Lakini serikali ya Kikwete inatutaka nini?

Tikerra

JF-Expert Member
Sep 3, 2008
1,702
146
Nimeshasikia na kuona irresponsible governments lakini hii ya Kikwete ni mwisho.Ndugu zangu,hivi mnajua kwamba sasa watu wanamuita Kiwete badala ya Kikwete,loo, mbayaaaa.Ukiwete huu uko kwenye maeneo mengi wote tunayajua,lakini leo nitaongelea hili la mabomu ya Mbagala.

Hivi kulikuwa na sababu yeyote kweli ya wananchi wetu wale 25 au hata zaidi kuuwawa.Jamani hivi hatuna vichwa jeshini vya kuweza kujua kwamba mabomu yale katika mazingira yalipokuwa yatalipuka.Mungu wangu kweli tuamini hivyo. Na kwanini mabomu yahifadhiwe kwenye kadamnasi ya watu kule mbagala.Kwanini lakini.Mtasema jeshi ndilo liloanza kujenga kambi yake halafu wananchi ndio wakaja.Sawa lakini serikali haikuwawaona?Kama wanachi wameshakuwepo karibu kulikuwa na sababu gani ya msingi ya kuyahifadhi mabomu yale Mbagala.Kwa nini hayakuhamishwa.Si kuna makambi yetu mengi yaliyopo mbali na watu,kwanini hayaku hifadhiwa huko.

Sasa wabomu ya awali yameshalipuka,lakini bado tunaona na kusikia mengine yakiendelea kulipuka.Jamani hivi ni kitu gani hasa kinaendelea.Hivi Watanzania tumefika mahali we can't do anything right.Hawa watu hasa watoto ambao wanaishi katika mazingiza ya milipuko ya mabomu kila kukicha, tunategemea wawe watu wa aina gani baadae?Serikali inapashwa kukumbuka kwamba hawa nao ni watu,na uzembe huu uliokidhiri na kuvuka mipaka una athiri maisha yao na ya vizazi vyao kwa kiwango kikubwa

Lakini katika mazingira ya kushangaza bado namuona Waziri anayehusika anedelea kupeta!Hivi nchi hii hakuna swala la uwajibikaji kabisa.Mbona Mwinyi aichukua collective responsibility kwa yale yaliyotokea magereza?Watu wamekufa kizembe,lakini Wazini na wahusika wengine wanaendelea kula kuku kwa mrija.Hivi kuna nini hasa?

Sawa tutamlilia Mungu katika hili, kwa kuwa ndiye pekee sasa aliye baki kuwa mtetezi wetu.Tukaze moyo watanzania Mungu yupo.
 
Mkuu Tikerra heshima mbele!

Mimi napinga utawala wa JK kwa zaidi ya 100% lakini kwa hoja yako ya leo kuhusu kulipuka kwa mobomu mbagala na impact yake kwa wananchi, sioni uhusiano wa moja kwa moja na utawala wa JK.....to me hili lingewa kutokea kipindi cha BM,AHM au hata kipindi cha JKN!

Labda kitu ambacho ungemlaumu JK ni namna walivyohandle tatizo lile baada ya kutokea na sio kwa nini JK hakuzuia kutokea mkuu! Ile ilikuwa ajali ambapo si Tanzania tu bali hata sehemu nyingi duniani ajali hizi huwa zinatokea......hata na hivyo kwa milipuko ya mbagala pengine impact haingekuwa kubwa vile kama wananchi wangekuwa mbali na eneo lile!.....to me kama ni kulaumiwa wananchi kusogea maeneo ya jeshi, basi ni tawala zote zilizopita i.e JKN,AHM,BM itabidi walaumiwe kwa sababu hawakuweka utaratibu ambao ungehakikisha wananchi hawasogelei maeneo ya jeshi!

So kwa hili, sitaki kurusha lawama moja kwa moja kwa JK!
 
Hata kama wasingekuwa wamepata taarifa kwamba mabomu yana uwezekano wakulipuka tungewalaumu.Kumbuka unapokuwa kiongozi mahali unawajibika na lolote linalotokea mahali pale.Kwa hiyo una wajibika moja kwa moja.Hizo ndizo sheria za kiutendaji.Kwa hiyo Kikwete anawajibika moja kwa moja.

Lakini hata hivyo kuna taarifa za kuaminika kabisa kwamba walipata taarifa mapema kwamba mabomu husika yalikuwa na uwezekanao wa kulipuka lakini waka puuzia.Kwa hiyo hakuna cha kujitetea.

Mkuu Tikerra heshima mbele!

Mimi napinga utawala wa JK kwa zaidi ya 100% lakini kwa hoja yako ya leo kuhusu kulipuka kwa mobomu mbagala na impact yake kwa wananchi, sioni uhusiano wa moja kwa moja na utawala wa JK.....to me hili lingewa kutokea kipindi cha BM,AHM au hata kipindi cha JKN!

Labda kitu ambacho ungemlaumu JK ni namna walivyohandle tatizo lile baada ya kutokea na sio kwa nini JK hakuzuia kutokea mkuu! Ile ilikuwa ajali ambapo si Tanzania tu bali hata sehemu nyingi duniani ajali hizi huwa zinatokea......hata na hivyo kwa milipuko ya mbagala pengine impact haingekuwa kubwa vile kama wananchi wangekuwa mbali na eneo lile!.....to me kama ni kulaumiwa wananchi kusogea maeneo ya jeshi, basi ni tawala zote zilizopita i.e JKN,AHM,BM itabidi walaumiwe kwa sababu hawakuweka utaratibu ambao ungehakikisha wananchi hawasogelei maeneo ya jeshi!

So kwa hili, sitaki kurusha lawama moja kwa moja kwa JK!
 
Hata kama wasingekuwa wamepata taarifa kwamba mabomu yana uwezekano wakulipuka tungewalaumu.Kumbuka unapokuwa kiongozi mahali unawajibika na lolote linalotokea mahali pale.Kwa hiyo una wajibika moja kwa moja.Hizo ndizo sheria za kiutendaji.Kwa hiyo Kikwete anawajibika moja kwa moja.

Twende polepole basi......! Nacho sema mimi, kama ilivyo kwa ajali yoyote ile, serikali italaumiwa labda moja kwa kushindwa kuzuia (kama inazuilika) pili, kwa kushidwa kuhandle vizuri madhara ya ajali husika......etc! sasa ndugu yangu unaushahidi gani kama serikali eti ilikuwa na taarifa kuwa mabomu yangelipuka na ikakaa kimya bila kuchukua hatua yoyote?

Lakini hata hivyo kuna taarifa za kuaminika kabisa kwamba walipata taarifa mapema kwamba mabomu husika yalikuwa na uwezekanao wa kulipuka lakini waka puuzia.Kwa hiyo hakuna cha kujitetea

Nani kakupa weye taarifa hizo mkuu?
 
Back
Top Bottom