Kwanini watanzania wengi hawapigi kura?

Watu wanapiga KURA. Tatizo TUME ya uchaguzi siyo huru. Tuna uhakika gani kuwa zile takwimu za watu waliojiandikisha zinazotangazwa na TUME kuwa ni sahihi?
 
dalili ya kukata tamaa -- "even if i vote nothing changes!!!" hali inabaki ni ile ile tu miaka nenda miaka rudi.

inabidi elimu ya uraia itembee sana hasa vijijini - chadema wanajitahidi sana kutoa elimu hii ya uraia.
 
Voter apathy iko kila mahali duniani hata katika demokrasia zilizokomaa kama India na Marekani. issue hapa ni kuongeza elimu ya uraia ili watu wajue umuhimu wa kushiriki katika demokrasia ya uchaguzi. Jukumu hili ni la kila raia.
 
kwa kweli hili ni tatizo kubwa, kama alivyosema mbopo kuna haja ya elimu ya uraia kutolewa, imenishangaza igunga, tofauti ya idadi ya waliojiandikisha na waliopiga kura ni kubwa mno. Pia kuna haja ya watu kuhamasishwa kujiandikisha wakati utakapofika maana inaonesha pia watu wengi hawajajiandikisha na wengi ni vijana ambao ndio waleta mabadiliko.
 
Watanzania wengi(nami nikiwemo) hawana Imani na Tume ya Uchaguzi,utamsikia mtu akisema "siendi kupiga kura kwani hata nikipiga najua jamaa watachakachua tu" hata maeneo yale ambayo wapinzani wameshinda ni baada ya wananchi kulinda kwa nguvu kubwa sana kura zao,na tume haiwezi kuwa fair kwa sababu ni zao la Serikali na watumishi wake waandamizi ni wateule wa Rais.
Nini Kifanyike?
  1. Vyama vya siasa vihamasishe na kuelimisha wananchi hasa Vijana umuhimu wa kupiga kura kama wanataka mabadiliko
  2. Wananchi wenye uelewe zaidi(wasomi) tuwe msitari wa mbele kuelimisha ndugu zetu hasa wa vijijini umuhimu wa kupiga kura bila kuhofia vitisho vya wanasiasa.
  3. Elimu ya mpiga kura iingizwe kwenye mitaala ya Elimu kama somo maalumu(Sio Civics ana GS,Ds zilivo sasa) kwa kuwa uchaguzi ndio huamua na kuweka mustakabali wa Taifa.
  4. Katika mchakato wa Katiba mpya tume ya Uchaguzi iundwe kama chombo huru ambacho wajumbe wake wanapendekezwa na kuteuliwa na bunge.
  5. Wakurugenzi wa uchaguzi wilayani na mikoani wasiwe watendaji wa Serikali kama ilivyo sasa(wakurugenzi wa wilaya na mikoa,manispaa,jiji).
  6. Vyama vya siasa hasa vya upinzani viwe na mikakati endelevu ya kujinadi na kujiimarisha kwa wananchi na sio kusubiri wakati wa Uchaguzi tu.
  7. Tume iliyopo sasa(japo mbovu)itumie technologia ya digitali ya kuonyesha matokeo moja kwa moja kama yanavyoletwa toka vituoni bila kusubiri majumuishoa ya pamoja ambayo hutoa mwanya wa uchakavhuaji.
Yangu machache ni hayo,wanajamvi watatoa mengi zaidi

Great thinkers,
Katika uchaguzi mkuu mwaka 2010 idadi kubwa ya wapiga kura waliojiandikisha na wale waliokwenda vituoni siku ya uchaguzi inafikirisha sana.Watu wengi hawakwenda kupiga kura.
Tujiulize ni kwanini.
1.Rafu za wasiotaka kushindwa ambao hununua kadi za wapiga kura na kuzitupa barabarani wakishatangazwa washindi?
2.Watu wamekata tamaa na hivyo hawaoni umuhimu wa kupiga kura?
3.Watu hawajajua umuhimu wa kupiga kura?

Maswali ni mengi na majibu yake sio mepesi.Sisi tunaojua umuhimu wa kupiga kura tuna jukumu la kutafuts sababu zinazowafanya watu wajiandikishe kwa wingi,mikutano ijae wakati wa kampeni lkn idadi iwe pungufu baada ya matokeo kusomwa/kutangazwa kama tulivyojionea leo hii matokeo ya kura za ubunge wa jimbo la Igunga.
Tutafakari kwa pamoja na tuiokoe nchi yeti iliyo katika hatari ya kuporomoka kwa demokrasia maana uchaguzi bila idadi tosha ya wapiga kura ni upuuzi mtupu unaoweza kuwaweka madarakani wapuuzi na hivyo kuwatia kitanzi watanzania maskini
 
Issue siyo kukosa imani na Tume. Watu hawajajua kwamba wana wajibu wa kuamua hatma ya uongozi wa nchi na matokeo yake baada ya uchaguzi wanalia lia kama vile hawakuwa na fursa.
 
WATANZANIA TUNAPIGA SANA KURA ISIPOKUA WALE WAPIGA KURA MARUANI SIKU ZOTE WANATUZIDI IDADI WAPIGA KURA TULIOHAI, NA MTAJI WA CCM KUTISHA WANANCHI

Wa-Tanzania tunnapiga sana kura isipokua wale Wa-Tanzania WAFU WASIOONEKANA ni wengi zaidi kuliko wale wanaoonekana kwa macho na wenye uamuzi kuchagua kukipigia kura chama tofauti na CCM.

Hivi karibuni kumeibuka aina ya demokrasia mpya nchini ya (1) demokrasia ya Bastola kiunoni kwenye kampeni za kisiasa, (2) Matumizi ya maruani kwenye daftari la wapiga kura ambalo ni miliki ya CCM tu, (3) uhuru wa rushwa za mapishi na nafaka kwenye kampeni, na hivi sasa (4) ubunifu mpya kwa CCM kuibuka na fesheni mpya ya
'CCM GREENGUARD MUNGIKI' na utekaji, uchomaji nyumba za watu ubakaji na kadhalika.

Hivyo ni muhimu ikawekwa kwamba
DAFTARI LA WAPIGA KURA liwe likifanyiwa uhakiki na CHOMBO HURU kinachokubalika na vyama vyote vya siasa nchini.

Vile vile ni vema utaratibu ukawepo wa wazi zaidi kwamba uchaguzi wowote unapoitishwa katika jimbo lolote lile basi ni sharti vyama vyote vitakavyoshiriki uchaguzi huo vishiriki moja kwa moja kufanya uhakiki mwingine, hata kama uhakiki wa kile chombo huru kilimalizika tu jana yake, ili kuwepo na uwanja sawa kwa waashiriki wote kwa wakati husika.

Huwezi kumridhisha mtu yeyote aakilini kwamba daftari la wapiga kura aliloliacha Rais Mstaafu Mkapa zaidi ya miaka kumi iliopita ndio bado hutumika kuendeshea uchaguzi mpaka leo kwa kuwa watakaokua wamekufa ni wengi sana hapo kati kati ambo majina yao yafaa kuondolewa kwenye daftari hilo kabla CCM inayohodhi utunzaji wa daftari hajaamua kutumia faida ya WAFU KUTOWEZA KUJIELEZA hivyo kuelekeza kura zao zote kwake jinsi apendavyo.

Na huo ndio demokrasia ya CCM miaka yote huku akiwatisha na wale waapiga kura wachache waalio hai wasijitokeze. Kwa misingi hii inamaanisha kwamba Tanzania hatujawahi kuwa na kitu
FREE AND FAIR ELECTIONS isipokua geresha tu.
 
Trend inaonyesha kuwa idadi ya wapiga kura inapungua., uchaguzi mkuu 2010 ni karibu 42% ndio waliopiga kura, uchaguzi wa Igunga sina Takwimu sahihi ila napo ni almost 50% hawakupiga kura,. uchaguzi wa juzi wa Uzini pia karibu nusu hawajapiga kura?? kulikoni?? daftari la wapiga kura lipo sahihi kweli au kuna namna limefanyiwa manuva???
 
Back
Top Bottom