Kuvunja soko la Kariakoo ni upumbavu kabisa...

masoko makubwa ya katikati ya majiji yapaswa kuwa ardhini na juu kunafanyika shughuli nyingine tofauti na barabara zinapita na majumba yanajengwa.

yaani karibu theluthi moja ya wakazi wa jiji watakuwa wanafanya shughuli zao chini ya ardhi............ na wakimaliza shughuli zao wanakutana na sub-way/metro, inawachukua chini kwa chini hadi huko kimara, sijui gongo la mboto nk na kuacha daladala juu ya ardhi zikiwa nyeupe 24/7 .............. na hii ingepunguza sana msongamano juu ya ardhi............. kama ni mawazo kama hayo, mi naunga mkono ujenzi huo mia kwa mia..............

Hilo balaa Mungu atuepushie huo muda bado haujafika mkuu.......kama magorofa tunayoyaona yanaanguka kwa ujenzi mbovu sembuse hayo mahandaki si itakuwa balaa
 
DUH ...ama kweli tumekosa ma"thinkers".....Hizi kelele wadau zinawafikia?
Ni Kweli kabisa. Hivi JF umekuwa ukumbi wa kuomboleza? Kulaumu na kutukana kutaleta mabadiliko gani? Kama kweli ni great thinkers kama tunavyojinadi tuje na practical solutions kwa mambo tunayoyaona hayafai. Kwa mfano kuanzisha petitions kwenye mtandao na mitaani kupinga wazo la kubomolewa soko la KARIAKOO TUKIJIWEKEA LENGO LA KUKUSANYA SAHIHI MILIONI MOJA. Baadaye hizo petitions ziwasilishwe Ikulu, au City Council, au Bungeni vyoyvyote vile itakavyoonekana inafaa. Kelele tena mtu uko kilometre elfu tano au zaidi hazisaidii kitu. Hutaki watawala wabovu lakini hujiandikishi kupiga kura, wapi na wapi.
 
ni kweli kabisa. Hivi jf umekuwa ukumbi wa kuomboleza? Kulaumu na kutukana kutaleta mabadiliko gani? Kama kweli ni great thinkers kama tunavyojinadi tuje na practical solutions kwa mambo tunayoyaona hayafai. Kwa mfano kuanzisha petitions kwenye mtandao na mitaani kupinga wazo la kubomolewa soko la kariakoo tukijiwekea lengo la kukusanya sahihi milioni moja. Baadaye hizo petitions ziwasilishwe ikulu, au city council, au bungeni vyoyvyote vile itakavyoonekana inafaa. Kelele tena mtu uko kilometre elfu tano au zaidi hazisaidii kitu. Hutaki watawala wabovu lakini hujiandikishi kupiga kura, wapi na wapi.


nafikiria kufanya hivyo kwa kweli...............
 
Ni jambo la kushangaza kwa sababu wengi wanaotumia soko la kariakoo sio wakazi wa kariakoo...kwa hiyo ni wazi kama watumiaji wanao ishi maeneo yaliyo mbali na kariakoo wakijengewa masoko huko waliko hawatakuwa na uhitaji wa kufunga safari kuja kujazana hapo kariakoo. Na hivyo tutakuwa tumetatua tatizo la msongamano na pia kulinda heshima ya majengo yetu ya ukumbusho.

Lakini swali linabaki,huyo alietoa 'mawazo mtindi' kama hayo ya kubomoa soko la kariakoo halifahamu hili wazo la kuwasogezea huduma wana nchi huko waliko ili kupunguza msongamano hapo sokoni kariakoo????

Au ndo ile wanatengeneza naman nyingine ya ulaji....tunakumbuka ni juzi juzi tu tuliambiwa bora tufe njaa lakini lazima ndege ya raisi na rada zinunuliwe, matokeo yake tumeyaona watu walipiga mamilioni ya hela wakatia mfukoni....nhi yetu bwana,kama kajishamba ka bibi!!

Huu ndo uozo mwingine kama Gogo hotel, lini tutaamka? Kwanza zile Machinga complex zinafanya nini mbona haitumiki? Waboreshe barabara zote zinazoenda Kkoo, wajenge masoko aidha Kawe, Ubungo Mbezi ya Morogoro rd au Tegeta kwa wakazi wa Kinondoni na maeneo mengine nje ya mji kwa ajili ya manispaa nyingine. Watu tumehamia suburban kukimbia msongamano bado mnataka hata weekend tupange foleni kufata nyanya Kkoo? Mbona hakuna mipango mji Dar ovyo sana.
 
Yaani its unbelievable kwamba kuna watu wanalipwa
mishahara hapa jijini na kazi yao ni mipango miji....
...........ukishangaa ya musa.........................
 
Back
Top Bottom