Daudi Maginga
New Member
- Jul 10, 2009
- 1
- 0
Tarehe 30 mwezi wa sita, Waziri wa katiba na Sheria aliwasilisha bajeti ya wizara yake kwa mwaka 2009/2010 bungeni mjini Dodoma. Pamoja na mambo mbalimbali aliyoyaeleza kutoka katika hotuba yake, ilikuwa ni pamoja na kuahidi kuifanyia marekebisho ya sheria inayoanzisha shule ya sheria ya mafunzo kwa vitendo yaani Law School of Tanzania.
Sheria ya Tanzania Law School Act ya mwaka 2007 ndio iliyoanzisha shule ya sheria kwa vitendo. Madhumuni ya kuanzishwa kwa shule hiyo ilikuwa pamoja na mambo mengine kutoa mafunzo kwa vitendo kwa wahitimu wa shahada ya kwanza ya Sheria nchini na hii inajumuisha wale waliosoma nje ya nchi ambao wanatakiwa kwa utaratibu wa sasa kipitia mafunzo kwa vitendo katika shule hiyo ya sheria kabla ya kuingia katika ajira rasmi ya utumishi wa umma na nyanja tofauti tofauti.
Sheria hiyo ambayo ilianzisha shule ya mafunzo kwa vitendo imekuwa ikilaumiwa na wadau wengi wa sheria kutokana na mfumo wake mbovu tena usioeleweka hata kidogo. Baadhi ya lawama ambazo wadau wengi wa sheria nchini wamekuwa wakitaka kujua ni ubora halisi wa elimu inayotolewa na shule hiyo, mantiki ya elimu yenyewe na ubovu wa sheria inayosimamia shule hiyo.
Serikali kwa kipindi kirefu sasa imekuwa ikipitisha sheria nyingi zinazowagusa wananchi moja kwa moja pasipo hata kupata maoni ama ushauri wa wadau ili kuboresha sheria husika. Mojawapo ya sheria ambazo zimepitishwa bila kujali maoni ya wadau basi ni hii ya Law School of Tanzania ya mwaka 2007.
Ukiitazama sheria husika, utakubaliana nami kuwa sheria hiyo ilipitishwa kwa kufuata matakwa ama maoni ya kundi flani la watu waliokubaliana kwa maslahi yao binafsi. Imekuwa ni tabia kwa serikali kuanzisha baadhi ya mifumo katika nchi hii pasipo hata kuwa na maandalizi ya kutosha ama kutokufanya utafiti wa kutosha kutoka kwa wenzetu waliopiga hatua katika nyanja husika.
Kwa upeo wangu nilionao nilidhani sheria hii ya shule ya mafunzo ya sheria kwa vitendo ingekuwa ni bora zaidi kuliko ya nchi yeyote ile inayotoa mafunzo ya namna hiyo. Kwa mfano kitivo cha sheria cha chuo kikuu cha Dar es Salaam, ndicho kongwe hapa Afrika Mashariki, kilianzishwa mwaka 1954. Hebu tazama ni takribani miaka 45 tangu mafunzo ya sheria yaanze kutolewa nchini, haiingii akilini eti mpaka mwaka 2007 ndipo ilipoanzishwa shule ya sheria kwa vitendo. Hapo unaweza kuona kuwa kulikuwa na muda mrefu wa kuanzisha mfumo huo kwani kulikuwa na maandalizi ya kutosha na si ubabaishaji unaoekana sasa.
Kwa upande wa Kenya, wao mfumo shule ya sheria kwa vitendo wameanza tangu mwaka 1963. Hivyo basi kwa kuwa wao walikwishaanza muda mrefu, kwetu ingelikuwa sehemu nzuri sana ya kwenda kujifunza wenzetu wamewezaje kufika hapo walipo leo hii. Kwa jambo hili haihitaji hata kuwa profesa ama daktari wa sheria kuweza kulitambua jambo hili. Unaweza kudhani ni utani lakini ndio hali halisi, yapata mwezi wa nne mwaka huu baadhi ya wakufunzi na kaimu mkuu wa shule hiyo walikwenda katika nchi za Kenya na Ghana kwa kile kilichoelezwa kuwa ni ziara ya mafunzo. Hapa unaweza kuona ubabaishaji iweje wapitishe mfumo ambao unagharimu maisha ya wanafunzi pasipo hata kufanya utafiti kabla ya kutunga sheria husika.
Hebu tutazame baadhi ya mapungufu yaliyojitokeza mpaka sasa:
Mosi, Kwa sasa chini ya sheria hiyo ni lazima (mandatory) kwa kila mhitimu wa shahada ya kwanza ya sheria kupita kwanza katika shule ya sheria kwa vitendo ili aweze kuwa na sifa ya kuajiriwa na mashirika ya umma na yale binafsi. Haiwezekani kwa nchi iliyo na uhaba wa wanasheria kama yetu kuweza kuwa na mfumo kama huu kwa sababu kwa utafiti uliofanyika kwa nchi za Kenya na Uganda wao mfumo wa shule ya sheria kwa vitendo si kwa wahitimu wote bali ni kwa wale wanaotaka kuwa mawakili wa kujitegemea pekee na si kama hapa kwetu.
Pili, ubora wa mafunzo. Hapa ndipo kichekesho kinapokuja, mafunzo yanayotolewa katika shule hii ya mafunzo hayana ubora na hayana tija kwa wanafunzi kwani hayana tofauti na yale ambayo wamejifunza walipokuwa wanayasoma katika shahada ya kwanza. Tunaamini ya kwamba tunaposema mafunzo kwa vitendo (Practical training) ni vitendo kweli katika eneo husika na sio kuendeleza dhana ile ile ya mafunzo kwa nadharia (Theory). Ninachokiona katika mafunzo haya na mwendelezo ule ule usio na mantiki wa kufanya masomo kuwa magumu na kuweka mizengwe na fitina zisizo na maana. Wakufunzi wamekuwa wakijali maslahi yao binafsi na siyo yale yanayowaweka pale.
Kwa upande mwingine wakufunzi wa semina wamekuwa ni mzigo usiobebeka na wasio na sifa husika. Walio wengi ni wale ambao ni wanafunzi wanaosomea shahada ya uzamili, wamekuwa hawajui kile wanachokifanya na kuendeleza dhana ya nadharia na ubabe kuliko uwezo halisi wa kisomi.
Mpaka sasa ni aibu kwa serikali na viongozi wanaosimamia shule hii kiasi kwamba hadi hii leo mafunzo haya yamekuwa hayana tija na kukosa mantiki ya uanzishwaji wake. Mafunzo yamekuwa mzigo kwa serikali. Mzigo kwa maana kwamba mfumo wa utoaji mikopo umekuwa ni tatizo na kulalamikiwa na wanafunzi husika huku viongozi wakishindwa kuwasaidia na kutatua tatizo hilo. Kwa mfano wanafunzi wa awamu ya tatu (third Cohort) wamesimamishwa masomo kutokana na matatizo ya mikopo. Kuna habari kuwa watahamishiwa katika kampasi ya Mlimani pindi watakaporejea, hivi hawa viongozi hawatambui wala kuthamini utu wa wanafunzi? Walio wengi wanatoka mikoani na kabla hawajasimamishwa walikuwa tayari wamekwisha kulipia kodi za pango mahala wanapoishi, je kwa huu mkanganyiko nani anawajibika kwa hasara hii wanayopata wanafunzi hawa? Ni ukweli usiopingika kwamba uanzishwaji wa mafunzo haya ulikuwa ni wa kukurupuka.
Utaratibu wa kutahini wanafunzi umekuwa ni ule ule wa mitihani, tena ikiwa imeongezewa ugumu wa makusudi kwa lengo la kufelisha wanafunzi. Kwa mfano matokeo ya wanafunzi wa awamu ya kwanza(first cohort) yaliyotoka hivi majuzi yanaonesha zaidi ya asilimia 73 wamefeli masomo yao. Hapa utashangaa ni wanafunzi hao hao waliomaliza shahada zao za kwanza tena kwa alama za juu, leo hii anaonekana si kitu katika shule hii, hilo kwa mwenye akili timamu halimuingii akilini.
Mgongano wa maslahi ni jambo la tatu linalotia doa mfumo mzima wa mafunzo ya sheria kwa vitendo. Watu wanaounda bodi ya shule hii wamekuwa na mgongano wa maslahi na kazi zao wanazozifanya. Kwa mfano mtu hawezi kuwa mkufunzi wa mafunzo hapo hapo ni mjumbe wa bodi na wakati huo huo ni raisi wa chama cha mawakili Tanzania. Hapo hakuna haki yoyote itakayotolewa kwa misingi ya namna hiyo. Ndio maana bodi hiyo imekuwa ikitoa maamuzi ya ajabu na ubabe usio na weredi hata kidogo na kuendeleza mfumo wa kubeza kila hoja inayotolewa kwa lengo la kufanya maboresho katika shule hiyo.
Pia haiwezekani Dean wa kitivo cha Sheria cha chuo kikuu cha Dar es Salaam kuwa mjumbe wa kudumu wa shule hiyo ya mafunzo ya sheria kwa vitendo. Iweje awe Dean wa chuo hicho pekee kama hakuna ajenda ya siri iliyojificha? Kwa kuwa wanafunzi wa shule hiyo wanatoka katika vyuo mbalimbali nchini, kwanini Dean wa vyuo vyao wasiwe wajumbe wa bodi ama wao hawahusiki? Pia mbona wakufunzi ni hao hao wa chuo kikuu cha dar es salaam na sio wa vyuo vingine? Hapa kuna tatizo, tena si dogo bali ni kubwa na nimeanza kuamini kuwa wakufunzi wa chuo kikuu cha dar es salaam wamefanya mafunzo hayo kuwa mali yao.
Ama kwa hakika ni jambo la kushangaza sana kwa shule hii ya mafunzo ya sheria kwa vitendo ambayo imekuwa ikiongozwa kwa ubinafsi na ubabaishaji wa hali ya juu sana na kaimu mkuu wa shule hiyo. Kaimu huyo hashauriki na pia hajawahi kuongea na wanafunzi wake tangu waingie katika shule hiyo na wamekuwa wanashindwa kutoa maoni yao na dukuduku zao kuhusiana na mfumo mzima wa mafunzo wanayopata.
Ni ukweli usiopingika kuwa kati ya kozi zilizowekewa ugumu, ubinafsi, mizengwe, na umimi wa hali ya juu hapa nchini, basi kozi ya sheria inatia fora. Kwa ujumla kwa yeyote yule ambaye anajitahidi kusoma ili angalau aingie kwenye fani hii anajua jinsi anavyokumbana na vitisho, manyanyaso, uonevu wa waziwazi toka kwa wataaluma wanaofundisha fani hii.
Kwa kumalizia napenda kutoa ushauri kwa viongozi husika na serikali kwa ujumla. Kwanza wanatakiwa kuelewa kuwa wanaharibu mifumo kwa kukosa ushauri mzuri na kutotaka kufuata maoni ya wadau, hivyo basi ni rai yangu kwamba katika mabadiliko ya sheria hiyo wanapaswa kuileta kwa wadau ili watoe maoni yao kwa ajili ya maboresho yenye tija kwa taifa.
Kitu cha pili ni kwamba serikali iwe sikivu na iache kuchezea tena kwa makusudi nguvu kazi ya vijana wenye kiu ya kuitumikia nchi yao kwa moyo wote lakini wanakwamishwa kwa mifumo mibovu inayowekwa. Hivyo basi hakuna haja ya kuendelea kunganganiza wahitimu wote wa shahada ya kwanza ya sheria kusoma mafunzo hayo bali iwe kwa wale wachache tu wanaopenda kuwa mawakili wa kujitegemea pekee.
Jambo la tatu ni kwamba si lazima mafunzo hayo yatolewe Dar es Salaam pekee, naamini ya kwamba mafunzo haya haya kwa nchi za wenzetu kama Australia, wao kila chuo kinakuwa na mafunzo kwa vitendo (Law School). Hivyo basi hapa nchini ingekuwa ni jambo rahisi kuwa na mafunzo haya kwa kila chuo. Hebe tazama vyuo vyote vivavyotoa shahada ya kwanza ya Sheria mahala vilipo kuna mahakama kuu ya Tanzania. Kwa mfano SAUT- Mwanza, RUCO na TUMAINI-Iringa, MZUMBE-Mbeya, Makumira-Arusha, UDSM na TUMAINI tawi la Dar es Salaam. Kwa hakika wanafunzi hao wangepata wasaa mzuri wa kujifunza kwa vitendo.
Masomo hayaeleweki na yamekuwa ya nadharia mno hivyo kukosa mantiki na kushindwa kukidhi matakwa ya kuanzishwa kwake. Tulitegemea wanafunzi wangekuwa wanafanya mazoezi ya vitendo kwa kufanya kesi za kutengenezwa ili mafunzo yawe ya uhalisia zaidi kuliko hali ya sasa ambapo ni nadharia pekee. Kwa sasa mafunzo hayo hayana tofauti na mfumo wa zamani wa internship. Hivyo basi mfumo wote wa mafunzo utazamwe upya ili mafunzo yaweze kuleta mantiki ya uanzishwaji wake.
Nikija katika utaratibu wa kutahini wanafunzi, hapa watanzania hasa wakufunzi inabidi kubadilika, tuondokane na utaratibu wa kutahini wanafunzi kwa kutumia kigezo cha mitihani pekee. Katika sheria mwanafunzi anafundishwa jinsi ya kutafuta sheria na si vinginevyo. Kupitia mitihani huwezi kutambua uwezo binafsi wa mwanafunzi husika ila ni kuendeleza mfumo wa kuwakaririsha wanafunzi.
Kitu kingine cha msingi kuwekwa wazi hapa ni kwamba, wanafunzi wa sheria nchini kwa sasa wamekuwa wakinyanyasika na kukosa mtu wa kuwasemea machungu yao wanayoyapata. Kwa mfano mpaka sasa wanafunzi wa awamu ta tano(fifth Cohort) wamekuwa wakipigwa danadana na hawajui ni lini hasa watajiunga na masomo yao hayo. Kwa kawaida walitakiwa kuingia mwezi wa sita mwanzoni. Kiukweli wamechoka kukaa nyumbani kwani kwa sasa ni mwaka mmoja tangu wamalize shahada yao ya kwanza lakini mpaka sasa hawajui hatima ya maisha yao.
Ushauri wa bure kwa kaimu mkuu wa shule hii ni kwamba upotoshaji wa taarifa ama tabia ya kukimbia matatizo si suruhisho na ni kinyume cha maadili ya utumishi wa umma. Hivyo basi akae na wanafunzi wake ili kwa pamoja waweze kutatua baadhi ya matatizo yanayojitokeza mara kwa mara.
Mwisho napenda kumpongeza waziri wa katiba na sheria kwa kuliona tatizo hili na kuahidi kufanya mabadiliko katika sheria ya shule ya mafunzo ya sheria kwa vitendo, naamini huu ni mwanzo tu wa mabadiliko makubwa yanayotarajiwa na wadau wa sheria. Pia napenda kuwaasa wanafunzi wa sheria kote nchini kuamka na kudai haki zao na si kunungunika moyoni na kujaa woga kwamba wakikosoa watafeli, hiyo ni nidhamu ya woga.
Haya ni mawazo binafsi tu, naamini ujumbe umefika kwa wahusika.
Ahsanteni.
Sheria ya Tanzania Law School Act ya mwaka 2007 ndio iliyoanzisha shule ya sheria kwa vitendo. Madhumuni ya kuanzishwa kwa shule hiyo ilikuwa pamoja na mambo mengine kutoa mafunzo kwa vitendo kwa wahitimu wa shahada ya kwanza ya Sheria nchini na hii inajumuisha wale waliosoma nje ya nchi ambao wanatakiwa kwa utaratibu wa sasa kipitia mafunzo kwa vitendo katika shule hiyo ya sheria kabla ya kuingia katika ajira rasmi ya utumishi wa umma na nyanja tofauti tofauti.
Sheria hiyo ambayo ilianzisha shule ya mafunzo kwa vitendo imekuwa ikilaumiwa na wadau wengi wa sheria kutokana na mfumo wake mbovu tena usioeleweka hata kidogo. Baadhi ya lawama ambazo wadau wengi wa sheria nchini wamekuwa wakitaka kujua ni ubora halisi wa elimu inayotolewa na shule hiyo, mantiki ya elimu yenyewe na ubovu wa sheria inayosimamia shule hiyo.
Serikali kwa kipindi kirefu sasa imekuwa ikipitisha sheria nyingi zinazowagusa wananchi moja kwa moja pasipo hata kupata maoni ama ushauri wa wadau ili kuboresha sheria husika. Mojawapo ya sheria ambazo zimepitishwa bila kujali maoni ya wadau basi ni hii ya Law School of Tanzania ya mwaka 2007.
Ukiitazama sheria husika, utakubaliana nami kuwa sheria hiyo ilipitishwa kwa kufuata matakwa ama maoni ya kundi flani la watu waliokubaliana kwa maslahi yao binafsi. Imekuwa ni tabia kwa serikali kuanzisha baadhi ya mifumo katika nchi hii pasipo hata kuwa na maandalizi ya kutosha ama kutokufanya utafiti wa kutosha kutoka kwa wenzetu waliopiga hatua katika nyanja husika.
Kwa upeo wangu nilionao nilidhani sheria hii ya shule ya mafunzo ya sheria kwa vitendo ingekuwa ni bora zaidi kuliko ya nchi yeyote ile inayotoa mafunzo ya namna hiyo. Kwa mfano kitivo cha sheria cha chuo kikuu cha Dar es Salaam, ndicho kongwe hapa Afrika Mashariki, kilianzishwa mwaka 1954. Hebu tazama ni takribani miaka 45 tangu mafunzo ya sheria yaanze kutolewa nchini, haiingii akilini eti mpaka mwaka 2007 ndipo ilipoanzishwa shule ya sheria kwa vitendo. Hapo unaweza kuona kuwa kulikuwa na muda mrefu wa kuanzisha mfumo huo kwani kulikuwa na maandalizi ya kutosha na si ubabaishaji unaoekana sasa.
Kwa upande wa Kenya, wao mfumo shule ya sheria kwa vitendo wameanza tangu mwaka 1963. Hivyo basi kwa kuwa wao walikwishaanza muda mrefu, kwetu ingelikuwa sehemu nzuri sana ya kwenda kujifunza wenzetu wamewezaje kufika hapo walipo leo hii. Kwa jambo hili haihitaji hata kuwa profesa ama daktari wa sheria kuweza kulitambua jambo hili. Unaweza kudhani ni utani lakini ndio hali halisi, yapata mwezi wa nne mwaka huu baadhi ya wakufunzi na kaimu mkuu wa shule hiyo walikwenda katika nchi za Kenya na Ghana kwa kile kilichoelezwa kuwa ni ziara ya mafunzo. Hapa unaweza kuona ubabaishaji iweje wapitishe mfumo ambao unagharimu maisha ya wanafunzi pasipo hata kufanya utafiti kabla ya kutunga sheria husika.
Hebu tutazame baadhi ya mapungufu yaliyojitokeza mpaka sasa:
Mosi, Kwa sasa chini ya sheria hiyo ni lazima (mandatory) kwa kila mhitimu wa shahada ya kwanza ya sheria kupita kwanza katika shule ya sheria kwa vitendo ili aweze kuwa na sifa ya kuajiriwa na mashirika ya umma na yale binafsi. Haiwezekani kwa nchi iliyo na uhaba wa wanasheria kama yetu kuweza kuwa na mfumo kama huu kwa sababu kwa utafiti uliofanyika kwa nchi za Kenya na Uganda wao mfumo wa shule ya sheria kwa vitendo si kwa wahitimu wote bali ni kwa wale wanaotaka kuwa mawakili wa kujitegemea pekee na si kama hapa kwetu.
Pili, ubora wa mafunzo. Hapa ndipo kichekesho kinapokuja, mafunzo yanayotolewa katika shule hii ya mafunzo hayana ubora na hayana tija kwa wanafunzi kwani hayana tofauti na yale ambayo wamejifunza walipokuwa wanayasoma katika shahada ya kwanza. Tunaamini ya kwamba tunaposema mafunzo kwa vitendo (Practical training) ni vitendo kweli katika eneo husika na sio kuendeleza dhana ile ile ya mafunzo kwa nadharia (Theory). Ninachokiona katika mafunzo haya na mwendelezo ule ule usio na mantiki wa kufanya masomo kuwa magumu na kuweka mizengwe na fitina zisizo na maana. Wakufunzi wamekuwa wakijali maslahi yao binafsi na siyo yale yanayowaweka pale.
Kwa upande mwingine wakufunzi wa semina wamekuwa ni mzigo usiobebeka na wasio na sifa husika. Walio wengi ni wale ambao ni wanafunzi wanaosomea shahada ya uzamili, wamekuwa hawajui kile wanachokifanya na kuendeleza dhana ya nadharia na ubabe kuliko uwezo halisi wa kisomi.
Mpaka sasa ni aibu kwa serikali na viongozi wanaosimamia shule hii kiasi kwamba hadi hii leo mafunzo haya yamekuwa hayana tija na kukosa mantiki ya uanzishwaji wake. Mafunzo yamekuwa mzigo kwa serikali. Mzigo kwa maana kwamba mfumo wa utoaji mikopo umekuwa ni tatizo na kulalamikiwa na wanafunzi husika huku viongozi wakishindwa kuwasaidia na kutatua tatizo hilo. Kwa mfano wanafunzi wa awamu ya tatu (third Cohort) wamesimamishwa masomo kutokana na matatizo ya mikopo. Kuna habari kuwa watahamishiwa katika kampasi ya Mlimani pindi watakaporejea, hivi hawa viongozi hawatambui wala kuthamini utu wa wanafunzi? Walio wengi wanatoka mikoani na kabla hawajasimamishwa walikuwa tayari wamekwisha kulipia kodi za pango mahala wanapoishi, je kwa huu mkanganyiko nani anawajibika kwa hasara hii wanayopata wanafunzi hawa? Ni ukweli usiopingika kwamba uanzishwaji wa mafunzo haya ulikuwa ni wa kukurupuka.
Utaratibu wa kutahini wanafunzi umekuwa ni ule ule wa mitihani, tena ikiwa imeongezewa ugumu wa makusudi kwa lengo la kufelisha wanafunzi. Kwa mfano matokeo ya wanafunzi wa awamu ya kwanza(first cohort) yaliyotoka hivi majuzi yanaonesha zaidi ya asilimia 73 wamefeli masomo yao. Hapa utashangaa ni wanafunzi hao hao waliomaliza shahada zao za kwanza tena kwa alama za juu, leo hii anaonekana si kitu katika shule hii, hilo kwa mwenye akili timamu halimuingii akilini.
Mgongano wa maslahi ni jambo la tatu linalotia doa mfumo mzima wa mafunzo ya sheria kwa vitendo. Watu wanaounda bodi ya shule hii wamekuwa na mgongano wa maslahi na kazi zao wanazozifanya. Kwa mfano mtu hawezi kuwa mkufunzi wa mafunzo hapo hapo ni mjumbe wa bodi na wakati huo huo ni raisi wa chama cha mawakili Tanzania. Hapo hakuna haki yoyote itakayotolewa kwa misingi ya namna hiyo. Ndio maana bodi hiyo imekuwa ikitoa maamuzi ya ajabu na ubabe usio na weredi hata kidogo na kuendeleza mfumo wa kubeza kila hoja inayotolewa kwa lengo la kufanya maboresho katika shule hiyo.
Pia haiwezekani Dean wa kitivo cha Sheria cha chuo kikuu cha Dar es Salaam kuwa mjumbe wa kudumu wa shule hiyo ya mafunzo ya sheria kwa vitendo. Iweje awe Dean wa chuo hicho pekee kama hakuna ajenda ya siri iliyojificha? Kwa kuwa wanafunzi wa shule hiyo wanatoka katika vyuo mbalimbali nchini, kwanini Dean wa vyuo vyao wasiwe wajumbe wa bodi ama wao hawahusiki? Pia mbona wakufunzi ni hao hao wa chuo kikuu cha dar es salaam na sio wa vyuo vingine? Hapa kuna tatizo, tena si dogo bali ni kubwa na nimeanza kuamini kuwa wakufunzi wa chuo kikuu cha dar es salaam wamefanya mafunzo hayo kuwa mali yao.
Ama kwa hakika ni jambo la kushangaza sana kwa shule hii ya mafunzo ya sheria kwa vitendo ambayo imekuwa ikiongozwa kwa ubinafsi na ubabaishaji wa hali ya juu sana na kaimu mkuu wa shule hiyo. Kaimu huyo hashauriki na pia hajawahi kuongea na wanafunzi wake tangu waingie katika shule hiyo na wamekuwa wanashindwa kutoa maoni yao na dukuduku zao kuhusiana na mfumo mzima wa mafunzo wanayopata.
Ni ukweli usiopingika kuwa kati ya kozi zilizowekewa ugumu, ubinafsi, mizengwe, na umimi wa hali ya juu hapa nchini, basi kozi ya sheria inatia fora. Kwa ujumla kwa yeyote yule ambaye anajitahidi kusoma ili angalau aingie kwenye fani hii anajua jinsi anavyokumbana na vitisho, manyanyaso, uonevu wa waziwazi toka kwa wataaluma wanaofundisha fani hii.
Kwa kumalizia napenda kutoa ushauri kwa viongozi husika na serikali kwa ujumla. Kwanza wanatakiwa kuelewa kuwa wanaharibu mifumo kwa kukosa ushauri mzuri na kutotaka kufuata maoni ya wadau, hivyo basi ni rai yangu kwamba katika mabadiliko ya sheria hiyo wanapaswa kuileta kwa wadau ili watoe maoni yao kwa ajili ya maboresho yenye tija kwa taifa.
Kitu cha pili ni kwamba serikali iwe sikivu na iache kuchezea tena kwa makusudi nguvu kazi ya vijana wenye kiu ya kuitumikia nchi yao kwa moyo wote lakini wanakwamishwa kwa mifumo mibovu inayowekwa. Hivyo basi hakuna haja ya kuendelea kunganganiza wahitimu wote wa shahada ya kwanza ya sheria kusoma mafunzo hayo bali iwe kwa wale wachache tu wanaopenda kuwa mawakili wa kujitegemea pekee.
Jambo la tatu ni kwamba si lazima mafunzo hayo yatolewe Dar es Salaam pekee, naamini ya kwamba mafunzo haya haya kwa nchi za wenzetu kama Australia, wao kila chuo kinakuwa na mafunzo kwa vitendo (Law School). Hivyo basi hapa nchini ingekuwa ni jambo rahisi kuwa na mafunzo haya kwa kila chuo. Hebe tazama vyuo vyote vivavyotoa shahada ya kwanza ya Sheria mahala vilipo kuna mahakama kuu ya Tanzania. Kwa mfano SAUT- Mwanza, RUCO na TUMAINI-Iringa, MZUMBE-Mbeya, Makumira-Arusha, UDSM na TUMAINI tawi la Dar es Salaam. Kwa hakika wanafunzi hao wangepata wasaa mzuri wa kujifunza kwa vitendo.
Masomo hayaeleweki na yamekuwa ya nadharia mno hivyo kukosa mantiki na kushindwa kukidhi matakwa ya kuanzishwa kwake. Tulitegemea wanafunzi wangekuwa wanafanya mazoezi ya vitendo kwa kufanya kesi za kutengenezwa ili mafunzo yawe ya uhalisia zaidi kuliko hali ya sasa ambapo ni nadharia pekee. Kwa sasa mafunzo hayo hayana tofauti na mfumo wa zamani wa internship. Hivyo basi mfumo wote wa mafunzo utazamwe upya ili mafunzo yaweze kuleta mantiki ya uanzishwaji wake.
Nikija katika utaratibu wa kutahini wanafunzi, hapa watanzania hasa wakufunzi inabidi kubadilika, tuondokane na utaratibu wa kutahini wanafunzi kwa kutumia kigezo cha mitihani pekee. Katika sheria mwanafunzi anafundishwa jinsi ya kutafuta sheria na si vinginevyo. Kupitia mitihani huwezi kutambua uwezo binafsi wa mwanafunzi husika ila ni kuendeleza mfumo wa kuwakaririsha wanafunzi.
Kitu kingine cha msingi kuwekwa wazi hapa ni kwamba, wanafunzi wa sheria nchini kwa sasa wamekuwa wakinyanyasika na kukosa mtu wa kuwasemea machungu yao wanayoyapata. Kwa mfano mpaka sasa wanafunzi wa awamu ta tano(fifth Cohort) wamekuwa wakipigwa danadana na hawajui ni lini hasa watajiunga na masomo yao hayo. Kwa kawaida walitakiwa kuingia mwezi wa sita mwanzoni. Kiukweli wamechoka kukaa nyumbani kwani kwa sasa ni mwaka mmoja tangu wamalize shahada yao ya kwanza lakini mpaka sasa hawajui hatima ya maisha yao.
Ushauri wa bure kwa kaimu mkuu wa shule hii ni kwamba upotoshaji wa taarifa ama tabia ya kukimbia matatizo si suruhisho na ni kinyume cha maadili ya utumishi wa umma. Hivyo basi akae na wanafunzi wake ili kwa pamoja waweze kutatua baadhi ya matatizo yanayojitokeza mara kwa mara.
Mwisho napenda kumpongeza waziri wa katiba na sheria kwa kuliona tatizo hili na kuahidi kufanya mabadiliko katika sheria ya shule ya mafunzo ya sheria kwa vitendo, naamini huu ni mwanzo tu wa mabadiliko makubwa yanayotarajiwa na wadau wa sheria. Pia napenda kuwaasa wanafunzi wa sheria kote nchini kuamka na kudai haki zao na si kunungunika moyoni na kujaa woga kwamba wakikosoa watafeli, hiyo ni nidhamu ya woga.
Haya ni mawazo binafsi tu, naamini ujumbe umefika kwa wahusika.
Ahsanteni.