Kuchasoni Kuchawangu
JF-Expert Member
- Aug 21, 2012
- 603
- 340
Wa JF Kumekuwa na mnyukano mkali sana katika ulingo wa siasa za CCM Wilaya Nzega,kati ya Hussein Bashe na mbuge wa sasa Hamisi Kigwangala.Wamekuwa wakishutumiana kwa wazi mpaka kutishiana maisha kwa bastora.Kitendo hiki kimewafanya wote kwa pamoja kutoswa kwenye kinyang'anyiro cha kugombea ujumbe wa Nec kupitia wilaya ya Nzega. Aliyekuwa mbunge wa zamani Lucas Selelii hasikiki ktk duru hizi za siasa za CCM Nzega.Ikizingatiwa kwenye kura za maoni alishika nafasi ya pili nyuma ya Bashe aliyekuwa wa kwanza na juu ya Kigwangala aliyeshika nafasi ya tatu. Je ugomvi wa Bashe na Kigwangala utamrudisha Selelii kwenye siasa za nzega tena? Maoni kwenu wadau.