Kwikwi za huduma ya m-pesa; kulikoni?

KAPONGO

JF-Expert Member
May 29, 2009
1,661
668
Juzi, jana na hadi hivi sasa huduma ya kutuma na kupokea fedha kwa kutumia M-Pesa imekufa "kwishney' kabisa hapa jijini Dar es salaam, na nadhani nchini kote. Kila wakala wa huduma hiyo niliyemtembelea maelezo yake yalikuwa yaleyale- HAKUNA MTANDAO. Na ukiuliza sababu ya kuwepo kwa tatizo hilo wanasema hawajui na wala hawajaarifiwa kulikoni. Pamoja na usumbufu huo wanaopata wateja cha ajabu ni kuwa hata Voda wenyewe ama kwa kiburi, ukiritimba, ama dharau za maksudi, hawajatoa maelezo yoyote kwa wateja kuhusu tatizo hilo, kiasi cha baadhi ya wateja niliowakuta wakisotea huduma hiyo katika vituo vya mawakala, kuingiwa na hofu kuwa waje wakaingizwa mjini kama ile habari ya DECI. Mmoja alikwenda mbali kwa kusema kuwa kama watu waliaminika katika jamii ndio waliotuingiza mkenge katika mambo mengi ya uchumi, Voda watashindwaje kutu-deci. Voda toeni ufafanuzi kuhusu kadhia hii!:A S cry:
 
Hizi transactions za via mobile nafikiri wamiliki hawajajipanga vizuri. Ukiacha network kusumbua unaweza ukaenda kwa wakala akakwambia hana hela subiria hadi watu watakapoenda kudeposit.
 
mimi nimelizwa pesa zangu hadi leo sijazipata, zimetolewa na mtu kaenda bila kitambulisho lakini cha ajabu wakala kampa as simple as that. nafika naambiwa zimeshachukuliwa, kwenye simu bado hata sijapata sms kusema zimetolewa -- watch out this system, hasa unapotuma M-PESA kwenda TIGO pesa hapo kuibiwa ni rahisi sana then wanasingiziana, mara nenda TIGO, mara Nenda M -PESA.
 
Yani imeshakuwa tatizo,minafikiri hawa jamaa wanapenda pesa tu kabla ya kujipanga,inaonekana kama vile system imezidiwa.Au ndio DECI nyingine maana huko kuna hela kibao za wateja pengine kuliko hata DECI.
 
Mmiliki wa server za M_pesa yupo kenya, sasa voda fone wanunuzi wa leseni ya M-pesa hawawezi kuwa na jibu la moja kwa moja wakati kuikwa na tatizo la m-pesa. ili jua kuwa pesa zako zipo salama.
 
SEACOM ipo down - Nairobi ipo down - MPESA ipo down - Hakuna System!

nashukuru kwa kunijuza, ngoja nipunguzve jazba

hata mwili wa binadamu wakati mwingine hupata hitilafu na kusababisha homa
 
Mmiliki wa server za M_pesa yupo kenya, sasa voda fone wanunuzi wa leseni ya M-pesa hawawezi kuwa na jibu la moja kwa moja wakati kuikwa na tatizo la m-pesa. ili jua kuwa pesa zako zipo salama.

Kama nilivyobandika hapo juu - SEACOM Link to Nairobi (from Mombasa) is currently down na ndiyo maana M-PESA service haipatikani kwa sasa.. Nina ofisi jijini Nairobi ambazo hadi sasa tuna-run kwenye secondary link (VSAT) kutokana na tatizo hilo la SEACOM .. so far no ETA!
 
Tumieni mabenki kutuma pesa zenu hasa zikiwa zaidi ya laki tano, hizi systems za fasta fasta zina majuto yake, mawakala wenyewe elimu darasa la saba utata mtupu hata elimu ya mwanzo ya utunzaji pesa hawana. wakala kama muuza duka.
 
Bora hata muuza duka,wakala hawa kama wauza kalanga

mbali ya hili mie nimelizwa pesa mara2,ya kwanza 30 nilimtumia mama (wa kunizaa),akanambia hata meseji hakuipata na wakati M-pesa wanasema imetumwa,paka leo nilipoteza

mara ya pili kituo tofauti nikatuma 10elfu nikaituma kwingine,hakupata meseji lakini salio linasoma,alivyoongea na voda akaambiwa mimi nirudi kwa wakala a-resend kwa maana wakati inatumwa mtandao ulifeli,kufika kwa wakala akawa mbogo,akawa mkali,akakataa katakata ku-resend,nikamuuliza kwani hajawahi kupata hasara kwa nini anakataa kuresend?akasusa,basi nikaamua kuipotezea nikaondoka

ila frankly speaking,M-PESA ina matatizo sana pamoja na mawakala wao,wanajua kuandika tu,hawawezi kuhandle wala kusolve out contingencies,binafsi sina imani tena na mambo yao
 
mimi nimelizwa pesa zangu hadi leo sijazipata, zimetolewa na mtu kaenda bila kitambulisho lakini cha ajabu wakala kampa as simple as that. nafika naambiwa zimeshachukuliwa, kwenye simu bado hata sijapata sms kusema zimetolewa -- watch out this system, hasa unapotuma M-PESA kwenda TIGO pesa hapo kuibiwa ni rahisi sana then wanasingiziana, mara nenda TIGO, mara Nenda M -PESA.

Ni kweli mkuu, nami wiki 4 zilizopita nilipoteza hivyo hivyo, nilimtumia dogo kijijini lakini bahati mbaya siku hiyo hiyo akapoteza simu na jamaa aliyechukua simu kaenda kutoa pesa bila kitambulisho.
 
Bora hata muuza duka,wakala hawa kama wauza kalanga

mbali ya hili mie nimelizwa pesa mara2,ya kwanza 30 nilimtumia mama (wa kunizaa),akanambia hata meseji hakuipata na wakati M-pesa wanasema imetumwa,paka leo nilipoteza

mara ya pili kituo tofauti nikatuma 10elfu nikaituma kwingine,hakupata meseji lakini salio linasoma,alivyoongea na voda akaambiwa mimi nirudi kwa wakala a-resend kwa maana wakati inatumwa mtandao ulifeli,kufika kwa wakala akawa mbogo,akawa mkali,akakataa katakata ku-resend,nikamuuliza kwani hajawahi kupata hasara kwa nini anakataa kuresend?akasusa,basi nikaamua kuipotezea nikaondoka

ila frankly speaking,M-PESA ina matatizo sana pamoja na mawakala wao,wanajua kuandika tu,hawawezi kuhandle wala kusolve out contingencies,binafsi sina imani tena na mambo yao

mimi wamenilamba laki 700,000 sitaki hata kusikia kitu kinaitwa MPESA in my life - kuna vijana wanjanja wanjanja wanachezea network - nimefuatilia makao makuu hapa mlimani city wananizingua na kunipotezea muda wangu. sababu hata message kwamba pesa imetolewa sijawahi ipata, na jamaa kaenda kwa wakala kalamba pesa zote eti bila kitambulisho - inaingia akililini kweli?
 
system inaweza kuwa genuine ila watu wenyewe ndyo matatizo matupu kuanzia wanaoangalia network pamoja na mawakala wao - na mbaya zaidi ukituma MPESA kwenda TIGO PESA basi hapo andika ni maumivu.
 
Juzi, jana na hadi hivi sasa huduma ya kutuma na kupokea fedha kwa kutumia M-Pesa imekufa "kwishney' kabisa hapa jijini Dar es salaam, na nadhani nchini kote. Kila wakala wa huduma hiyo niliyemtembelea maelezo yake yalikuwa yaleyale- HAKUNA MTANDAO. Na ukiuliza sababu ya kuwepo kwa tatizo hilo wanasema hawajui na wala hawajaarifiwa kulikoni. Pamoja na usumbufu huo wanaopata wateja cha ajabu ni kuwa hata Voda wenyewe ama kwa kiburi, ukiritimba, ama dharau za maksudi, hawajatoa maelezo yoyote kwa wateja kuhusu tatizo hilo, kiasi cha baadhi ya wateja niliowakuta wakisotea huduma hiyo katika vituo vya mawakala, kuingiwa na hofu kuwa waje wakaingizwa mjini kama ile habari ya DECI. Mmoja alikwenda mbali kwa kusema kuwa kama watu waliaminika katika jamii ndio waliotuingiza mkenge katika mambo mengi ya uchumi, Voda watashindwaje kutu-deci. Voda toeni ufafanuzi kuhusu kadhia hii!:A S cry:
Sure Mkuu!
Mi ni mmoja wa waathirika sana wa hii shida!...
Nilitumia MPESA jana kwa minajili ya kununua umeme, na hadi leo sijarudishiwa hata delivery msg. Na hata nikiuliza salio hakuna majibu....sIELEWI KAMA SALIO LANGU LIMEPUNGUZWA AU LIPO.
 
Jana niliwaachia laki mbili ilikuwa mida ya saa sita wamefanikiwa kunitumia leo asbi ebu imagine.
Alafu sio mara moja mara nyingi tuu mmpesa ni issue kama yamewashinda si mbwage manyanga
 
mimi wamenilamba laki 700,000 sitaki hata kusikia kitu kinaitwa MPESA in my life - kuna vijana wanjanja wanjanja wanachezea network - nimefuatilia makao makuu hapa mlimani city wananizingua na kunipotezea muda wangu. sababu hata message kwamba pesa imetolewa sijawahi ipata, na jamaa kaenda kwa wakala kalamba pesa zote eti bila kitambulisho - inaingia akililini kweli?
Pole sana, hiyo ni hela nyingi. Mi nakushauri uende TCRA, kuna fomu za malalamiko kwenye website yao (TCRA|Tanzania Communications Regulatory Authority). Jaza hiyo fomu peleka TCRA na nakala wapelekee wao-M-Pesa.Hata kama hutapewa pesa zako, ni lazima uonyeshe unatambua haki yako. Hii itawasaidia hata ndugu na rafiki zako wa karibu wasipatwe na madhila kama yako. Hiyo pesa ni nyingi na kosa ni lao (wamekiuka utaratibu kwa kutoa pesa bila kibali), don't go down without a fight!
 
Back
Top Bottom