Msafiri Kasian
JF-Expert Member
- Sep 9, 2011
- 2,133
- 659
Jana kuna kitendo kilinishangaza Arusha,niliingia kwenye Zahanati ya Polisi pale Central(kwa wale wa Arusha wanafahamu mahali hapa) kwa sababu za kitabu tu.
Nilipoingia pale Zahanati,wahudumu walikuwa ni Polisi waliovalia sare nyeupe(kama traffic police vile) na dada mmoja aliyekuwa amevaa kiraia(t-shirt yake ya Yanga na suruali) ambaye ndiye aliyekuja kunihudumia baadae.
Katika ile sehemu ya kupumzkia wagonjwa huku wakisubiri huduma,kulikuwa na Polisi wengine wa kiume wanne waliokuwa wamevalia sare zao zile za khaki. Hawa walikuwa ni vijana kabisa wanatazama runinga kubwa iliyokuwepo mahali pale huku wakipiga stori.
Ilipofika mida ya saa 6 mchana,taarifa ya habari ITV ikamwonyesha Mbunge wa Arumeru Mashariki,Ndg. Joshua Nassari akiwa Iringa anahutubia hadhira ya watu.
Katika yake,Nassari alikemea kitendo cha yule mtuhumiwa wa mauji(sikumbuki alitaja mauaji ya nani) kutoroka mbele ya Polisi... Ndipo wale polisi nao wakaanza;
Wa kwanza "hawa nao hawana sera kabisa..."
wa pili "hawa kazi kuilalamikia polisi tu..."
mwingine nae akadakia,"hawa ingekuwa kipindi cha Mkapa na Mahita wangekoma...",hapa aliongea akimahanisha rais Kikwete hawezi kuwafanya kitu.
waliendelea na maneno mengine ya kejeli kwa CHADEMA kama vile,hawa wanapiga tu kelele majukwaani na mengine sikuyanukuu kichwani.
Sasa tujiulize,kwa majadiliano kama haya miongoni mwa polisi yanaashiria nini?
Mtazamo wangu: Hawa wakiambiwa,"nenda pale piga risasi wale...",watapiga tu na ndio maana mauaji ya raia wasio na hatia hayapungui,kwasababu polisi wanadhihirisha kutumika kisiasa.
Nilipoingia pale Zahanati,wahudumu walikuwa ni Polisi waliovalia sare nyeupe(kama traffic police vile) na dada mmoja aliyekuwa amevaa kiraia(t-shirt yake ya Yanga na suruali) ambaye ndiye aliyekuja kunihudumia baadae.
Katika ile sehemu ya kupumzkia wagonjwa huku wakisubiri huduma,kulikuwa na Polisi wengine wa kiume wanne waliokuwa wamevalia sare zao zile za khaki. Hawa walikuwa ni vijana kabisa wanatazama runinga kubwa iliyokuwepo mahali pale huku wakipiga stori.
Ilipofika mida ya saa 6 mchana,taarifa ya habari ITV ikamwonyesha Mbunge wa Arumeru Mashariki,Ndg. Joshua Nassari akiwa Iringa anahutubia hadhira ya watu.
Katika yake,Nassari alikemea kitendo cha yule mtuhumiwa wa mauji(sikumbuki alitaja mauaji ya nani) kutoroka mbele ya Polisi... Ndipo wale polisi nao wakaanza;
Wa kwanza "hawa nao hawana sera kabisa..."
wa pili "hawa kazi kuilalamikia polisi tu..."
mwingine nae akadakia,"hawa ingekuwa kipindi cha Mkapa na Mahita wangekoma...",hapa aliongea akimahanisha rais Kikwete hawezi kuwafanya kitu.
waliendelea na maneno mengine ya kejeli kwa CHADEMA kama vile,hawa wanapiga tu kelele majukwaani na mengine sikuyanukuu kichwani.
Sasa tujiulize,kwa majadiliano kama haya miongoni mwa polisi yanaashiria nini?
Mtazamo wangu: Hawa wakiambiwa,"nenda pale piga risasi wale...",watapiga tu na ndio maana mauaji ya raia wasio na hatia hayapungui,kwasababu polisi wanadhihirisha kutumika kisiasa.