Kwanini vijiji vingi vya usukumani havina wezi kama kwingineko?

Mwalusembe, wizi, uchawi, umalaya, umbeya vyote vyao.

Kile kijiji sijui kimelaaniwa na nani ?

Nimewahi kukaa hapo 2015-2017 nilikuwa nalima matikiti maji kijiji cha Kikoo picha linaanza ile kufikisha watu wangu wa kazi wote wakaugua macho kila siku wanatoa machozi tu, usiku ndani vurugu haziishi. Ikabidi niwahamishie shambani huko huko hapo mwalusembe siyo.
Kuna mdau wangu anaheka saba hapo, aliniarika nichukue eneo karibu yake ili tuwe na eneo hapo majirani, kumbe wale jamaa nao ni balaa. Nimewahi kukaa masaa kama 12 tu mama mmoja akapewa namba yangu..Kila siku ni kubeep na kunipigia hadi nikablock
 
1. Pesa/mali kila mtu anayo ya kutosha siyo kama zile sehemu za wazee wa sokoni 7days/week.
2. Hawana tamaa za hovyo hovyo juu ya mali ya mtu
3. Maadili mema ni jadi yao
Kuwa kabila moja kunasaidia mikoa mingine kama mkoa wa Mara wanaibiana sababu ni makabila tofauti na wana uadui kati ya kabila moja na lingine na wanapakana na wakenya wezi wakubwa wa mifugo
 
Wasukuma oyeee,
Kweli ni wachapa kazi, wakarimu, utani mwingi, na waanzilishi wa sungusungu. Ukujikanganya ukapelekwa kwenye mahakama yao utataja mpaka uhalifu aliofanya babu yako.
Mfumo wao wa utawala wa wanazengo uko vizuri sana kudhibiti uhalifu na kudhibiti mtu kuto behave kijijini kinyume na maratajio ya wanakijiji

Kuna mfanyabiashara alifungua duka kubwa tu kijijini aligoma kwenda kujitolea kutengeneza barabara wakati mkutano wa kijiji wa wanazengo ulikubaliana kuwa jumamosi waende kutengeneza watu waende na majembe nk

Akagoma akasema hiyo ni kazi ya serikali inayopokea kodi hataenda.Wanakijiji yaani wanazengo wakalima barabara baadaye kikaitishwa kikao kumjadili wakakubaliana kumuadhibu.Kuwa ni marufuku mtu yeyote kwenda kwenye duka lake au kumtembelea au kuajiriwa naye .Atakayeonekana kukaidi atalipishwa faini elfu 70 na kutengwa na jamii

Yeye akatakiwa alipe laki tano kama faini ya kukaidi maamuzi ya kijiji ya wanazengo na aombe msamaha kwenye mkutano wa kijiji ili watu waruhusiwe kwenda dukani kwake
Mwezi mzima hakuna mtu alikanyaga dukani kwake akaona eee hii kesi mbaya akawalipa laki tano yao wakaendelea kwenda dukani kwake Umoja wao kwenye vijiji vyao una uwezo mkubwa sana kuzuia uhalifu
 
Kweli wanaungwana sana japo wapo wenye tabia za hovyo lakini wengi ni watu wema tu
Wapo wabaya pia ila majority ni wema sana especially vijijini
Kuna minada nilikuwa naenda utakuta ni wao tu wanakuambia weka makoti na kila kitu hapo maana hakuna waizi hapa
Nikawauliza ikitokea nimeibiwa kitu ?
Akasema atasakwa mwizi na kuchomwa moto hii ni baada ya watu kuanza kuchanganyika
 
Mfumo wao wa utawala wa wanazengo uko vizuri sana kudhibiti uhalifu na kudhibiti mtu kuto behave kijijini kinyume na maratajio ya wanakijiji

Kuna mfanyabiashara alifungua duka kubwa tu kijijini aligoma kwenda kujitolea kutengeneza barabara wakati mkutano wa kijiji wa wanazengo ulikubaliana kuwa jumamosi waende kutengeneza watu waende na majembe nk

Akagoma akasema hiyo ni kazi ya serikali inayopokea kodi hataenda.Wanakijiji yaani wanazengo wakalima barabara baadaye kikaitishwa kikao kumjadili wakakubaliana kumuadhibu.Kuwa ni marufuku mtu yeyote kwenda kwenye duka lake au kumtembelea au kuajiriwa naye .Atakayeonekana kukaidi atalipishwa faini elfu 70 na kutengwa na jamii

Yeye akatakiwa alipe laki tano kama faini ya kukaidi maamuzi ya kijiji ya wanazengo na aombe msamaha kwenye mkutano wa kijiji ili watu waruhusiwe kwenda dukani kwake
Mwezi mzima hakuna mtu alikanyaga dukani kwake akaona eee hii kesi mbaya akawalipa laki yao wakaendelea kwenda dukani kwake Umoja wao kwenye vijiji vyao una uwezo mkubwa sana kuzuia uhalifu
Hatari sana.
Nimeona kijiji kimoja walikuwa wanatii amri ya serikali kujenga maboma ya madarasa ili wao waje wamalizie. Jamaa walikomaa kila familia inaleta mchanga, kwa punda wengine wanabeba vichwani, wakachanga cement ufundi na vibarua wakajitolea yaani ndani ya mida mfupi madarasa ya kutosha na nyumba za waalimu maboma yakakamilika. Kijiji kimoja kiko mkoa wa geita.
 
Nimewahi kuishi usukumani,kule kuna ulinzi shirikishi aidha mgeni yeyote akija lazima areport kwa mwenyekiti wakijij na pia bado wanaheshimu mila na desturi (wazee wanaheshima bado mbele ya jamii).kuna jamaa mmoja akihisiwa kutunza wezi aiseeee nilishuhudia kwa macho yangu akicharazwa viboko hadi akajinyea mbele ya umati wawatu na akatozwa faini ya ng'ombe wawili palepale akatubu mbele ya halaiki yawatu kua hatarudia.
 
Hatari sana.
Nimeona kijiji kimoja walikuwa wanatii amri ya serikali kujenga maboma ya madarasa ili wao waje wamalizie. Jamaa walikomaa kila familia inaleta mchanga, kwa punda wengine wanabeba vichwani, wakachanga cement ufundi na vibarua wakajitolea yaani ndani ya mida mfupi madarasa ya kutosha na nyumba za waalimu maboma yakakamilika. Kijiji kimoja kiko mkoa wa geita.
Mtu akitaka kujua nguvu za serikali za vijiji aende usukumani kule ndiko wanajua maana ya serikali ya kijiji ni nini.Kuwa ni serikali kamili na serikali kwelikweli sio utani
 
Mtu akitaka kujua nguvu za serikali za vijiji aende usukumani kule ndiko wanajua maana ya serikali ya kijiji ni nini.Kuwa ni serikali kamili na serikali kwelikweli sio utani
Jamaa wako siriasi sana. Hasa ukikuta wanajeshi la jadi sungusungu na kuongozi wao Sumbantale.😁😁
 
Niliona vijana wanawacheka graduates. Yaani dogo Kamaliza STD7 anauwezo wa kununua Boda. Shamba la familia lipo, ngombe na zana zipo yeye ni bidii yake.

Uwezekano wa kupata pesa kama.mvua ipo unakuwa mkubwa, ukimuambia asome ili aje apate pesa, alafu anamuona graduate ni masikini kuliko yeye mzee hakuelewi.
Hili la graduate kukosa mipango ya kusaka mahela ni suala linafikirisha sana. Nafikiri graduate wengi ni wachagua jembe, hivyo sio wakulima. Namaanisha wengi ni wachagua kazi badala ya kuwa direct kwenye kusaka noti. Graduates wabadili fikra!
 
Nimekaa vijiji kadhaa, na kupita katika harakati zangu nimeona tofauti kubwa.

Usukumani ndani kabisa vijijini hakuna wiziwizi wa ajabu.

Huwezi kusikia wizi wa mifugo.
Watu wanaweka magunia ya mipunga bila ulinzi wa kutisha na unayakuta.

Cha ajabu hata vijiji vya wasukuma waliohamia Sumbawanga na Morogoro hivyohivyo.

Unatembea usiku hakuna mtu mwenye hamu ya kukukaba. Ukisahau pembejeo shambani unazikuta.

Jamaa wengi sio wezi, babda utokee ukame na kuwe na baa la njaa. Ila kwingineko huko tunakopitapita jamaa ni wepesi sana, tena ukiwa mgeni lazima uonewe.

Nini chanzo cha hii kitu
Uchapakazi ndio unawafanya wasiwe wajanjawajanja kama Wazaramo! Kila mtu anaridhika na alichonacho!
 
Mtu unaamka saa tisa usiku na sheli yako unalima mpaka saa tatu hapo unatoka shamba ng,ombe wakapumzike na wapate malisho ww unarudi shamba kurendelea kusaidia wapandaji mda unao kuja kupata kupumzika ni usiku na tena ni masaa machache huo mda wa kuwaza ukaibe cha mtu unaupata wapi.Hata tukisha vuna ndo mda mzuri wa kutembelea ndugu na jamaaa na kwenda kuuza mazao mwaka mzima unakuta tuko bize.Sasa huku pwani mtu anaamka hana kazi ya kufanya akiona hata chuma chakavu tu kwa jirani limekaa kihasara anapita nalo akauze screpa.Wazee wetu nawapongeza sana kutupa akili ya kupenda kufuga na kilimo ndo maana mikoa yote lazima ukutane na wasukuma na lazima utawakuta wanapambna sana
ongw'ise ogonojwa na bhagokolo bhenabha,onsambo lokwe lofuu kwisha habar!
 
Back
Top Bottom