BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,789
- 288,015
Ni bahati kupata Mke/Mume anayefaa.
Kwa kifupi na kwa maelezo rahisi naweza kusema kwamba wanaume wana advantage ya kuchagua wa kumuoa, mwanamke anasubiri kufuatwa na mwanaume ambaye anaona anamfaa kumuoa.Subira hiyo inaweza kuwa ya muda mfupi au mrefu.Wasichana wengine ni kweli wanachagua sana hadi umri unapitiliza na kufanya ushindani kuwa mkali zaidi katika " soko la wachumba".Wengine wanafikiria kujipanga vema kabla ya kuolewa - elimu au kiuchumi na wakati mwingine malengo haya huja kuwa kikwazo katika kupata mchumba mzuri!
Naam ni bahati kupata Mume. Unaweza kukuta msichana bomba sana katulia na labda madarasa yamepanda ya kutosha tu lakini wanaume wanapishana kila baada ya muda mfupi na huyo mwanadada kuendelea kubaki katika single's club kwa miaka kibao na hata kuanza kuingiwa na wasiwasi kuhusu biological clock yake. Wengine huanza kwenda hata kwa waganga kutumia miti shamba ili waongeze mvuto ili hatimaye wapate mume.
Ni kweli pia wengine wanakuwa wameweka requirements zao juu sana kiasi ambacho kumpata mtu ambaye anaweza kuzitimiza zote inakuwa ni kazi mno hivyo huishia kung'aa macho na wanapokuja kushtuka it is too late hivyo wanabaki solemba.