Kwanini Karume?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,478
39,997
Sijui kama wenzangu mlinotice au la.. hivi kwanini Karume apewe heshima ya Kijeshi Tanzania bara na kupokea saluti kwenye siku kuu ya Mashujaa wakati nafasi yake kwenye baraza la mawaziri wa Muungano ni kama waziri tu? Wakati Rais na Makamu wake hawapo nchini anayefuatia ni Waziri Mkuu na hakuna mahali hata pamoja panapompa Rais wa Zanzibar protokali hiyo. Waziri Mkuu yupo Dar kwanini Karume asimame kama vile ni kiongozi wa Muungano??? Hizi nazo ni kasoro za muungano wetu!!!!

726.jpg
 
Mwanakijiji,
Hata mimi nafikiri ilikuwa ni makosa kwa Raisi wa Zanzibar kumuwakilisha Raisi wa Jamhuri ktk sherehe za Mashujaa. Kwa sababu Raisi na Makamu wake walikuwa nje ya nchi, kikatiba Waziri Mkuu ndiye aliyekuwa akikaimu nafasi ya Raisi wa Muungano.Labda Waziri Mkuu naye alikuwa na udhuru.

Sioni kama hii ni kasoro ya Muungano, nadhani hapa ni wahusika kutokuifahamu au kuidharau Katiba.
 
Mzee Mwanakijiji,
Mkuu wa Itifaki, Balozi Cisco Mtiro, yuko chini ya wizara ya mambo ya nje. uamuzi wa Amani Karume kumwakilisha Raisi wa Muungano nahisi umefanywa na mtu mkubwa zaidi ya Balozi Mtiro.
 
Sasa hivi hakuna cha Itifaki wla nini ni Kasi mpya mwendo mpya mavirigiza mapya na viringavirnga upya, serikali ya JK imejaa watu wanaotafuta hela tu!!
Ana kazi kweli, labda tumuangalie miaka mitano ijayo kama atabadilika kwasasa anasoma mambo yanavyoenda
 
JokaKuu, nitasahihishwa, lakini sidhani Mkuu wa Itifaki ya Mambo ya nje anahusika na Itifaki ya Rais au Ikulu. Nafikiri Ikulu wana mkuu wao wa Itifaki...
 
Back
Top Bottom