Chiya Chibi
JF-Expert Member
- Jul 6, 2011
- 484
- 110
Naomba nisizunguke sana waungwana, kuna jamaa zangu wamepata wagen kutoka kule wabongo wenzetu walipoficha Fedha na wameamua wajifunze kiswahili kwa huu muda wataokuwa nchini. Sasa kuna maneno yamewatatiza sana na hata sis wenyeji imetutatiza pia, nadhan inatokana kusoma masomo mengine (sayans) kuliko lugha yetu.
- Kwanin 'a Dog' iandikwe MBWA badala ya MMBWA??
- Kwanin 'Outside' iandikwe NJE badala ya NNJE??
- Na kama hivyo ndivyo kwanin 'country, iandikwe NCHI badala ya CHI??