Kwanini Watanzania hatuna Ukabila lakini tunapenda kujua unaezungumza nae ni kabila gani

yaani utambulisho wowote mitaani ushwahili au vijijini achilia mbali makanisani utakuwa haujakamilika kama mgeni hajajulikana ni kabila gani.

japo swali hilo huulizwa kwa nia njema lakini binafsi huwa naona kero kubwa.
kuna watu maofisini bila hata kugundua utajikuta wameshafanya viutafiti na kujua kila mtu pale ni kabila gani.
Madhara yake wakishajua ni kabila gani chochote utakachofanywa kitahusianishwa na kabila lako na sio wewe kama mwanadamu hai mwenye uwezo huru wa kuchagua cha kufanya.

unadhani chanzo ni nini na nini suluhisho?
anaweza akawa ni ndugu yako
 
Naomba nikuulize unajua au kuelewa vyema maana ya ukabila???[/QUOTED]
loyalty to a tribe or other social group especially when combined with strong negative feelings for people outside the group.
hii ni moja ya maana.unaweza kutoa elimu kama unakitu chaziada
 
nakubaliana na wewe mkuu.
TATIZO linaanza pale mtu anapojua wewe ni kabila gani aanze kuleta maneno maneno na kulazimisha mwenendo wako kuwa ni zao la kabila lako na sio maamuzi yako binafsi na taratibu ulizojiwekea wewe mwenyewe.
naunga mkono watu kuongea lugha zao na mfano mzuri ni jiji la mwanza. pale mjini utasikia watu wa lugha moja wakiongea bila wasiwasi katikati ya jiji.mfano wakurya,waha,wajita,wajaluo,wasukuma,wakelewe,wakara,wahaya.

Tatizo pia ni pale inapotokea coincidence watu wa kabila moja bila kupanga kuonyesha uwezo na kuchukua nafasi za juu mfano. Wengine wote hawataangalia uwezo wa wale watu bali ufanano wao kikabila. hii nayo sio sawa.
Mambo ya kusema huyu kabila fulani hivyo atakuwa hivi ni ujima.

Mimi upande wa baba Msukuma, kaja Pwani zamani kusoma. Tanzania mimi nimezaliwa na kukulia Dar, mama mtu wa Uzaramo, kwa hiyo huku Pwani kwetu pia, sijakaa sana nimeondoka Tanzania kwenda kusoma Chuo Marekani, nimekaa Marekani miaka 20 sasa.

Mimi Msukuma Mzaramo Mtanzania wa Dar na Marekani kabila lolote utakalonipa halitanifaa.

Iam a citizen of the world.

I refuse to be pigeon holed.
 
Msingi Wa kuuliza Kabila ni Ubaguzi.., na mara nyingi huwa tunabaguana kwa Makabila bila kujijuwa!!!
 
Back
Top Bottom