naggy
Member
- Apr 27, 2011
- 97
- 152
Mimi si mtaalamu wa sheria lakini napata wasiwasi kwa kutumia ufahamu wa kawaida. Kuna uhalari gani wa kurejea kwenye vifungu vya katiba ambayo sote tumeiona haifai, kutengeneza katiba itakayokidhi matakwa ta wananchi? Ni kweli, kwa mujibu wa katiba ya sasa rais ana mamlaka makubwa sana na ni halari kwa yeye kufanya kama mswaada uliopitishwa unasema. Lakini tukumbuke hatuwezi kutumia malighafi mbovu, iliyooza, isiyo na ubora, kutengeneza bidhaa bora. Kwamba haramu haiwezi kuzaa halari hata siku moja. Sote hili tunalifahamu, wanaccm wanalifahamu, hata rais pia analifahamu. Halihitaji mtu awe na elimu ya chuo kikuu, just logic- simple reasoning. Hata sisi tunaoupinga huu mswaada wa mchakato wa kupata katiba mpya hatujaliweka wazi hili katika kutetea hoja zetu. Nahisi hili tulitumie kutetea hoja zetu za kuupinga mswaada unaotegemewa kusainiwa. Mchakato huu ulipaswa uwe huru kabisa, tukitumia matakwa ya wananchi kama ndo mwongozo wa kutengeneza mchakato, na si katiba na taratibu zilizopo.
Swala la mamlaka makubwa ya rais ni swala moja kubwa linalopigiwa kelele kwenye katiba ya sasa. Na kwamba katiba mpya tunayotegemea kuiunda hakika hatutegemei rais awe na mamlaka makubwa kiasi hicho. Tukikubari rais atumie mamlaka makubwa aliyonayo katika mchakato huu, kuna hatari ya kupata katiba ambayo haitakuwa na tofauti sana na iliyopo. Kwamba, ingekuwa ni bora zaidi kufanya marekebisho ya katiba kwa baadhi ya vifungu kuliko kutumia gharama kubwa kwa kufanya kiini macho cha kukidhi haja ya wananchi ya kutaka katiba mpya. Napatwa na wasiwasi kwamba rais wetu, mawaziri wake na wabunge wake wote, kama kweli wanadhamira ya kweli ya kuunda katiba mpya. Nahisi wanataka kufanya kiini macho tu. Kulikuwa na tatizo gani mswaad huu kuusoma kwa mara ya kwanza? Kuna tatizo gani la kuwaacha wananchi wao wenyewe waamue namna ya kupata katiba mpya? Kwa nini wabunge wa ccm wameshupaa kuutetea? Nalazimika kuamini kwamba kuna ajenda ya siri hapa tunayopaswa kuipinga kwa pamoja.
Lakini ndo hivyo, wamepitisha, na rais kasema atausaini katika hotuba yake jana akiongea na wazee wa Dar es Salaam. Swali muhimu la kujiuliza TUTAFANYAJE KUZUIA HIZI NJAMA ZA SERIKALI KUUTEKA MCHAKATO WA KUPATA KATIBA MPYA? KILICHOAMULIWA KUFANYWA NA JUKWAA LA KATIBA NA WANA CHADEMA NA NCCR KITAFANIKIWA? KISIPOFANIKIWA TUTAFANYAJE? Kwa jukwaa la katiba na vyama vya upinzani(CDM na NCCR) TUNAFAHAMU AINA YA WATANZANIA TULIO NAO AMBAO NDIYO MTAJI WA KUFANIKISHA HAKI AMBAYO WENGI WANAITAKA (PEOPLES' POWER)? Tusaidiane kwa haya.
Nawasilisha!
Swala la mamlaka makubwa ya rais ni swala moja kubwa linalopigiwa kelele kwenye katiba ya sasa. Na kwamba katiba mpya tunayotegemea kuiunda hakika hatutegemei rais awe na mamlaka makubwa kiasi hicho. Tukikubari rais atumie mamlaka makubwa aliyonayo katika mchakato huu, kuna hatari ya kupata katiba ambayo haitakuwa na tofauti sana na iliyopo. Kwamba, ingekuwa ni bora zaidi kufanya marekebisho ya katiba kwa baadhi ya vifungu kuliko kutumia gharama kubwa kwa kufanya kiini macho cha kukidhi haja ya wananchi ya kutaka katiba mpya. Napatwa na wasiwasi kwamba rais wetu, mawaziri wake na wabunge wake wote, kama kweli wanadhamira ya kweli ya kuunda katiba mpya. Nahisi wanataka kufanya kiini macho tu. Kulikuwa na tatizo gani mswaad huu kuusoma kwa mara ya kwanza? Kuna tatizo gani la kuwaacha wananchi wao wenyewe waamue namna ya kupata katiba mpya? Kwa nini wabunge wa ccm wameshupaa kuutetea? Nalazimika kuamini kwamba kuna ajenda ya siri hapa tunayopaswa kuipinga kwa pamoja.
Lakini ndo hivyo, wamepitisha, na rais kasema atausaini katika hotuba yake jana akiongea na wazee wa Dar es Salaam. Swali muhimu la kujiuliza TUTAFANYAJE KUZUIA HIZI NJAMA ZA SERIKALI KUUTEKA MCHAKATO WA KUPATA KATIBA MPYA? KILICHOAMULIWA KUFANYWA NA JUKWAA LA KATIBA NA WANA CHADEMA NA NCCR KITAFANIKIWA? KISIPOFANIKIWA TUTAFANYAJE? Kwa jukwaa la katiba na vyama vya upinzani(CDM na NCCR) TUNAFAHAMU AINA YA WATANZANIA TULIO NAO AMBAO NDIYO MTAJI WA KUFANIKISHA HAKI AMBAYO WENGI WANAITAKA (PEOPLES' POWER)? Tusaidiane kwa haya.
Nawasilisha!