Ufugaji wa Kuku wa Kisasa: Fahamu Mbinu, Faida, Changamoto na Masoko

Nina maswali kadhaa kuhusu utotoleshaji wa viifaranga wa kienyeji/CHOTARA

1. Kama una incubator yenye capacity ya mayai 1000 unahitaji kuku wangapi as parent stock ili kuendesha hiyo incubator bila shids?
2. Napataje parent stock.?
3. Kwa nini kuku chotara sometimes wanatoa vifaranga vidhaifu sana na wasiokua?

Natanguliza shukrani zangu
 
Nina maswali kadhaa kuhusu utotoleshaji wa viifaranga wa kienyeji/CHOTARA
1. Kama una incubator yenye capacity ya mayai 1000 unahitaji kuku wangapi as parent stock ili kuendesha hiyo incubator bila shids?
2. Napataje parent stock.?
3. Kwa nini kuku chotara sometimes wanatoa vifaranga vidhaifu sana na wasiokua?
Natanguliza shukrani zangu

htuc, Kimsingi ukiwa na Incubator moja yenye uwezo wa kuchukua mayai 1000, huwezi kuweka mayai yote 1000 kwa wakati mmoja kwani ukifanya hivyo ina maana kuna mayai mengine utapoteza kwa kusubiri wiki tatu ili mayai uliyoweka yotorewe kwanza kisha uweke mengine.Incubator yenye uwezo wa kuchukua mayai 1000, utatakiwa ugawanye idadi hiyo ya mayai kwa tatu ili upate mayai utakayokuwa unayaweka kila wiki. Ukigawanya utapata mayai 333 ambayo kila wiki utapaswa kuyaingiza kwenye Incubator yako.Utaweka siku ya kwanza mayai 333, yatakopofika siku ya saba unayashusha chini,unaweka mengine yanakuwa na siku 1 na haya siku 1 yakifikia siku 7 na ya yale ya siku 7 yankuwa na siku 14. Siku ya 19 unayashusha kwenye kitotoleo (hatcher).

Hivyo ukiwa na machine ya kutotoa mayai 1000, utatakiwa uwe na parent stock 100,na kwa kuwa ni parest stock aina ya chotara utakagaji wake si mkubwa sana kama parent stock wa kuku pure wa mayai. Hao kuku 100 kila siku utaokota mayai 50 na mayai 50 ukizidisha kwa 7 utapata mayai 350 kati ya hayo, mayai 333 ndiyo utakayoingiza kwenye incubator.

Parent stock wa chotara wanatengenezwa kwa kuchukua kuku pure wa kienyeji(majike) ukipata kuchi wa Singida au Tabora ni wazuri zaidi then unacross na majogoo pure wa kisasa breed ya MAYAI mfano Rhode Ireland red(RID) au Barred polmouth rock. Ile cross ya kwanza ndio utakayoifanya parent wako na utawawekea tena majoo ya kisasa ili kuboresha kosaafu yao ili waweze kutaga zaidi.Kama utahitaji waliocrosiwa kabisa tuwasiliane.

Kupata vifaranga dhaifu kunasababishwa na mambo mengi sana. Mfano, mayai yakiwa madogo chini ya gram 45, kuweka mayai kwenye machine bila kuyatibu,joto kuwa dogo kwenye Incubator nk.
 
htuc,Kimsingi ukiwa na Incubator moja yenye uwezo wa kuchukua mayai 1000,huwezi kuweka mayai yote 1000 kwa wakati mmoja kwani ukifanya hivyo ina maana kuna mayai mengine utapoteza kwa kusubiri wiki tatu ili mayai uliyoweka yotorewe kwanza kisha uweke mengine.Incubator yenye uwezo wa kuchukua mayai 1000,utatakiwa ugawanye idadi hiyo ya mayai kwa tatu ili upate mayai utakayokuwa unayaweka kila wiki.Ukigawanya utapata mayai 333 ambayo kila wiki utapaswa kuyaingiza kwenye Incubator yako.Utaweka siku ya kwanza mayai 333,yatakopofika siku ya saba unayashusha chini,unaweka mengine yanakuwa na siku 1 na haya siku 1 yakifikia siku 7 na ya yale ya siku 7 yankuwa na siku 14.Siku ya 19 unayashusha kwenye kitotoreo(hatcher).

Hivyo ukiwa na machine ya kutotoa mayai 1000,utatakiwa uwe na parent stock 100,na kwa kuwa ni parest stock aina ya chotara utakagaji wake si mkubwa sana kama parent stock wa kuku pure wa mayai.Hao kuku 100 kila siku utaokota mayai 50 na mayai 50 ukizidisha kwa 7 utapata mayai 350,kati ya hayo, mayai 333 ndiyo utakayoingiza kwenye incubator.

Parent stock wa chotara wanatengenezwa kwa kuchukua kuku pure wa kienyeji(majike) ukipata kuchi wa Singida au Tabora ni wazuri zaidi then unacross na majogoo pure wa kisasa breed ya MAYAI mfano Rhode Ireland red(RID) au Barred polmouth rock.Ile cross ya kwanza ndio utakayoifanya parent wako na utawawekea tena majoo ya kisasa ili kuboresha kosaafu yao ili waweze kutaga zaidi.Kama utahitaji waliocrosiwa kabisa tuwasiliane.

Kupata vifaranga dhaifu kunasababishwa na mambo mengi sana.Mfano,mayai yakiwa madogo chini ya gram 45,kuweka mayai kwenye machine bila kuyatibu,joto kuwa dogo kwenye Incubator nk.

Vp Kuhusu uwezo wa utagaji wa cross breed ukilinganisha na pure breed?
 
htuc,Kimsingi ukiwa na Incubator moja yenye uwezo wa kuchukua mayai 1000,huwezi kuweka mayai yote 1000 kwa wakati mmoja kwani ukifanya hivyo ina maana kuna mayai mengine utapoteza kwa kusubiri wiki tatu ili mayai uliyoweka yotorewe kwanza kisha uweke mengine.Incubator yenye uwezo wa kuchukua mayai 1000,utatakiwa ugawanye idadi hiyo ya mayai kwa tatu ili upate mayai utakayokuwa unayaweka kila wiki.Ukigawanya utapata mayai 333 ambayo kila wiki utapaswa kuyaingiza kwenye Incubator yako.Utaweka siku ya kwanza mayai 333,yatakopofika siku ya saba unayashusha chini,unaweka mengine yanakuwa na siku 1 na haya siku 1 yakifikia siku 7 na ya yale ya siku 7 yankuwa na siku 14.Siku ya 19 unayashusha kwenye kitotoreo(hatcher).

Hivyo ukiwa na machine ya kutotoa mayai 1000,utatakiwa uwe na parent stock 100,na kwa kuwa ni parest stock aina ya chotara utakagaji wake si mkubwa sana kama parent stock wa kuku pure wa mayai.Hao kuku 100 kila siku utaokota mayai 50 na mayai 50 ukizidisha kwa 7 utapata mayai 350,kati ya hayo, mayai 333 ndiyo utakayoingiza kwenye incubator.

Parent stock wa chotara wanatengenezwa kwa kuchukua kuku pure wa kienyeji(majike) ukipata kuchi wa Singida au Tabora ni wazuri zaidi then unacross na majogoo pure wa kisasa breed ya MAYAI mfano Rhode Ireland red(RID) au Barred polmouth rock.Ile cross ya kwanza ndio utakayoifanya parent wako na utawawekea tena majoo ya kisasa ili kuboresha kosaafu yao ili waweze kutaga zaidi.Kama utahitaji waliocrosiwa kabisa tuwasiliane.

Kupata vifaranga dhaifu kunasababishwa na mambo mengi sana.Mfano,mayai yakiwa madogo chini ya gram 45,kuweka mayai kwenye machine bila kuyatibu,joto kuwa dogo kwenye Incubator nk.

Mayai yanatibiwa vipi? na njia zipi hutumika kuyatibu kabla ya kuyaweka kwenye Mashine?
 
Mayai yanatibiwa vipi? na njia zipi hutumika kuyatibu kabla ya kuyaweka kwenye Mashine?

Mayai kabla hayajaingizwa kwenye incubator yanatakiwa kwanza yatibiwe kwa kutumia Potassium permanganate pamoja formaldehyde 40%.Utibuji wa mayai kabla ya kuingizwa kwenye Incubator husaidia kuua wadudu waingiao kwenye kiini cha yai na kukiharibu toka yai litagwe.Pia huzuia magonjwa ya uambukizo toka kwa mama kwenda kwa kifaranga.

Husaidia pia kuwafanya vifaranga waliozaliwa kuwa strong. Na pia utibuji wa mayai unaongeza hatch ability. Kwa prossess za utibuji tunaweza kuwasiliana kama unajihususha na shughuli za utotoreshaji.
 
Mkuu vipi kuhusu Dawa? ni dawa zipi ni muhimu mtu kuwa nazo kama za huduma ya kwanza ukiachilia zile za Chanjo? Na vipi zile za Chanjo kuna mbadala wa zile za kuwekwa kwenye Fridge?

Na mwisho ukisoma machapisho mbalimbali kuna kukinzana kuhusu njia za kutumia wakati wa kuchanja hao kuku, Mfano unaweza kuta dawa ya ugonjwa mmoja tu ina Maelezo tofauti tofauti ya jinsi ya kuwapa dawa, wapo wana dai inatakiwa wawekewa machoni, wengine kwenye mabawa na wengine kwenye maji hiyo ni chanjo ya Ugonjwa mmoja tu
 
Mkuu vipi kuhusu Dawa? Ni dawa zipi ni muhimu mtu kuwa nazo kama za huduma ya kwanza ukiachilia zile za Chanjo? Na vipi zile za Chanjo kuna mbadala wa zile za kuwekwa kwenye Fridge?

Na mwisho ukisoma machapisho Mbalimbali kuna kukinzana kuhusu njia za kutumia wakati wa kuchanja hao kuku, Mfano unaweza kuta Dawa ya Ugonjwa mmoja tu ina Maelezo tofauti tofauti ya Jinsi ya Kuwapa dawa, Wapo wana dai inatakiwa wawekewa Machoni, wengine kwenye Mabawa na wengine kwenye Maji hiyo ni chanjo ya Ugonjwa mmoja tu

Asante chasha kwa maswali yako mazuri.Mfugaji wa kuku anatakiwa awe na dawa zifuatazo kama huduma ya kwanza;kwa vifaranga vitalyte/amin'total/au antistress pamoja na trisulmysine/trimazine 30%.Ukichanganya dawa mojawapo ya vitamini mf.vitalyte na dawa mojawapo ya sulfa mf. trisulmysine au trimazin 30% zitakusaidia kupunguza vifo kwani dawa hizi ukitumia kuanzia siku ya 2-6 inazuia na kutibu ugonjwa wa matumbo kwa vifaranga (ugonjwa wa pullorum) na pia ukaja kurudia siku ya 16-20 husaidia kuzua ugonjwa wa kuhara damu(coccidiosis).Magonjwa haya mawili huua sana vifaranga.

Muda hakuna but kwa kifupi tu dalili kubwa ya ugonjwa pullorum ni kushusha mabawa,mharo mweupe kama chokaa na wakati mwingine kinakuwa kama rangi ya udongo.Pia kifaranga anaonekana kama mwenye baridi,hawezi kumove mpaka umsukume, anasinzia,anakalia miguu yake. Vifo vingi kwa vifaranga.

Na ugonjwa wa kuhara damu dalili yake kubwa ni kuwa kifaranga huonekana kama amevaa koti,wakati mwingine kifaranga huarisha damu.Dalili zingine ni kama ugonjwa wa pullorum.
Dawa zingine zinazotakiwa ni Otetracycline 20%,Coridix,tylosine 75%.nk.

Kuhusu chanjo,hakuna mbadala ambazo haziwekwi kwenye friji.Chanjo zote lazima zihifadhiwe kwenye friji,vinginevyo zinaharibika.

Njia ya utoaji chanjo.

Kwa mfano ugonjwa wa mdondo/kideri una njia mbili za utoaji chanjo yake,ni kwa kuwadondoshea tone la dawa jichoni au kuwawekea wenye kwenye maji.Ugonjwa wa ndui(fowl pox) wenye huchanjwa kwa kuwachoma sindano kwenye mabawa.Wakati Gumboro huchanjwa kama kama wanavyochanjwa mdondo.Ni muhimu kufuata maelekezo ya dawa kutoka kwa mtengenezaji.Chanjo ya sindano huwezi kuitoa kwenye maji na kuwapa kuku wanywe,sawasawa na dawa ya matone kunya kwenye maji huwezi kuichanganya kwaenye maji.
 
Ndugu wana jamii forum,ifike wakati tuache kulalamika, tujitume kwa bidii kufanya kazi kwani kazi ndio msingi wa maisha yetu.Vijana graduates kutoka vyuo mbalimbali tuwaze zaidi kwenye kujiajiri kuliko kuajiriwa,kuajilikiwa ni utumwa pia ni hasara kama utapiga vizuri hesabu zako.Kwa wastaafu pia wana fursa ya kutumia mafao yao vyema kwenye miradi ya ufugaji.

Kwa kuanzia tu naruhusu kuulizwa maswali kutoka kwa wale wote wanaojihusisha na ufugaji wa kuku, kama kuna jambo lolote linasumbua na kutaka kupata ufafanuzi .Pia kwa wanaohitaji kuanzisha mradi wa ufugaji wa kuku,utotoreshaji wa vifaranga,biashara ya uchanganyaji na uuzaji wa vyakula vya kuku nk ,kama watanzania tunaweza kusaidiana ili hatimae tuondokane na umasikini.Kila mtu awe msaada kwa watu wengine kwa fani aliyesomea.

Karibuni kwa mjadala.
Mheshimiwa Kichwa mbovu, nataka nijikite kwenye uzalishaji wa vifaranga wa kuku wa kienyeji! Ni wapi naweza pata mashine ya uhakika ya kutotolesha mayai yenye kutumia mafuta ya taa? Maana za umeme sizitaki umeme hauaminiki tena. Uwezo wa juu kwa mashine hizo zinazotumia mafuta ya taa zinazopatikana Tanzania ni mayai mangapi? Unaweza kunidokeza juu ya bei zake na ubora wake! Nikiipata nitanunua nitotoreshe vifaranga nawalisha kwa mwezi mmoja nawauza! Najua italipa tu. Natanguliza shukrani zangu.

Kuhusu kujadili hakuna la kujadili hapa mada yako iko bayana kabisa kwamba kujiajiri ndiyo jibu la kujiweka huru kifedha, huko kwenye kazi za mishahara ya kupimiwa acha wakae walioridhika, tutawaajiri ukifika wakati maana wao wanaogopa risk! Wewe tumwagie maarifa tu hapa sisi tuanze kidogo kidogo tutaendelea kupeana updates mbele kwa mbele!
 
Mheshimiwa Kichwa mbovu, nataka nijikite kwenye uzalishaji wa vifaranga wa kuku wa kienyeji! Ni wapi naweza pata mashine ya uhakika ya kutotolesha mayai yenye kutumia mafuta ya taa? Maana za umeme sizitaki umeme hauaminiki tena. Uwezo wa juu kwa mashine hizo zinazotumia mafuta ya taa zinazopatikana Tanzania ni mayai mangapi? Unaweza kunidokeza juu ya bei zake na ubora wake! Nikiipata nitanunua nitotoreshe vifaranga nawalisha kwa mwezi mmoja nawauza! Najua italipa tu. Natanguliza shukrani zangu.

Kuhusu kujadili hakuna la kujadili hapa mada yako iko bayana kabisa kwamba kujiajiri ndiyo jibu la kujiweka huru kifedha, huko kwenye kazi za mishahara ya kupimiwa acha wakae walioridhika, tutawaajiri ukifika wakati maana wao wanaogopa risk! Wewe tumwagie maarifa tu hapa sisi tuanze kidogo kidogo tutaendelea kupeana updates mbele kwa mbele!

Mkuu hizi mashine za kutumia Mafuta ya Taa ni pasua kichwa unaweza ukafa kwa presha, Tatizo ni kwamba watengenezaji wa hizo mashine hawajawekeza vya kutosha kwenye utafiti wao wako bise na pesa tu, Bado za Umeme ndo solution ingawa China unaweza pata za kutumia Umeme na Gesi yaani inaweza endeshwa kwa gesi endapo umeme haupo na vilevile zipo za kuweza kutunza moto kwa masaa zaidi ya 9.
 
Mheshimiwa Kichwa mbovu, nataka nijikite kwenye uzalishaji wa vifaranga wa kuku wa kienyeji! Ni wapi naweza pata mashine ya uhakika ya kutotolesha mayai yenye kutumia mafuta ya taa? Maana za umeme sizitaki umeme hauaminiki tena. Uwezo wa juu kwa mashine hizo zinazotumia mafuta ya taa zinazopatikana Tanzania ni mayai mangapi? Unaweza kunidokeza juu ya bei zake na ubora wake! Nikiipata nitanunua nitotoreshe vifaranga nawalisha kwa mwezi mmoja nawauza! Najua italipa tu. Natanguliza shukrani zangu.
Alichosema chasha ni sahihi kabisa,mashine zinazotengenezwa hapa nchini ni usanii tupu,watengenezaji hawako serious na kazi.Kuzinunua ni kutupa pesa tu pasi na sababu yoyote ya maana.Hata hizi zinazotumia umeme bado ufanisi wake ni mdogo sana kiasi kwamba haziwezi kukupa faida.Kama uko serious na kazi pata machine kutoka nje ya nchi,mfano China au Italy huko utapata za uhakika.Kisha nunua generator kwa ajili ya emergence hapo utatengeze pesa,haitakiwi kufanya biashara kwa kubahatisha.
 
Mkuu hakuna njia yoyote ya kuifadhi hizo dawa zaidi ya kuweka kwenye friji?Hasa kwa wale ambao wanaishi vijijini au mbali na miundo mbinu ya umeme.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom