Freedom tommorrow
JF-Expert Member
- Jan 31, 2015
- 1,795
- 1,130
Kwa jinsi Muheshimiwa Dr. JPM anavyokamua majipu kila kukicha, inaonekana wazi kabisa taifa hili limeangushwa watumishi wachache tuliowaamini na kuwalipa mishahara mizuri kwa lengo wasije pokea rushwa TRA ni moja wapo. Kama watumishi hawa wangekuwa na uchungu na nchi yetu basi leo Tanzania tusingekuwa Omba Omba.
Angalia Magogo yanavunwa TZ yanapitishiwa Zambia kwa documents feki za baadhi ya watumishi ambao si waaminifu kwa Taifa letu. Makontena yanapita bila kulipiwa ushuru na mengine yakuja.
Laiti kama wakusanya ushuru wangewakomalia matajiri nchi hii ingekuwa mbali sana. lakini si hivyo anakomaliwa mfanya biashara wa maduka ya kariakoo tena wengine kipato chao ni kidogo...inashangaza!
"chochote kilichosimama kwa dhulma, kitakatika" (Muhammad PBU)
Angalia Magogo yanavunwa TZ yanapitishiwa Zambia kwa documents feki za baadhi ya watumishi ambao si waaminifu kwa Taifa letu. Makontena yanapita bila kulipiwa ushuru na mengine yakuja.
Laiti kama wakusanya ushuru wangewakomalia matajiri nchi hii ingekuwa mbali sana. lakini si hivyo anakomaliwa mfanya biashara wa maduka ya kariakoo tena wengine kipato chao ni kidogo...inashangaza!
"chochote kilichosimama kwa dhulma, kitakatika" (Muhammad PBU)