Kwa njia za kawaida, uwezo huo hauna. Ila kiheshima, eti unao….

..mtoa mada anadai aliyepewa ndio feki, hana uwezo wa kupata PhD kwa kuisomea.

..je, wewe unaamini Maza ana uwezo wa kielimu na kitaalum kupata PhD?

..Maza amewahi kuandika makala yoyote ktk maarifa ya kitaalam?

..Maza amewahi kuandika kitabu chochote kudhihirisha usomi wake?

..Maza amewahi kualikwa popote na wasomi kutoa mhadhara na kuulizwa maswali kutokana na mada aliyowasilisha?
Mkuu kwanza tukubaliane kuwa Rais Samia ametunukiwa PhD ya udaktari wa heshima sio wa kusomea.

Walio mtunuku waliamua wenyewe, kwa hiyari yao na kwa vigezo vyao kumpa kwa sababu ya heshima yao kwake, sio kwa sababu ya uwezo wake wa kusoma, hapana.

Pili, nilitaka kuweka kumbukumbu sawa kwa sababu ndugu Goodluck5 alipotosha kuwa ile PhD aliyopewa Rais Samia ni feki/mchongo.

Tatu, Rais Samia ametunukiwa heshima hiyo na watalaamu wa nchi ya nje bila Rais Samia kuwalazimisha.

Ninaami wao kwa utalaamu wao wameona jambo adhimu kwa Rais Samia kiasi cha kustahili hiyo heshima!

Kama mashaka ni uwezo basi wakutiliwa mashaka kuhusu uwezo ni hao maprofesa kwa kumpa heshima ambayo wengi wetu tu naona hakustahili.

Kimsingi kama tunafikira hasi namna hii juu uwezo Rais na kiongozi wetu, basi tujue yeye ni true reflection ya jinsi tulivyo! Maana hajashuka kutoka mbinguni!

Nne, kuhusu kuandika Makala au kitabu, ni mapema mno kusema hata weza kuandika. Kwa maoni yangu, jinsi ambavyo ameweza kuongoza nchi kwa utulivu akiwa mwanamke amedhihirisha uwezo wake kiasi cha a
Kustahili heshima hiyo!

Ukweli usio na shaka ni kuwa ameingia madarakani katika mazingira magumu, hatari na ya pekee. Kaingia baada ya Rais kufa akiwa madarakani, umbi la uchaguzi mkuu halijatulia na bado korona ikiwepo.

Pamoja na hayo amepambana mno hadi nchi sasa ni tulivu, uchumi unatengamaa na kuinukia vizuri, uhuru na demokrasia ya wananchi imetamalaki ilihali uwekezaji umeongezeka miongoni mwa machache

Mkuu waswahili husema, mnyonge, mnyonge ila haki yake mpenzi.
 
Naona kama vile kuna watu hapa nchini waonao mtu kupewa ule udaktari wa heshima ni sawa na ule wa kuusomea.

Ukweli ni kwamba, si sawa hata kidogo.

Juzi hapa Rais wenu kapewa tena udaktari wa heshima huko India.

Tayari sasa katika utambulisho wake, watu wameshaanza kumwita eti Dr. Samia Suluhu Hassan.

Naye kwa kupenda ujiko, hata hagomi kuitwa hivyo.

Yupo tu anachekelea na kufurahia.

Now let’s face it. Katika hali ya kawaida, Samia hana uwezo wa kusoma na kufaulu mpaka kiwango cha PhD.

Kuna watu unaona kabisa huyu ana uwezo huo. Mfano Julius Nyerere au Benjamin Mkapa.

Hao ukiwasikiliza tu hata vile waongeavyo kuhusu mada mbali mbali, unauona kabisa uwezo wao.

Ni watu ambao wamewahi kuandika makala zilizochapishwa na magazeti na majarida mbali mbali duniani. Ni watu ambao wameshaahiriki kwenye mijadala mikubwa ya kimataifa na kutoa, kujenga, na kutetea hoja zao kwa umahiri mkubwa sana huku wakiwa na ‘command ya facts’ isiyo na mashaka.

Hao hata wakipewa udaktari wa heshima, mtu unaona kweli wanastahili maana hata wangeamua kupitia mkondo wa elimu, huo udaktari wangeupata tu.

Ila huyu tuliyenaye sasa, hana uwezo wa kupitia mkondo wa elimu na kuipata Phd.

Huo udaktari wake wa kupewa, unatokana na yeye kubahatika tu kuwa Rais.

Hana uwezo wa kuwa PhD wa ukweli…..
You nailed it
 
Nyerere aliwahi kuwa na PhD ya darasani?

Ilimchukuwa Nyerere miaka mingapi ya Urais kabla ya chuo kikuu chochote duniani kumpa "Honoris causa"?

Imemchukuwa mama Samia Suluhu Hassan chini ya miaka mitatu ya Urais kupata "honoris causa" ya Kimataifa.

"naona donge mie".
 
Ukiifatilia historia ya PhD, ilianzia kwenye zote kuwa ni za heshima, PhD baadae sana ndiyo zikaja kutolewa kwa "kusoma".

Zote msingi wake ni heshima, hakuna zaidi.

Nafahamu huu uzi lengo lake ni jaribio la "character assassination" lakini mleta mada anasahau kuwa kuna hata academically failures" wametunukiwa Honoris Causa.

Ma shaa Allah Mama Samia hana historia ya kufeli. Nanihii je?
 
Nyerere aliwahi kuwa na PhD ya darasani?

Ilimchukuwa Nyerere miaka mingapi ya Urais kabla ya chuo kikuu chochote duniani kumpa "Honoris causa"?

Imemchukuwa mama Samia Suluhu Hassan chini ya miaka mitatu ya Urais kupata "honoris causa" ya Kimataifa.

"naona donge mie".
Ulinganifu babaifu.
 
Mr. Ngabu,

hii ni dalili ya inferiority or seniority complex, ni conflict! Hivi Lula alikuwa mbeba mabox kama wewe, ulimsikia lini anaenda kutafuta degree ili aongoze nchi; typical Africa; kila kitu kudanganya danganya hamna viongozi wenye kujiamini. These are Banana republics; mie nashangaa sana kwa nini umejisumbua kuandika hayo yote!
Wahindi,waarabu na wachina... na hata wazungu ni wajanja sana. Wakisikia raia wa kiafrika anafanya ziara kwenye nchi zao huwa wanapelelezi weakness zake na kuzitumia kumfurahisha. Bila shaka wahindi wameshajua viongozi wa Tanzania wanapenda kusifiwa na kupewa degree za heshima hivyo wamaamua kutumia nafasi...
 
Ukiifatilia historia ya PhD, ilianzia kwenye zote kuwa ni za heshima, PhD baadae sana ndiyo zikaja kutolewa kwa "kusoma".

Zote msingi wake ni heshima, hakuna zaidi.

Nafahamu huu uzi lengo lake ni jaribio la "character assassination" lakini mleta mada anasahau kuwa kuna hata academically failures" wametunukiwa Honoris Causa.

Ma shaa Allah Mama Samia hana historia ya kufeli. Nanihii je?
Swadakta!
 
Nimenukuu
"
Tayari sasa katika utambulisho wake, watu wameshaanza kumwita eti Dr. Samia Suluhu Hassan.

Naye kwa kupenda ujiko, hata hagomi kuitwa hivyo.

Yupo tu anachekelea na kufurahia.

Now let’s face it. Katika hali ya kawaida, Samia hana uwezo wa kusoma na kufaulu mpaka kiwango cha PhD."





Mungu mtie nguvu Rais.
Form tu alishindwa kupata D 3 huko pHd si atapauona kama jahanam sasa
 
Naona kama vile kuna watu hapa nchini waonao mtu kupewa ule udaktari wa heshima ni sawa na ule wa kuusomea.

Ukweli ni kwamba, si sawa hata kidogo.

Juzi hapa Rais wenu kapewa tena udaktari wa heshima huko India.

Tayari sasa katika utambulisho wake, watu wameshaanza kumwita eti Dr. Samia Suluhu Hassan.

Naye kwa kupenda ujiko, hata hagomi kuitwa hivyo.

Yupo tu anachekelea na kufurahia.

Now let’s face it. Katika hali ya kawaida, Samia hana uwezo wa kusoma na kufaulu mpaka kiwango cha PhD.

Kuna watu unaona kabisa huyu ana uwezo huo. Mfano Julius Nyerere au Benjamin Mkapa.

Hao ukiwasikiliza tu hata vile waongeavyo kuhusu mada mbali mbali, unauona kabisa uwezo wao.

Ni watu ambao wamewahi kuandika makala zilizochapishwa na magazeti na majarida mbali mbali duniani. Ni watu ambao wameshaahiriki kwenye mijadala mikubwa ya kimataifa na kutoa, kujenga, na kutetea hoja zao kwa umahiri mkubwa sana huku wakiwa na ‘command ya facts’ isiyo na mashaka.

Hao hata wakipewa udaktari wa heshima, mtu unaona kweli wanastahili maana hata wangeamua kupitia mkondo wa elimu, huo udaktari wangeupata tu.

Ila huyu tuliyenaye sasa, hana uwezo wa kupitia mkondo wa elimu na kuipata Phd.

Huo udaktari wake wa kupewa, unatokana na yeye kubahatika tu kuwa Rais.

Hana uwezo wa kuwa PhD wa ukweli…..
Kabisa! Viongozi wanafuja mambo sana mfano Magufuli akiwa waziri alifanyiwa PhD na mhadhiri mmoja (jina nalihifadhi) pale chemistry department UDSM. Tulimwona Magufuli akija mara moja moja na kuonana na Dr huyo na kuondoka mda mfupi baadaye. Lab technicians walichakarika na baadaye kidogo tulisikia Magufuli ametunukiwa PhD ya chemistry!

Ben Saanane alipotezwa hadi leo hii kwa kuhoji uhalali wa hiyo PhD feki niliyoshuhudia mwenyewe! Okay

Magufuli alipokuwa rais yule mhadhiri alipewa cheo kuwa Katibu Mkuu wizara flani hadi leo!

Ukiwa kiongozi nchi hii utakuwa multibilionare, professor, generali, chifu na budget ya nchi nzima watasema umetoa wewe na utashukuriwa sana kwa miradi mbali mbali ya kitaifa kwa nyimbo na picha yako itabandikwa kwa lazima kila ofisi na katika mabango barabarani!
 
Dkt Joseph Kasheku alivyoshiriki kufutilia mbali Bandari ya DSM mikononi ya watanzania na kupewa DPw. Akiwa tayari anajiita Dkt Musukuma alienda Dubai na wenzake. Ni katika safari hiyo deal la DPw ilikamilika na yeye akawa mtetezi wa hao waarabu mwanzo mwisho.
Hadi hapo nguvu ya degrees za mtaani tumeshuhudia waziwazi
sasa ukishakuwa CCM lini unaruhusiwa kutumia akili? unatakiwa kutumia tu tumbo kufikiria. hayo mengine ya vyeti ukishakuwa CCM damu si jambo linalohitajika. hutakiwi kutumia akili kuwa ccm damu ama sivyo hautakuwa
 
Back
Top Bottom