Eddo Sambai
JF-Expert Member
- Aug 1, 2013
- 2,344
- 1,771
Ndugu watu wa Jf amani ya Bwana ikae nanyi.
Awali ya yote naomba ninukuu 1Samweli 15: 2 - 3 iwe ndio msingi wa mada yangu.
2 - Bwana wa majeshi asema hivi "Nimeyatia moyoni mwangu mambo hayo Amaleki waliyowatendea Israeli, jinsi walivyowapinga njiani, hapo walipopanda kutoka Misri."
3 - "Basi sasa nenda ukawapige Amaleki, Na kuviharibu kabisa vitu vyote walivyonavyo, wala msiwaachilie; bali waueni, mwanamume na mwanamke, mtoto naye anyonyaye, ng'ombe na Kondoo, Ngamia na Punda"
Baada ya nukuu hiyo ya mistari miwili kutoka kwenye Biblia takatifu ambacho ndicho kitabu cha imani cha Wakristo wote pamoja na Wayahudi, naomba niseme yafuatayo.
Moja ya kazi ambazo kanisa imepewa ni kuiombea Israeli na hii nI kwasababu Taifa la Israeli limebarikiwa na yeyote atakayeibariki/kuiombea Israeli basi naye atabarikiwa.
Sasa basi kutokana na matendo pamoja na mienendo inayofanywa na majirani wa Israeli (Arabic Countries) juu ya kuizuru Israeli, pia tukio la tarehe 05/10/2023 kitendo cha kundi la HAMASI kuivamia na kuishambulia na kuuwa makumi ya wana wa Israel.
Je, ni nani anayejua hasira ya Mungu wa Izrael imewaka kiasi gani?
Je, ni nani anayejua ni maelekezo yapi wana wa Israeli waliyopewa na Mungu kufanya dhidi ya maadui zake?
Hayo maswali mawili yananipelekea kusema "KANISA LIOMBE JUU YA ISRAELI"
Ukristo na Uyahudi wote kwapamoja huamini katika Mungu Mmoja. Tofauti yao ni kwamba Myahudi haamini katika Kristo wakati Wakristo huamini kuwa Kristo ndiye njia ya pekee ya kumwendea/kumwabudu Mungu muumba mbingu na nchi.
Israeli ilipewa Sheria (Torati) waitumie ili kuweza Kumwabudu na kumtumikia Mungu.
Kristo yeye ni Imani, Imani sio sheria na kila mwenye kumwamini Kristo basi huyo hana haja ya kufungwa na sheria.
Tuiombee ISRAELI.
Awali ya yote naomba ninukuu 1Samweli 15: 2 - 3 iwe ndio msingi wa mada yangu.
2 - Bwana wa majeshi asema hivi "Nimeyatia moyoni mwangu mambo hayo Amaleki waliyowatendea Israeli, jinsi walivyowapinga njiani, hapo walipopanda kutoka Misri."
3 - "Basi sasa nenda ukawapige Amaleki, Na kuviharibu kabisa vitu vyote walivyonavyo, wala msiwaachilie; bali waueni, mwanamume na mwanamke, mtoto naye anyonyaye, ng'ombe na Kondoo, Ngamia na Punda"
Baada ya nukuu hiyo ya mistari miwili kutoka kwenye Biblia takatifu ambacho ndicho kitabu cha imani cha Wakristo wote pamoja na Wayahudi, naomba niseme yafuatayo.
Moja ya kazi ambazo kanisa imepewa ni kuiombea Israeli na hii nI kwasababu Taifa la Israeli limebarikiwa na yeyote atakayeibariki/kuiombea Israeli basi naye atabarikiwa.
Sasa basi kutokana na matendo pamoja na mienendo inayofanywa na majirani wa Israeli (Arabic Countries) juu ya kuizuru Israeli, pia tukio la tarehe 05/10/2023 kitendo cha kundi la HAMASI kuivamia na kuishambulia na kuuwa makumi ya wana wa Israel.
Je, ni nani anayejua hasira ya Mungu wa Izrael imewaka kiasi gani?
Je, ni nani anayejua ni maelekezo yapi wana wa Israeli waliyopewa na Mungu kufanya dhidi ya maadui zake?
Hayo maswali mawili yananipelekea kusema "KANISA LIOMBE JUU YA ISRAELI"
Ukristo na Uyahudi wote kwapamoja huamini katika Mungu Mmoja. Tofauti yao ni kwamba Myahudi haamini katika Kristo wakati Wakristo huamini kuwa Kristo ndiye njia ya pekee ya kumwendea/kumwabudu Mungu muumba mbingu na nchi.
Israeli ilipewa Sheria (Torati) waitumie ili kuweza Kumwabudu na kumtumikia Mungu.
Kristo yeye ni Imani, Imani sio sheria na kila mwenye kumwamini Kristo basi huyo hana haja ya kufungwa na sheria.
Tuiombee ISRAELI.