Kweli harusi sasa zinazidi kututia umasikini

Ni ushauri tu,
kama unataka kuoa na una uwezo wa kufanya arusi, fanya, na kama umejitathmini pamoja na familia yenu na kujikuta hamuwezi gharama za harusi, tafadhali usitafute urafiki na kuchukua namba kwa kila utakae salimiana nae ili mradi baadae uombe mchango.
unajipa mzigo ambao utakusumbua kwa muda mrefu hasa wakitaka na wewe uwachangie wakati bajeti yako unajua mwenyewe.
Naamini kama kweli mwanamke anakupenda,harusi haiwezi kuwa kigezo cha kutofunga ndoa.
 
huwa najiuliza mwisho wake lini watanzania wa hali ya kati na chini kimaisha, hasa mijini, wataachana na ulimbukeni wa kufanya gharama kubwa za harusi?

Tukio ambalo linachukua mamilioni halafu linafanyika within few hrs watu wanakula wanakunywa wanaondoka, bajeti ya milioni 9 baada ya honey moon maharusi wanayaanza maisha kwa taabu kulipa madeni n.k., kwanini watanzania hatubadiliki?

Wazungu miaka ya nyuma walishapita humu wakabadilika miaka mingi ilopita karne hii wakihudhuria harusi zetu wanatushangaa na kutuona ni matajiri sana kumbe hamna kitu!

Kweli hatukatai wapo wanaojiweza kifedha wacha wafanye, lakini wenzangu na miye unajikamua unafanya sherehe kubwa na mnaendelea katika circle ya kuchangiana the whole year unajikuta unachangia harusi tu, sijui kama kuna wanaopiga hesabu ya hizo kadi familia iliochanga kwa mwaka na si kana kwamba ina mwisho, no, na mwaka ujao hivyo hivyo.

Tuamke watanzania, tufanye harusi za gharama ndogo, kama ni swala la kuchangishana basi tuchangishane ada-fees-watoto wakasome vyuoni malaysia, london na us, matunda yatakuja onekana. Wakenya wenzetu waliliona hili mapema, leo wengi ni maboss ktk nchi yetu wenyewe!

Tubadilike watanzania! Harusi nacho ni chanzo cha kutiana umasikini!

tungekuwa mahiri mambo kama haya ndo tungeanza nayo yanayotuzidishia umaskini bahati mbaya tuna wanaharakati wengi wa kulinda maslahi ya wazungu badala ya kuondoa hulka hii mbovu.
 
bora umesema wenzako na wewe, waache wenye nazo wafanye wee unakereka nini? Ni siku haitajirudia kamwe wacha waenjoy to the fullest

tatizo wanatuchangisha hata maskini na usipochanga watapiga kampeni utengwe na jamii kwa kuwa wana nguvu kwenye jamii
 
Tafadharini naombeni kipimio cha kudhibitisha kuwa hii ni ndoa ya gharama na hii ni kawaida na hii ni ya chini.
 
mimi hujanitoa milion mfukoni kwa ajili ya harusi aisee simple and clear pete, dress nzur yangu na baba yoyoo kachakula kidogo jama party hivi kwishinei wataotaka matarumbeta wajichange wao wayalete tu sitaki stress mmeoana badala mfurahie ndoa yenu mnawaza madeni, sijui wanakamati wanavunja, mara oooh kuna ndugu hajachanga!!! shiiiiiiiit sina muda huo mimi
 
Tafadharini naombeni kipimio cha kudhibitisha kuwa hii ni ndoa ya gharama na hii ni kawaida na hii ni ya chini.

Kipimo ni uwezo wa mtu binafsi. Mtu eti inaandaliwa harusi ya bajeti ya 15m halafu bwana harusi yeye ana 1m; zilizobaki zote ni wanakamati na ndugu wakunjane mashati mpaka zipatikane.
Mimi nimewahi kuwa mwanakamati mara 3 aisee ni stress tupu!! Bajeti kubwaaa, pesa hakuna bwana harusi nae anasema hana pesa.
Lakini ukifanya kitu kadri ya uwezo wako,huchangishi mtu huna stress wala huanzi maisha ya ndoa na stress, safi kabisa.
 
Kwaiyo kama mtu ana uwezo unataka asiji enjoy? Msio na uwezo jikuneni mkono unakofika

Wewe tumia akili kidogo. Wewe kama unauwezo unachangisha watu pesa za nini??. Mtoa mada kaweka wazi kabisa ya kwamba kama wewe unauwezo basi fanya hiyo shughuli kwa gharama yako mwenyewe. Watu hawataki michango, hii michango inachangia kwa kiasi kikubwa kutia watu umasikini, kisa ni ulimbukeni. Eti kuji enjoy, ji enjoy kwa pesa yako, acheni kuchangisha watu michango isiyokuwa na maana.
Mimi nina miaka mitatu sasa tangia nimeweka fulstop kwenye suala zima la kuchangia Harusi, kipaimara, sijui send off party etc.. Mtu akiniletea kadi namtaarifu kabisa kuwa mimi huwa nachangia Misiba, masuala ya ugonjwa na mambo kama hayo. Nachangia haya mambo kwakuwa ni mambo ambayo yanatokea bila taaria, na linaweza kukukuta wakati wowote.
Sasa nyie mmekaa mnafanya yenu siku zooote, mmepanga kuishi pamoja mnakuja kutukurupusha na michango, tena mnaweka na kima cha chini as if mnafahamu kipato changu. Halafu mtu huyo huyo anaenda hospitali kumuangalia mgonjwa anaenda mikono mitupu, au anapeleka Juice ya kijoti. This is nonsense
 
Kipimo ni uwezo wa mtu binafsi. Mtu eti inaandaliwa harusi ya bajeti ya 15m halafu bwana harusi yeye ana 1m; zilizobaki zote ni wanakamati na ndugu wakunjane mashati mpaka zipatikane.
Mimi nimewahi kuwa mwanakamati mara 3 aisee ni stress tupu!! Bajeti kubwaaa, pesa hakuna bwana harusi nae anasema hana pesa.
Lakini ukifanya kitu kadri ya uwezo wako,huchangishi mtu huna stress wala huanzi maisha ya ndoa na stress, safi kabisa.
Unafaa kuwa Mwalimu au Doctor, mambers wote wa JF tungekuwa kama wewe basi JF ingekuwa na heshima sana asante kwa kunielimisha.
 
Tafadharini naombeni kipimio cha kudhibitisha kuwa hii ni ndoa ya gharama na hii ni kawaida na hii ni ya chini.

Hakuna kipimo kwa kuwa suala hili ni subjective. Cha msingi ni kuwa usifanye sherehe ya harusi zaidi ya uwezo ulio nao period. Wewe kama unaweza ku raise milioni tano kwa kusave, fanya hivyo na fanya harusi ya milioni Tano. Kama unaweza kusave milioni Moja, fanya hivyo na ufanye harusi ya Milioni Moja. Sasa wewe unaweza ku save milioni moja, halafu unataka harusi ya Milioni 15, hii ni harusi kubwa kuliko uwezo wako na ndivyo vitu tunavyovipinga hapa
 
Back
Top Bottom