Mwande na Mndewa
JF-Expert Member
- Feb 26, 2021
- 949
- 2,865
KWAKO MH LUSINDE NA MH KENANI;DK BASHIRU ALIWAHI KUSEMA MANENO HAYA AKIWA KATIBU MKUU WA CCM,JE HAMKUMUELEWA ENZI ZILE!?
Leo 17:50hrs 20/11/2022
1. "Nimekuta wizi wa kutisha kwenye chama chetu cha CCM na wengine nikiwataja hamtanielewa. Wanajifanya ni waheshimiwa kumbe ni wezi,mijizi,wameiba magari, wameiba ardhi. Ukiwaskia nje wanabwatuka unawezakudhani ni wazalendo kumbe ni mijizi na kwenye vikao mkikaa hata kabla hamjafikia maamuzi, mijizi hiyo inatoka nje".
2. "Mijadala ndio namna ya kuendeleza nchi yetu, mijadala ndiyo inatufanya tujisahihishe. Hatuwezi kusonga mbele bila mijadala. Tumekosea sana katika nchi yetu, tumepotea sana katika nchi yetu. Mbaya zaidi tumeanza kuogopa kusema ukweli, lazma tubadilike".
3. "Tuambizane ukweli; kuanzia sasa CCM haitachukua tena wanamuziki kwaajili ya kampeni za chaguzi. Hivi wananchi mkiishapewa kofia na fulana halafu nyimbo za "mbele kwa mbele" zikapigwa, huwa mnapata nafasi ya kuhoji sifa za mnayetaka kumchagua? Wanamuziki wanakichaji chama fedha nyingi na wanafaidika wao na matumbo yao. Hivyo, kuanzia sasa hakuna tena kitu kama hicho";
4. "Wapigakura wajanja wameanza tabia ya kudharau chaguzi. Wanabaki nyumbani kwani wanaona chaguzi ni kituko, ni mchezo wa kuigiza. Ndio maana leo kupata watu wa kwenda kupiga kura imekuwa shida. Note CCM tunakoshinda ni chini ya 30%, chini ya 40% . hakuna mahali ambako wapigakura wamejitokeza kwa 50%. na mwaka 2010 ulitia fora. Watu wengi walijiandikisha kumbe walikuwa wanataka kile kiparata (kitambulisho cha mpigakura) kwasababu huwa kinatumika polisi kumwekea mtu dhamana. Wakiishakipata wanaingia mitini. Kwa mara ya kwanza katika historia nchini, mwaka 2010 tukapata serikali ambayo haina uhalali wa kisiasa kwasababu 50% ya wapigakura walibaki nyumbani".
5. "Msimu wa uchaguzi umekuwa msimu wa rushwa. Imefika mahali wagombea wanauza adi nyumba. Wengine wanaomba sana michango. Usipomchangia anakuwa mkali na kununua uso utadhani anakwenda kutibiwa,akiishazikusanya fedha anakwenda kuwanunua mawakala, nao wanawanunua wananchi. Wananchi mnachotakiwa kufanya ni kubomoa soko la kura".
6. "Napenda kuwafahamisha kwamba Hussein Bashe sio mkorofi bali ni miongoni mwa wabunge wa CCM wadadisi,kuna tofauti kubwa kati ya mdadisi na mkorofi,Bashe na Nape Nnauye ni miongoni mwa wanachama wetu wadadisi na wanasaidia kulichangamsha bunge ila wanatofautiana katika udadisi wao. Nape kidogo ana joto zaidi kuliko Bashe. Wote nawafahamu vizuri hivyo msidanganywe kuwa Nape na Bashe ni watukutu. Sio watukutu, ni wadadisi na wamewezesha mawaziri kufikiri kabla ya kutenda. Kutenda kila mmoja anawezakutenda, hata mwendawazimu anaweza kutenda lakini ili uweze kutenda kwa ufanisi na tija lazma ufikiri. Michango ya Bashe bungeni inafikirisha".
7. "Mimi ninachosisitiza ni nidhamu na si kunyamazisha watu. Tutapata wapi fikra mpya bila kuhojiana, bila kujadiliana na bila kudadisi? Tusipofanya hivyo, Chama Chetu cha Mapinduzi kitakuwa chama mfu".
8. "Nilikuwa Morogoro na akatajwa Waziri kuwa anamiliki hekari 1000. Watu wanatakakujua amezipataje na mi ntamwita waziri huyo nimuulize kusudi nikawajibu walioniuliza. Hatuwezi kuwa na viongozi ndani ya chama kinachojitambulisha kama chama cha wanyonge halafu baadhi yetu tunapora ardhi ya wanyonge. Ni suala la kuchagua kati ya kuwa Kiongozi wa CCM au kuwa Mporaji wa ardhi".
9. "Na hii habari ya "Dar Es Salaam ya Makonda" sio sahihi. Hakuna "Dar es Salaam ya Makonda" ni "Dar we Salaam chini ya Mkuu wa mkoa wa Dar Es Salaam, Makonda". Kuna wakati huwa namsikia Makonda akasema "Wananchi wangu", nani kamwambia ana wananchi wake? Hakuna wananchi wako,hakuna kiongozi anamiliki wananchi, ni "wananchi wenzangu". Mwalimu Nyerere aliwahi kuonya juu ya ubinafsi .."mkianza kusema- mimi, wewe, sisi au wao hamfiki". Vongozi vijana mnapaswa kuwa wanyenyekevu na kuacha papara. Vinginevyo mtapotea kama walivyopotea viongozi wengine vijana waliopewa madaraka wakakosa unyenyekevu" .
10. "Nawashukuru sana watanzania. Nawashukuru watanzania kwa kunisomesha kwa kodi zao na hatimaye nikaweza kupata shahada zote tatu, kamwe sitawasahau watanzania,nina deni kubwa la kulipa utumishi uliotukuka. Kazi niliyopewa ya kuwa Mtendaji Mkuu katika chama ni kubwa mno".
Kwa hakika, nukuu hizi kuntu zinamtanabaisha Mh Daktari Bashiru alikuwa ni mwanadamu wa aina gani,na alidhamiria kuifanya CCM iwe chama cha aina gani,"Nitasema kweli daima fitna kwangu mwiko" tulifundishwa hivyo na Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.
-Hofu yenu iko hapa.
Mnasema huenda he is ready for the worse !! Come what may ! Che guevara alisema “ its better to die standing than to live kneeling “. !!
Shida nyingine ndani ya chama,Vigogo ndani ya chama wanajua kabla haujaanzisha vita na kamati kuu ya chama,hakikisha kwanza una back-up ya kutosha kupitia wenyeviti wa mikoa na wilaya,ukiisha kusanya hiyo support ndio twende sasa na ‘twanga, nikutwange’ mpaka ndani ya vikao vya ndani,mifano ni minyukano ya Chama tola ile dhana ya kuvua gamba hadi uchaguzi wa 2015.
Niseme tu kama mwanazuoni,maneno ya Daktari Bashiru ni Phd in delivery,Daktari Bashiru ni freemind, hategemei hisani kama ninyi, ndio maana pamoja na kupewa ukatibu mkuu wa CCM na Rais Magufuli ila bado alikuwa anaongea maneno yenye ukakasi mno dhidi ya CCM na Rais Magufuli aliyachukua hayo kama feedback na kuyatafutia solution.
Nikiishia hapa,Mimi ni
Msemakweli Chakubanga,
Dar es Salaam.
0755078854.
-Bachelor of Business Administration in International Business
-Master of Leadership and Management.
Recent Publication;-
-Assessment on the effects of Micro-Financing on Poverty Reduction.
Leo 17:50hrs 20/11/2022
1. "Nimekuta wizi wa kutisha kwenye chama chetu cha CCM na wengine nikiwataja hamtanielewa. Wanajifanya ni waheshimiwa kumbe ni wezi,mijizi,wameiba magari, wameiba ardhi. Ukiwaskia nje wanabwatuka unawezakudhani ni wazalendo kumbe ni mijizi na kwenye vikao mkikaa hata kabla hamjafikia maamuzi, mijizi hiyo inatoka nje".
2. "Mijadala ndio namna ya kuendeleza nchi yetu, mijadala ndiyo inatufanya tujisahihishe. Hatuwezi kusonga mbele bila mijadala. Tumekosea sana katika nchi yetu, tumepotea sana katika nchi yetu. Mbaya zaidi tumeanza kuogopa kusema ukweli, lazma tubadilike".
3. "Tuambizane ukweli; kuanzia sasa CCM haitachukua tena wanamuziki kwaajili ya kampeni za chaguzi. Hivi wananchi mkiishapewa kofia na fulana halafu nyimbo za "mbele kwa mbele" zikapigwa, huwa mnapata nafasi ya kuhoji sifa za mnayetaka kumchagua? Wanamuziki wanakichaji chama fedha nyingi na wanafaidika wao na matumbo yao. Hivyo, kuanzia sasa hakuna tena kitu kama hicho";
4. "Wapigakura wajanja wameanza tabia ya kudharau chaguzi. Wanabaki nyumbani kwani wanaona chaguzi ni kituko, ni mchezo wa kuigiza. Ndio maana leo kupata watu wa kwenda kupiga kura imekuwa shida. Note CCM tunakoshinda ni chini ya 30%, chini ya 40% . hakuna mahali ambako wapigakura wamejitokeza kwa 50%. na mwaka 2010 ulitia fora. Watu wengi walijiandikisha kumbe walikuwa wanataka kile kiparata (kitambulisho cha mpigakura) kwasababu huwa kinatumika polisi kumwekea mtu dhamana. Wakiishakipata wanaingia mitini. Kwa mara ya kwanza katika historia nchini, mwaka 2010 tukapata serikali ambayo haina uhalali wa kisiasa kwasababu 50% ya wapigakura walibaki nyumbani".
5. "Msimu wa uchaguzi umekuwa msimu wa rushwa. Imefika mahali wagombea wanauza adi nyumba. Wengine wanaomba sana michango. Usipomchangia anakuwa mkali na kununua uso utadhani anakwenda kutibiwa,akiishazikusanya fedha anakwenda kuwanunua mawakala, nao wanawanunua wananchi. Wananchi mnachotakiwa kufanya ni kubomoa soko la kura".
6. "Napenda kuwafahamisha kwamba Hussein Bashe sio mkorofi bali ni miongoni mwa wabunge wa CCM wadadisi,kuna tofauti kubwa kati ya mdadisi na mkorofi,Bashe na Nape Nnauye ni miongoni mwa wanachama wetu wadadisi na wanasaidia kulichangamsha bunge ila wanatofautiana katika udadisi wao. Nape kidogo ana joto zaidi kuliko Bashe. Wote nawafahamu vizuri hivyo msidanganywe kuwa Nape na Bashe ni watukutu. Sio watukutu, ni wadadisi na wamewezesha mawaziri kufikiri kabla ya kutenda. Kutenda kila mmoja anawezakutenda, hata mwendawazimu anaweza kutenda lakini ili uweze kutenda kwa ufanisi na tija lazma ufikiri. Michango ya Bashe bungeni inafikirisha".
7. "Mimi ninachosisitiza ni nidhamu na si kunyamazisha watu. Tutapata wapi fikra mpya bila kuhojiana, bila kujadiliana na bila kudadisi? Tusipofanya hivyo, Chama Chetu cha Mapinduzi kitakuwa chama mfu".
8. "Nilikuwa Morogoro na akatajwa Waziri kuwa anamiliki hekari 1000. Watu wanatakakujua amezipataje na mi ntamwita waziri huyo nimuulize kusudi nikawajibu walioniuliza. Hatuwezi kuwa na viongozi ndani ya chama kinachojitambulisha kama chama cha wanyonge halafu baadhi yetu tunapora ardhi ya wanyonge. Ni suala la kuchagua kati ya kuwa Kiongozi wa CCM au kuwa Mporaji wa ardhi".
9. "Na hii habari ya "Dar Es Salaam ya Makonda" sio sahihi. Hakuna "Dar es Salaam ya Makonda" ni "Dar we Salaam chini ya Mkuu wa mkoa wa Dar Es Salaam, Makonda". Kuna wakati huwa namsikia Makonda akasema "Wananchi wangu", nani kamwambia ana wananchi wake? Hakuna wananchi wako,hakuna kiongozi anamiliki wananchi, ni "wananchi wenzangu". Mwalimu Nyerere aliwahi kuonya juu ya ubinafsi .."mkianza kusema- mimi, wewe, sisi au wao hamfiki". Vongozi vijana mnapaswa kuwa wanyenyekevu na kuacha papara. Vinginevyo mtapotea kama walivyopotea viongozi wengine vijana waliopewa madaraka wakakosa unyenyekevu" .
10. "Nawashukuru sana watanzania. Nawashukuru watanzania kwa kunisomesha kwa kodi zao na hatimaye nikaweza kupata shahada zote tatu, kamwe sitawasahau watanzania,nina deni kubwa la kulipa utumishi uliotukuka. Kazi niliyopewa ya kuwa Mtendaji Mkuu katika chama ni kubwa mno".
Kwa hakika, nukuu hizi kuntu zinamtanabaisha Mh Daktari Bashiru alikuwa ni mwanadamu wa aina gani,na alidhamiria kuifanya CCM iwe chama cha aina gani,"Nitasema kweli daima fitna kwangu mwiko" tulifundishwa hivyo na Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.
-Hofu yenu iko hapa.
Mnasema huenda he is ready for the worse !! Come what may ! Che guevara alisema “ its better to die standing than to live kneeling “. !!
Shida nyingine ndani ya chama,Vigogo ndani ya chama wanajua kabla haujaanzisha vita na kamati kuu ya chama,hakikisha kwanza una back-up ya kutosha kupitia wenyeviti wa mikoa na wilaya,ukiisha kusanya hiyo support ndio twende sasa na ‘twanga, nikutwange’ mpaka ndani ya vikao vya ndani,mifano ni minyukano ya Chama tola ile dhana ya kuvua gamba hadi uchaguzi wa 2015.
Niseme tu kama mwanazuoni,maneno ya Daktari Bashiru ni Phd in delivery,Daktari Bashiru ni freemind, hategemei hisani kama ninyi, ndio maana pamoja na kupewa ukatibu mkuu wa CCM na Rais Magufuli ila bado alikuwa anaongea maneno yenye ukakasi mno dhidi ya CCM na Rais Magufuli aliyachukua hayo kama feedback na kuyatafutia solution.
Nikiishia hapa,Mimi ni
Msemakweli Chakubanga,
Dar es Salaam.
0755078854.
-Bachelor of Business Administration in International Business
-Master of Leadership and Management.
Recent Publication;-
-Assessment on the effects of Micro-Financing on Poverty Reduction.