Resilience
JF-Expert Member
- Jan 4, 2023
- 876
- 4,101
Hawa wanawake na wanaume wanaodai kuchangia 120M wametumia posho na fedha za serikali ambazo ni kodi za wananchi.
Wengi wametoka Dodoma na wanalipwa kwa kuwepo nje ya ofisi kikazi. Lakini wengi wao wana ndugu na jamaa wenye kukosa mahitaji muhimu. Wengine wana ndugu wasiomudu huduma za afya huku baadhi wakiwa wamedhulumu lengo waonekane wapo na viongozi wa serikali.
Kwanini tuwaze kumchukulia fomu leo 2024? Pamoja na matatizo yote tuliyonayo tumefanya kampeni kipaombele cha nchi miaka miwili kabla? Tutatumia kiasi gani cha kodi za umma hadi tufike wakati wa uchaguzi?
Hofu hii imetoka wapi? Mbona mapema sana kuanza kampeni? Mbona Marais waliotangulia walikuwa na subira? Kwanini tunataka kumfanya Rais aone kama kuna shida ya kukubalika? Nashauri tupunguze haya mambo yanakwaza wapiga kura kuliko kuwapendeza.....yanakwaza kwa sababu ni sura zile zile zinajigeuza katika majukwaa mbalimbali kwa majina tofauti.....
Wengi wametoka Dodoma na wanalipwa kwa kuwepo nje ya ofisi kikazi. Lakini wengi wao wana ndugu na jamaa wenye kukosa mahitaji muhimu. Wengine wana ndugu wasiomudu huduma za afya huku baadhi wakiwa wamedhulumu lengo waonekane wapo na viongozi wa serikali.
Kwanini tuwaze kumchukulia fomu leo 2024? Pamoja na matatizo yote tuliyonayo tumefanya kampeni kipaombele cha nchi miaka miwili kabla? Tutatumia kiasi gani cha kodi za umma hadi tufike wakati wa uchaguzi?
Hofu hii imetoka wapi? Mbona mapema sana kuanza kampeni? Mbona Marais waliotangulia walikuwa na subira? Kwanini tunataka kumfanya Rais aone kama kuna shida ya kukubalika? Nashauri tupunguze haya mambo yanakwaza wapiga kura kuliko kuwapendeza.....yanakwaza kwa sababu ni sura zile zile zinajigeuza katika majukwaa mbalimbali kwa majina tofauti.....