Kwa nini mnichukie...!

Mtambuzi

Platinum Member
Oct 29, 2008
8,810
15,398
Old-African-Man-181829.jpg

Sisi binaadamu tunajipenda sana, katika kujipenda kwetu ndio maana tuko tayari kuwaona wengine wakiumia ili sisi tuone raha, yaani kuna watu wengine hufurahi sana kuwaona wengine wakiumia kihisia.

Kwa kujipenda kwake binadamu anataka aone kuwa yeye peke yake ndiye anafanikiwa maishani, yeye peke yake ndiye anayepata sifa na yeye peke yake ndiye anayepewa heshima. Ili hayo yatimie ni lazima binadamu wengine wawe chini yake, kwa maana kwamba wasifanikiwe, kwani kufanikiwa kwao kutakuwa na maana ya kumzidi yeye.

Wote tunajua maana ya chuki, ingawa kuna uwezekano mkubwa wengi wetu hatujui ni kwa kiasi gani chuki dhidi ya wengine hutuharibia maisha yetu na kutufanya kila siku kubaki katika hali duni tuliyomo.

Hebu jaribu na wewe kufanya utafiti mdogo. Ni mtu au watu gani ambao wewe unawafahamu vizuri kuwa wana chuki dhidi ya watu wengine?

Ninaposema chuki nina maana ya watu ambao wenzao wakipata wao hujisikia vibaya, wenzao wakifanikiwa wao huponda na kudharau mafanikio yao, wenzao wakijitahidi kupanda kimaendeleo wao huwashusha, wenzao wakisifiwa kwa jambo zuri wao hujitahidi kuwaharibia majina na tabia nyingine za namna hiyo.

Hebu waangalie watu hao ambao wana tabia kama hizo, halafu uangalie au upime kiwango cha maendeleo yao, unaweza ukapima pia aina ya maisha wanayoishi. Bila shaka utagundua kwamba kwa kiwango kikubwa ni watu ambao wana maisha duni siku zote na ni watu ambao maisha yao yanaonekana yamejaa nuksi na hawana furaha katika maisha.

Sisemi hata hivyo kwamba watu wote wasio na kitu wana chuki, au sisemi kuwa watu wote wenye uwezo hawana chuki, hapana. Kuna watu wenye chuki lakini ambao wana uwezo, ingawa uwezo huo kwa kawaida huzongwa na mikosi tele na kukosa amani ya nafsi.

Kuna watu wasio na kitu ambao hawana chuki hata asilani, lakini hawa maisha yao siku zote yamejaa matumaini na furaha ya kweli. Chuki kwenye maisha ina kazi moja tu, nayo ni kuhakikisha kwamba anayeifuga hata siku moja hapandi juu kimafanikio, na anaishi kwenye fadhaa, wasiwasi na kukosa furaha siku zote.

Chuki hupoteza muda wetu, hutuharibia mahusiano na watu, hutukosesha bahati na baraka, sasa kwa nini mtu usiamue kubadilika?

Ukianza kuondoa chuki moyoni au rohoni mwako ni wazi utaanza kujisikia mwepesi zaidi kimwili na kiakili na ninachoweza kukuhakikishia ni kwamba utaanza kuona mabadiliko kwenye shughuli na mambo yako.
 
No man is a true believer unless he desires for his brother that which he desires for himself.
Prophet Muhammad (pbuh)

:poa
 
shikamoo Mtambuzi!
yani unalosema ni maneno kuntu kuliko maelezo!
chuki huzidi kutudunisha na kuumiza miioyo yetu halafu la kuchekesha zaid utakuta mtu anamchuki mwingine huku yule mwingine hata hajui maskini kuwa anachukiwa na maisah yanasonga mbele!
CHUKI NICHUKIE ROHO YANGU NIACHIE!
 
Last edited by a moderator:
Siku za mwisho watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe,wenye chuki,wenye kupenda pesa etc
Haya yalisema na Yesu kabla hajafa

Sent from my BlackBerry 9860 using JnamiiForums
 
Asante kwa kunifungua macho Mtambuzi,, yaan nimepima juu ya mafanikio ya watu ambao wanachuki kali dhidi ya wengine na kiukweli hawana maendeleo hata kama huwa wanalipwa pesa nyingi,,
hii yote ni kutokana na kuwa pesa zao pia huwa hawafanyii mambo ya maendeleo ila hufanya show off ili wapate attention kwa wa2 wengine na waonekane wao ni bora zaidi,,
Asante kwa somo la Leo,,
 
True to the best of my knowledge, chuki hupelekea kuwa na vinyongo ambapo mwisho wa siku husababisha tupate magonjwa yawezayo kuzuilika.
 
Tunawahitaji sana watu wenye CHUKI zisizokuwa na msingi.Maana ndio wanaofanya wanaojitambua watumie vema vipawa vitatu vya AKILI,,UWEZO na UTASHI ili kusonga mbele.Katika Afrika watu hawa ndio bado kikwazo,ila nchi za wenzetu vikwazo ni mazingira,hali ya hewa n.k ILI tufike waliko wenzetu tunahitaji kundi kubwa la WALIOJITAMBUA ili wawapuuze WASIOJITAMBUA.
 
Chuki ni dhambi kuu ifikishayo motoni kwa waaminio Mungu, ila kwenye Satanic bible wanafundisha kitu tofauti, wana sema huwezi penda kila mtumaana ukifanya ivyo unakua umeloose power of selection
 
mtambuzi bana una akili sana wewe,yaani chuki huathiri hata siha ya mwili maana muda mwingi mtu huwa na jakamoyo na wengine ndipo wanapokuwa wachawi kabisa chuki ni giza la kujitakia.
 
Back
Top Bottom