Mbogela
JF-Expert Member
- Jan 28, 2008
- 1,384
- 257
Sina uhakika kama hii thread niianzishe kwenye jukwaa la habari za kimataifa au hapa.
Kama tunavyojua kuwa Tanzania imekuwa mstari wa mbele kwenye suala la ukombozi wa bara la Afrika. Tumesaidia kukomesha ukoloni, kutawaliwa na ubaguzi wa rangi kwa nchi zilizoko kusini mwa bara la afrika. Pia tumewasaidia Polisalio, tumesaidia Uganda, na nchi zote za ukanda wa maziwa makuu kutatua migogoro yao (ingawa hili la kuwauzia siraha tena, mmh! linatia doa). Tumepeleka majeshi yetu kulinda amani kwenye nchi zenye matatizo ya migogoro ya wenyewe kwa wenyewe. Bila kusahau operation ya JWTZ hivi karibuni huko Anjouan.
Lakini pamoja na yote hayo sasa hivi kuna tishio kubwa tishio jipya, tishio linalohatarisha sio usalama wa majirani zetu lakini ni tishio linaloweza kuua biashara na mahusiano yetu na dunia nyingine. Tatizo linalofanya kuwe na makonteina yanayopita ndani ya aridhi yetu kama yana mizigo kumbe ndani yamebeba watu wanaokimbia nchi yao.Tatizo hili ni tatizo katika ghuba ya Aden, iliyoko kwenye pembe ya Afrika. Naliona ni tatizo kutokana kuongezeka kwa vitendo vya utekaji nyara wa meli zinazotoka au kuja pwani ya afrika mashariki.
Kitendo cha maharamia wa kisomali kuendelea kupata malipo kutokana ana utekaji nyara wa meli hizo na raia wa kigeni hakitaisha leo wala kesho kama hatua za makusudi hazitachukuliwa. Maharamia wanajua kabisa kuwa hawawezi kukamatwa wala kushindwa kutoka na miundo mbinu yao waliyojiwekea ndani ya Somalia.
Lakini nadhani, kama Tanzania ikiamua, Kama Tanzania itadhamiria kweli uwezekano wa kumaliza tatizo la Somalia upo na unatekelezeka.
Kama ningekuwa waziri wa ulinzi wa JMT leo hii ningemshauri amiri jeshi mkuu, JK, kuanza operation maalumu ya kuisaidia Somalia. Kuisaidia Somalia kuwa na serikali yake imara yenye nguvu na jeshi imara lenye adabu na utiikwa serikali yao.
Ningemshauri Tanzania ianzishe kambi maalumu za mafuzo kwa vijana wa kisomali ambao watakuwa tayari kulitumikia jeshi jipya la nchi yao. Vijana hawa wawe recruited na kupigwa msasa kabambe ndani ya aridhi ya Tanzania, wapewe mafunzo ya kijeshi na kinadharia ya kuipenda nchi yao na kujua umuhimu wa kuwa na serikali yenye nguvu.
Kama tunaweza kufanikiwa kuzishawishi na nchi zingine kama South Afrika, Msumbiji, Zambia nk kila nchi ikazalisha wanajeshi wa kisomali sema kwa miaka mitatu mfululizo, kama kila mwaka tunatengeneza asikari 50,000 na nchi zingine zikafanya hivyo, ningekuwa na uhakika kuwa ifikapo mwaka 2015 hakuna tatizo la utekeji nyara meli na watu wasio hatia pwani ya Somalia.
Naamini nchi zilizoendelea zipo tayari kutoa michango na misaada kutaka kusaidia kuhakikisha kuwa Somalia inatawalika, kwani nazo zimechoka kuendelea kutengeneza vichwa vya habari kwenye media kutokana na watu wao kila siku kutishiwa kukatwa vichwa na magaidi wa kisomalia. Obama angefurahi sana mpango huo kwani ungemsaidia kuibomoa ngome mpya ya Al Qaeda inayodaiwa kuanza kujengwa kwenye nchi isiyo na serikali wala jeshi, angetoa support. Na Tanzania ingepata kujenga uhusiano wake na marafiki zake wa nje kwa ukaribu zaidi. Tanzania inaweza, nia na sababu tunazo, tuwasaidie wasomalia jamani!!!!
Kama tunavyojua kuwa Tanzania imekuwa mstari wa mbele kwenye suala la ukombozi wa bara la Afrika. Tumesaidia kukomesha ukoloni, kutawaliwa na ubaguzi wa rangi kwa nchi zilizoko kusini mwa bara la afrika. Pia tumewasaidia Polisalio, tumesaidia Uganda, na nchi zote za ukanda wa maziwa makuu kutatua migogoro yao (ingawa hili la kuwauzia siraha tena, mmh! linatia doa). Tumepeleka majeshi yetu kulinda amani kwenye nchi zenye matatizo ya migogoro ya wenyewe kwa wenyewe. Bila kusahau operation ya JWTZ hivi karibuni huko Anjouan.
Lakini pamoja na yote hayo sasa hivi kuna tishio kubwa tishio jipya, tishio linalohatarisha sio usalama wa majirani zetu lakini ni tishio linaloweza kuua biashara na mahusiano yetu na dunia nyingine. Tatizo linalofanya kuwe na makonteina yanayopita ndani ya aridhi yetu kama yana mizigo kumbe ndani yamebeba watu wanaokimbia nchi yao.Tatizo hili ni tatizo katika ghuba ya Aden, iliyoko kwenye pembe ya Afrika. Naliona ni tatizo kutokana kuongezeka kwa vitendo vya utekaji nyara wa meli zinazotoka au kuja pwani ya afrika mashariki.
Kitendo cha maharamia wa kisomali kuendelea kupata malipo kutokana ana utekaji nyara wa meli hizo na raia wa kigeni hakitaisha leo wala kesho kama hatua za makusudi hazitachukuliwa. Maharamia wanajua kabisa kuwa hawawezi kukamatwa wala kushindwa kutoka na miundo mbinu yao waliyojiwekea ndani ya Somalia.
Lakini nadhani, kama Tanzania ikiamua, Kama Tanzania itadhamiria kweli uwezekano wa kumaliza tatizo la Somalia upo na unatekelezeka.
Kama ningekuwa waziri wa ulinzi wa JMT leo hii ningemshauri amiri jeshi mkuu, JK, kuanza operation maalumu ya kuisaidia Somalia. Kuisaidia Somalia kuwa na serikali yake imara yenye nguvu na jeshi imara lenye adabu na utiikwa serikali yao.
Ningemshauri Tanzania ianzishe kambi maalumu za mafuzo kwa vijana wa kisomali ambao watakuwa tayari kulitumikia jeshi jipya la nchi yao. Vijana hawa wawe recruited na kupigwa msasa kabambe ndani ya aridhi ya Tanzania, wapewe mafunzo ya kijeshi na kinadharia ya kuipenda nchi yao na kujua umuhimu wa kuwa na serikali yenye nguvu.
Kama tunaweza kufanikiwa kuzishawishi na nchi zingine kama South Afrika, Msumbiji, Zambia nk kila nchi ikazalisha wanajeshi wa kisomali sema kwa miaka mitatu mfululizo, kama kila mwaka tunatengeneza asikari 50,000 na nchi zingine zikafanya hivyo, ningekuwa na uhakika kuwa ifikapo mwaka 2015 hakuna tatizo la utekeji nyara meli na watu wasio hatia pwani ya Somalia.
Naamini nchi zilizoendelea zipo tayari kutoa michango na misaada kutaka kusaidia kuhakikisha kuwa Somalia inatawalika, kwani nazo zimechoka kuendelea kutengeneza vichwa vya habari kwenye media kutokana na watu wao kila siku kutishiwa kukatwa vichwa na magaidi wa kisomalia. Obama angefurahi sana mpango huo kwani ungemsaidia kuibomoa ngome mpya ya Al Qaeda inayodaiwa kuanza kujengwa kwenye nchi isiyo na serikali wala jeshi, angetoa support. Na Tanzania ingepata kujenga uhusiano wake na marafiki zake wa nje kwa ukaribu zaidi. Tanzania inaweza, nia na sababu tunazo, tuwasaidie wasomalia jamani!!!!