Kubwajinga
JF-Expert Member
- Jan 23, 2008
- 2,194
- 297
1. Kwanini ukweli usisemwe? Si Mkoloni pekee, na wale walioachiwa na Mkoloni wameendeleza, msome Sivalon, Bergen hao wote ambao wewe kwako si matapeli huyo Sheikh anatowa reference, unaweza kuwanukuu japo kidogo kuhusu elimu?
2. Huna uwezo wa kutatua tatizo bila kujuwa chanzo chz tatizo.
3. Wapo wengi tu, wala usiwe na shaka, tulibanwa zamani, sasa tunaibuwa madudu mpaka NECTA. Hujaona? basi hata hujasikia? Hata Slaa hana degree yoyote lakini ana PhD, kwi kwi kwi teh teh teh! kuta nne siyo mwisho au mwanzo wa elimu, huo ni mwanzo wa kuwa "programmed" kama unavojidhihirisha.
4. Ullipoamka wewe, wenzako ndipo walipolala, mwenyewe unaona umetowa wazo la maana? soma hapa: Tanzania Muslim Professionals
Mkuu Zomba,
Kwanza nashukuru kwa kujibu hoja zangu kwa kiasi ulichoweza. Ningependa tuendelee kuelimishana kama tu tutakuwa wastaarabu kwenye maandiko yetu maana tuko kwenye Great Thinkers Forum na hoja tunayojadili ina maingiliano na dini na hivyo ni muhimu kutojadili kwa jazba bali kwa kutumia facts.
- Kutoa reference haina maana unachoongea kinaukweli au kina mahusiano na hizo references. Ndio maana yule 'Shehe' hakunukuu aya yoyote kwenye hivyo vitabu alivyo-refer bali alivitumia kama viini macho (references on the fly). Ningekushauri uvisome kabla hujaweka imani yako mikononi mwake na pia usome materials nyingine kama hii thesis ya Bwana Abdin Noor Chande niliyoibandika hapo juu. Hakuna mtu mwenye umiliki wa ukweli bali facts ndio zinazotofautisha claims za ukweli wa watu wasiokubaliana.
- Ni kweli kujaribu kutatua jambo bila kujua chanzo unaweza usipate ufumbuzi mzuri. Lakini ni vema pia ukaelewa historia kwa kusoma wewe mwenyewe na kujua facts, na sio kwa kusikiliza na kuyumbishwa na hotuba za watu wanaojifanya wajuzi kumbe ni mbwembwe zao tu kwa ajili ya ulaji na wengine wakiwa na nia mbaya na nchi.
- Nafikiri pia ni kosa kuwafikiria Watanzania wenzako kama 'sisi' na 'wao'. Tuwe wamoja maana hatuwezi kuigawa nchi kwa vile tumechanganyika.
- Halafu sidhani kama Nyerere yule yule aliyezifungua shule za Wamisionari kwa Wananchi wote awe eti ndio huyo huyo aliyebuni mbinu ya kuwaminya waislamu elimu. Kuna msemo unosema kuwa "unaweza kumpeleka farasi mtoni lakini huwezi kumlazimisha kunywa maji". Nyerere alifungua milango kwa waislamu lakini kwa sababu fulani fulani hawakusonga mbele haraka.
- Natumaini kuwa wewe huna fikra za kuwa kumekuwa na mbinu za serikali kuwaminya waislamu elim dunia. Kama unajua jinsi ya ku-program au hata kuandika tu formula za kawaida kwenye MS Excel au spreadsheet yoyote, utaelewa vema kilichotokea hapo NECTA. Lakini kama huelewi hizo software zinavyofanya kazi, basi inaweza ikawa rahisi kwako kukubali hizi conspiracy theories za kwamba waislam wanaonewa na NECTA. Binafsi sidhani kama idara nzima iliyojaa waislam na wakristo inaweza kufanya upuuzi wa kuwafelisha waislam tena kwenye somo ambalo ni la kwao tu na hawana ushindani nalo na wakristo.
- Nimeiangalia hiyo www ya TMP na nilichoona sikukifurahia. Ingawa siwajui wenye hicho kikundi, lakini sikuona chochote kinachoonyesha kuwa wana nia njema na waisalamu. Kwa mfano, nimeona wameandika kuwa wanataka kuwasaidia umma kwa kuwapatia ajira, lakini ni lazima kila anayetafuta msaada awalipe TShs 10,000. Huu ni utapeli.