Satoh Hirosh
JF-Expert Member
- Mar 30, 2021
- 5,950
- 23,267
Nipo naperuzi Jf huku naubembeleza usingizi maana Jana nilikesha,nakutana na Uzi umeandikwa 'Soko la karume lateketea Kwa Moto lote'...Nikakumbuka nilichokishuhudia usiku wakati nipo mzigoni.
Ilikuwa mida ya saa Saba usiku nipo zang kazini,nimetoka nje kupata hewa kidogo,mara naona anga lote upande wa kariakoo limekuwa jekundu na limetanda Moshi mkubwa,wakati nashangaa na wenzangu nao wanatoka nje kuangalia nini kinaendelea upande wa kariakoo,mara tunasikia milio ya gari za faya,tukaendelea na kazi lkn kila tukitupa jicho upande ule unaowaka Moto hatuoni unafuu wowte wa Moto kupungua ingawa sauti za gari za faya tunazisikia.
Hadi kufika saa kumi alfajiri bado tunaona anga limetanda Moshi mkubwa,mpaka namaliza kazi naenda home kupumzika bado ule Moshi mzito umetanda angani.
Sasa hivi naingia Jf ndiyo najua kwamba ule Moto mkubwa uliokuwa unawaka na Sisi tukawa tunaushuhidia tukiwa bandarini kumbe ilikuwa ni soko la karume linateketea.Pole Sana Kwa waliounguliwa na Mali zao.
Lakini kuna maswali najiuliza baada ya hili tukio;
1.Muda soko linaungua ilikuwa ni usiku Sana,barabara nyingi zinakuwa hazina magari,Kwa nn faya wameshindwa kuuzima ule Moto kabla haujawa mkubwa na kuteketeza soko zima?
2.Zile kelele za magari ya faya tulizozikia muda mwingi zilikuwa na faida gani,maana pamoja na faya kuwa bize usiku kucha soko limeteketea,au hawakuwa na maji?
3.Kwa nini masoko yanateketea Sana,alafu mara zote huwa usiku?
4.Matukio ya Moto yanayotokea mara Kwa mara hupangwa au miundombinu huwa mibovu?
Pole zao 'wanyonge' waliounguliwa na Mali na hawana BIMA.
Ilikuwa mida ya saa Saba usiku nipo zang kazini,nimetoka nje kupata hewa kidogo,mara naona anga lote upande wa kariakoo limekuwa jekundu na limetanda Moshi mkubwa,wakati nashangaa na wenzangu nao wanatoka nje kuangalia nini kinaendelea upande wa kariakoo,mara tunasikia milio ya gari za faya,tukaendelea na kazi lkn kila tukitupa jicho upande ule unaowaka Moto hatuoni unafuu wowte wa Moto kupungua ingawa sauti za gari za faya tunazisikia.
Hadi kufika saa kumi alfajiri bado tunaona anga limetanda Moshi mkubwa,mpaka namaliza kazi naenda home kupumzika bado ule Moshi mzito umetanda angani.
Sasa hivi naingia Jf ndiyo najua kwamba ule Moto mkubwa uliokuwa unawaka na Sisi tukawa tunaushuhidia tukiwa bandarini kumbe ilikuwa ni soko la karume linateketea.Pole Sana Kwa waliounguliwa na Mali zao.
Lakini kuna maswali najiuliza baada ya hili tukio;
1.Muda soko linaungua ilikuwa ni usiku Sana,barabara nyingi zinakuwa hazina magari,Kwa nn faya wameshindwa kuuzima ule Moto kabla haujawa mkubwa na kuteketeza soko zima?
2.Zile kelele za magari ya faya tulizozikia muda mwingi zilikuwa na faida gani,maana pamoja na faya kuwa bize usiku kucha soko limeteketea,au hawakuwa na maji?
3.Kwa nini masoko yanateketea Sana,alafu mara zote huwa usiku?
4.Matukio ya Moto yanayotokea mara Kwa mara hupangwa au miundombinu huwa mibovu?
Pole zao 'wanyonge' waliounguliwa na Mali na hawana BIMA.