapokufa!...

Kama mtu alikuwa na uwezo, basi kiasi cha mali zake kinaweza kusaidia hilo, lakini, asilimia 95 huwa ni kushikana mashati na kukamuana kama ulivyosema...Angalau kama marehemu alikuwa mtumishi wa mahali fulani inasaidia, maana mara nyingi organisation zinakuwa na sera ya kumrudisha mtu 'place of Domicile.

Kuna mtu kijijini kwangu alichonga sanduku ambalo alidai azikwe humo pindi akifa, watu walimwona kama mchuro, wazee wakamwita ajibu shauri hilo, na hatimaye sanduku hilo lilivunjwavunjwa![/COLOR]



Na hzi imani mzee tabu tupu...wengine wanaamini kujiandaa kwa kifo ni Uchuro wakati huo huo wanaweka wosia mzito wa usumbufu mkubwa kwa wale wanaobaki duniani...
kuwa wakazikwe nyumbani ili hali akipata akiwa na mali anafunja na wengine akiwa katika karibu kufa ndo anatandika mpka senti ya mwisho kwa staili ya ponda mali kufa kwaja.

sijajua kama mbinguni/ kwa Mungu ni "angani" au chini ya "ardhi"
na kama ukizikwa kule Kyela au Kanyigo, ngazi ya kuingia ipo straight....
 
haya mambo sana yanakuja kutokana na wish-jinsi mtu anapendelea, tatizo llinalokuwepo ni kwamba watu wengi wanakuwa hawajiandai mapema. mungu akibariki na kunipa nafasi na uwezo mwakani nitajenga kabisa pango shambani kwangu (mkoa tofauti kabisa na kwetu, lakini ndiyo hasa kwangu)
 
haya mambo sana yanakuja kutokana na wish-jinsi mtu anapendelea, tatizo llinalokuwepo ni kwamba watu wengi wanakuwa hawajiandai mapema. mungu akibariki na kunipa nafasi na uwezo mwakani nitajenga kabisa pango shambani kwangu (mkoa tofauti kabisa na kwetu, lakini ndiyo hasa kwangu)
 
Hii dhana ni zuri iwapo tu una maandalizi ya kutosha kabla ya kunyakuliwa na mja. Lakini mantiki hiyo inaweza kuwa ni kero kwa ndugu uliowaacha kama huna maandalizi. Fikiria mtu aliyetoka kwake katika umri wa ujana akachuma mali ya kutosha na akatanua vya kutosha bila kujenga kwao au hata kusalimia huko angalau mara moja kwa mwaka, kisha ukafilisika na baadae ukafariki ghafla na unatakiwa upelekwe huko kwenu kijijini huoni itakuwa kinyaa hata kwa ndugiu zako?
 
Japokuwa Mimi nadhani sio lazima sana kwenda kuzikwa nyumba pale mtu akifa akiwa mbali na nyumbani LAKINI nadhani wakati mwingine ni vizuri mtu akienda kuzikwa nyumbani kwao. Mara nyingine mtu nakuwa mjini lakini sehemu kubwa ya ndugu , jamaa na marafiki zake wanakuwa nyumbani hivyo itakuwa vizuri kuwapa hao wapendwa wake nafasi ya mwisho ya kumwona(japo ni mfu) na kumzika.
 
Faida zakuzikwa kwenu;
1. Jamaa ndugu wengi watapata fulsa ya kukuaga.
2.kuna watu hawaendi kwao au ndugu hawakutani hadi msibani,hii itasaidia kufika kwenu .
3.kaburi linapokuwa kwenu kunakuwa na kumbukumbu nzuri zaidi.

Hasara za kuzika kwenu;
1.gharama ni kubwa.
2.wakati fulani mwili hufika ukiwa umeharibika sana.
3.mara nyingi kwa vile ndugu wote wapo,suala la urithi huanza,kwa vile ndio kwanza
marehemu kazikwa utakuta watu huwa haafikiani.
 
Kufa ni kufa kaburi ni hifadhi tu. Wanaozama na meli na kama waliacha usia wakahifadhiwe makwao inasomekaje?
 
inaprndeza ukizikwa kwenu maana kabuli litakuwepo siku zote kumbukumbu tofauti namjini ambapo hawachelewi kuhamisha makabuli kama ambayvo iliwahi kutokea
 
binafsi sioni ulazima, am dead anyway!!

lakini pia wengine taratibu za imani hazituruhusu kufanya hivo......mwisho kusafirisha mwili ni umbali usiozidi saa moja, sasa n ahiz foleni za DSM dont ask me kama naweza kufikishwa mwembe jini on time au ntazikwa njiani!!!
 
Hivi nyumbani ni wapi? ulipozaliwa au unapoishi sasa?

Nyumbani ni kwenu ulikozaliwa, na ni muhimu sana kuzikwa kwenu ili kuweka kumbukumbu ya kaburi lako, maana nje na kwenu hakuna atakayeheshimu hilo kaburi, maana utasikia mala kupitisha barabara, kujenga viwanda na hata nyumba za kuishi.
 
Ni kweli siyo lazima na hasa hasa kama mhusika hakujenga uwezo wa kuhakikisha anasafirishwa.

Kwa upande wangu ningependa nizikwe nyumbani kwetu nilikozaliwa. Naamini ndugu zangu wasioweza kuja mjini watapata nafasi ya kuniaga na kunizika. Pia nitapata nafasi ya kuzikwa karibu na ndugu zangu wa karibu, mfano baba, mama n.k. Ni suala gumu ila hiyo ndiyo wish yangu.
 
Kaitaba mie nikifanya calculations naona possibilities za kuzikwa nyumbani ni ndogo sana... but I would love if my parents or my immediate family members wajekunizika...
 
Back
Top Bottom