Nimesikiliza hotuba ya Lissu leo Segerea, naona lissu ana improve safi sana, tatizo bado iko palepale japo limepungua kidogo katumia muda mwingi kumshambulia jpm kulipo kuelezea yeye na serikali yake watafanya nini, machache aliyo yaelezea nayo ni kama ifuatavyo.
1. Ujenzi wa barabara ya Salender Bridge; anashangaa hizo pesa nyingi hivyo zinatumika kwa ajili ya watu wachache, kwanza sio kweli kuwa salender bridge hutumiwa na matajiri na vip only, hiki ni kiungo cha kutokea mwenge mbezi ununio mbweni hadi bagamoyo, kusema ni pesa nyingi ni mawazo ya kimasikini tu
Sweden wanajenga barabara ya US$47B barabara ya chini ya maji leo sie kamchepuko tu mtu anaona aghali eti fedha zingetumika kuchimba mitaro vingunguti, naona huyu hakuwepo nchini muda mrefu sasa hivi vingunguti ni lami tupu sivyo alivyo acha.
2. Kuhusu country credit rating; Hivi ni vipimo vya unyonyaji vinavyotumiwa na wazungu kupima urahisi wa kunyonya, hatuwezi kujisifu eti sisi ni watu rahisi kunyonywa rasilimali zetu hapana hata yeye Lissu anajua ngosha hayuko hivyo, hizo FDI sio hela za shangazi zetu hawaji kuwekeza eti sisi ni masikini wanataka watuinue tuendelee kama wao hapana.
Sasa hivi chini ya JPM tunakaa tunazungumza biashara kama hailipi tunaachana nayo, kwa taarifa yako billionea tajiri wa kwanza duniani Jeff Bezos kanunua hisa Barrick za usd 686m na sehemu ya hizo pesa zitawekezwa Tanzania kupitia ubia wetu wa Twiga hayo aliyotumiwa kwenye whasap aka google apate ukweli
3. Kelele za uwanja wa chato; hivi jamani kuna tatizo gani kujenga ka uwanja ka kutua home, kwa taarifa yake hivi viwanja kanda ya ziwa viko vingi kipo Mugumu Serengeti Musoma Mwadui Ibadakuli Nyashimo mission GGM Bulyanhulu Buzwagi Tulawaka Rwamgasa, hiyo runway isimtishe Lissu, nimkumbushe uwanja wa kwanza kujengwa africa mashariki ulikuwa wa Williamson Diamond Mwadui na ndege ya kwanza kutua ilimleta mwana mfalme wa uingereza haya ni mambo ya kawaida sana yasimpe presha.
Na kwanini ujengwe chato? chato ni tambarare ukilinganisha na Geita Bukombe na Katoro ni Giographia tu ndiyo inaruhusu, isitoshe hiyo pesa angeweza kuitumia kuzurura ulaya kama kwenda WEF davos sullivan UN EU AU au hata kwenda kunywa chai na trump ka serve hela na sehemu ya hiyo hela kajijengea kakiwanja shida iko wapi? Kuna waziri mkuu aliwahi kusafiri na msafara wa watu 70 kwenda kwenye graduation ya mwanae marekani na huyuhuyu Lissu akiwa mbunge hakuhoji.
4. Kuhusu bei ya ndege huyu bwana anamatatizo gani? alishaenda atcl akauliza bei ya ndege akakosa jibu? alishaenda Boeng kuuliza bei ya ndege akanyimwa? anauliza bei ya ndege mbona haulizi bei ya nguzo za umeme? mbona haulizi bei ya Youtong za Shabiby? mbona haulizi bei ya mabehewa ya SGR? atcl ina management yake ina muundo na taratibu za uendeshaji tuiache ifanyekazi zake. kwahiyo anataka wabunge waanze kwenda boeng airbus beachcraft jumbojet kukusanya quotation?
5. Uhuru wa kuamua, kwahili bora angeanza kutuambia ruzuku ya chadema ya miaka mitano iko wapi, atuambie zile 500m kila mwezi wanazopokwa wabunge wa chadema ziko wapi? Kila mbunge wazamani analia hana hela za kampeni na juzi wamelipwa 200m kilamtu wamepeleka wapi? kama ni unyanganyi basi basi upo cdm.
6. Hili la NHIF mfumo anaotaka kuleta sio mgeni kule marekani alitaka kuuanzisha Obama ukapewa jina la "Obama care" kama wamarekani uliwashinda na Lissu ataufanikisha basi atakuwa mtu mwnye akili sana. na kwa taarifa yake Bima ya afya sio ya bure ni huduma unalipia kama unavyokata bima ya gari kuwa litakapopata ajali liweze kutengenezwa, unaposema kila mtu awe na bima maana yake kila mtu alipie matibabu kwa lazima uwe mzima mgonjwa lipa tu, ni sawa na mtu kumwambia kila mtu alipe bima ya gari uwe huna unalo lipa tu utajiju, hapana, wenye uwezo wacha walipe bima na ambao hawana uwezo wapate huduma bure.
7. Deni la Taifa, Lissu anasema tunajenga miradi kwa pesa zetu deni linatoka wapi? kwanza hawa contractors wanalipwa pesa ya kigeni sie tunakusanya pesa za kitanzania tunahitaji dola za kuwalipa hawa wakandarasi, pesa iko bank lakini yakitanzania na hawa Arab Contractors Yepi wanataka dola, lazima tukope na kukopa sio dhambi na zipo kanuni za kukopa. Ukioa kwa msomali anakuuliza kuna mtu anakudai ukisema hapana anakufukuza maana yake kuna siku mwanae atalala njaa kisa umeogopa kukopa.
1. Ujenzi wa barabara ya Salender Bridge; anashangaa hizo pesa nyingi hivyo zinatumika kwa ajili ya watu wachache, kwanza sio kweli kuwa salender bridge hutumiwa na matajiri na vip only, hiki ni kiungo cha kutokea mwenge mbezi ununio mbweni hadi bagamoyo, kusema ni pesa nyingi ni mawazo ya kimasikini tu
Sweden wanajenga barabara ya US$47B barabara ya chini ya maji leo sie kamchepuko tu mtu anaona aghali eti fedha zingetumika kuchimba mitaro vingunguti, naona huyu hakuwepo nchini muda mrefu sasa hivi vingunguti ni lami tupu sivyo alivyo acha.
2. Kuhusu country credit rating; Hivi ni vipimo vya unyonyaji vinavyotumiwa na wazungu kupima urahisi wa kunyonya, hatuwezi kujisifu eti sisi ni watu rahisi kunyonywa rasilimali zetu hapana hata yeye Lissu anajua ngosha hayuko hivyo, hizo FDI sio hela za shangazi zetu hawaji kuwekeza eti sisi ni masikini wanataka watuinue tuendelee kama wao hapana.
Sasa hivi chini ya JPM tunakaa tunazungumza biashara kama hailipi tunaachana nayo, kwa taarifa yako billionea tajiri wa kwanza duniani Jeff Bezos kanunua hisa Barrick za usd 686m na sehemu ya hizo pesa zitawekezwa Tanzania kupitia ubia wetu wa Twiga hayo aliyotumiwa kwenye whasap aka google apate ukweli
3. Kelele za uwanja wa chato; hivi jamani kuna tatizo gani kujenga ka uwanja ka kutua home, kwa taarifa yake hivi viwanja kanda ya ziwa viko vingi kipo Mugumu Serengeti Musoma Mwadui Ibadakuli Nyashimo mission GGM Bulyanhulu Buzwagi Tulawaka Rwamgasa, hiyo runway isimtishe Lissu, nimkumbushe uwanja wa kwanza kujengwa africa mashariki ulikuwa wa Williamson Diamond Mwadui na ndege ya kwanza kutua ilimleta mwana mfalme wa uingereza haya ni mambo ya kawaida sana yasimpe presha.
Na kwanini ujengwe chato? chato ni tambarare ukilinganisha na Geita Bukombe na Katoro ni Giographia tu ndiyo inaruhusu, isitoshe hiyo pesa angeweza kuitumia kuzurura ulaya kama kwenda WEF davos sullivan UN EU AU au hata kwenda kunywa chai na trump ka serve hela na sehemu ya hiyo hela kajijengea kakiwanja shida iko wapi? Kuna waziri mkuu aliwahi kusafiri na msafara wa watu 70 kwenda kwenye graduation ya mwanae marekani na huyuhuyu Lissu akiwa mbunge hakuhoji.
4. Kuhusu bei ya ndege huyu bwana anamatatizo gani? alishaenda atcl akauliza bei ya ndege akakosa jibu? alishaenda Boeng kuuliza bei ya ndege akanyimwa? anauliza bei ya ndege mbona haulizi bei ya nguzo za umeme? mbona haulizi bei ya Youtong za Shabiby? mbona haulizi bei ya mabehewa ya SGR? atcl ina management yake ina muundo na taratibu za uendeshaji tuiache ifanyekazi zake. kwahiyo anataka wabunge waanze kwenda boeng airbus beachcraft jumbojet kukusanya quotation?
5. Uhuru wa kuamua, kwahili bora angeanza kutuambia ruzuku ya chadema ya miaka mitano iko wapi, atuambie zile 500m kila mwezi wanazopokwa wabunge wa chadema ziko wapi? Kila mbunge wazamani analia hana hela za kampeni na juzi wamelipwa 200m kilamtu wamepeleka wapi? kama ni unyanganyi basi basi upo cdm.
6. Hili la NHIF mfumo anaotaka kuleta sio mgeni kule marekani alitaka kuuanzisha Obama ukapewa jina la "Obama care" kama wamarekani uliwashinda na Lissu ataufanikisha basi atakuwa mtu mwnye akili sana. na kwa taarifa yake Bima ya afya sio ya bure ni huduma unalipia kama unavyokata bima ya gari kuwa litakapopata ajali liweze kutengenezwa, unaposema kila mtu awe na bima maana yake kila mtu alipie matibabu kwa lazima uwe mzima mgonjwa lipa tu, ni sawa na mtu kumwambia kila mtu alipe bima ya gari uwe huna unalo lipa tu utajiju, hapana, wenye uwezo wacha walipe bima na ambao hawana uwezo wapate huduma bure.
7. Deni la Taifa, Lissu anasema tunajenga miradi kwa pesa zetu deni linatoka wapi? kwanza hawa contractors wanalipwa pesa ya kigeni sie tunakusanya pesa za kitanzania tunahitaji dola za kuwalipa hawa wakandarasi, pesa iko bank lakini yakitanzania na hawa Arab Contractors Yepi wanataka dola, lazima tukope na kukopa sio dhambi na zipo kanuni za kukopa. Ukioa kwa msomali anakuuliza kuna mtu anakudai ukisema hapana anakufukuza maana yake kuna siku mwanae atalala njaa kisa umeogopa kukopa.