Kwanza nimpongeze Ex DC Kitwala kwa kupigania HAKI yako. Nitoe mfano unaofanana wa Ex DC Kitwala. Kuna rafiki yangu aliteuliwakuwa Mkuu wa Wilaya akiwa na miaka 32 na akadumu kwenye Ukuu wa Wilaya kwa muda wa miaka mitano. Awamu hiyo ilipoisha hakupata uteuzi akiwa na miaka 37 na kabla kuteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya alikuwa Afisa Mipango. Baada ya kukosa uteuzi akarudi nyumbani na hakurudia ile kazi yake ya Afisa Mipango. Watendewe haki isheria. Mtu umekosa uteuzi na hujafikisha miaka 60 ya kustaafu kisa kukosa uteuzi wa kuendelea kuwa Mkuu wa Wilaya unanyimwa kuendelea na wadhifa wako wa zamani. Ninaishauri Serikali, kama mtumishi amekosa uteuzi na alikuwa ni mtumishi wa Umma ni vema akaurudi kuendelea na kazi yake ya awali kabla ya kuwa Mkuu wa Wilaya. Nitamshauri huyu rafiki yangu Ex DC naye akimbilie kwenye vyombo vya haki ili naye apate haki yake.