Ugumu wangu
JF-Expert Member
- May 6, 2021
- 1,685
- 3,549
Member wa JamiiForums wote nawasalimu kwa jina la Yesu Kristo aliekufa msalabani kwa ajili ya uovu wangu.
Leo nimependa kushare kidogo kuhusu historia ya maisha yangu inaweza kuwa funzo kwa mwingine pia.
Mara baada ya kumaliza darasa la Saba katika shule moja ya msingi mkoa wa Singida dc nilibahatika kuchaguliwa kujiunga na shule ya sekondari ya wavulana Tabora school, kwa bahati mbaya nilizaliwa katika familia ambayo bado haikuwa inatambua umuhimu wa elimu pamoja na ilikuwa na uwezo wa kunisomesha lakini haikuwa hivyo.
Mimi ni mtoto wa mwisho Kati ya watoto Tisa kutoka kwa baba mmoja na Mama mmoja hivyo nilikuwa napendwa sana kama mtoto wa mwisho na ndugu zangu wengine wapatao wanne walifaulu vizuri kwenye shule nzuri ambazo leo zinaitwa special school lakini wazazi waligoma kabisa kuwasomesha wakiwa na Imani wataenda kupotea, hivyo nami nikaunganishwa kwenye kundi hilo kuwa nitaenda kupotea na hivi ikizingatiwa Mimi ni mtoto wa mwisho na wazee wananipenda sana.
Baada ya kuomba ushauri kwa kaka zangu nao pia waligoma kabisa kunipa ushauri wowote na zaidi ya kuniambia kaa nyumbani wewe ndio utawalea wazazi na kuwatunza, nahisi kwa wale mliokulia Singida mnajua vizuri mtoto wa mwisho ndio mwenye jukumu la kubaki na wazazi kwa kipindi hicho,
Basi baada ya majibu hayo moyoni mwangu palikuwa na wingu zito la mawazo huku nikishuhudia wale tuliosoma wakiwa kwenye haraki za kujiandaa kuripoti shuleni na hasa marafiki tuliokuwa karibu sana na wengine walikuwa wa shule jirani na tulikuwa tukifanya mitihani ya ujirani mwema na kushindana kwa nguvu kubwa, pamoja na yote hayo sikuwa na njia nyingine ya kufanya.
Kuna siku nikiwa nachunga nikajiwa na wazo kwanini nisitafute shule za mashirika ya kidini niende kujieleza naweza pia kupata msaada wa kusomeshwa na ndugu wakiona juhudi zangu wanaweza kuamua kuanza kunipa msaada,
baada ya kupata wazo Hilo huku siku mbili nyuma nilisikia story kuhusu shule moja ya sekondari inamilikiwa kanisa la kilutheri Tanzania na huwa inatoa msaada hasa kwa watoto yatima na washio katika mazingira magumu.
Baada ya kupata wazo Hilo nilipanga safari ya miguu kwenda shule ya sekondari Iambi na mfukoni nikiwa na hela ya kula Kama elfu tatu nilitoka asubuhi bila kuaga kwa mtu yeyote na nilifanikiwa kufika shuleni hapo saa 6 hivi mchana na nikapokelewa na mwalimu Mpuni nikamweleza sababu ya Mimi kuja hapo, akanichukua na kunipeleka kwa mkuu wa shule hiyo Mchungaji Elirehema Nkungu.
Mkuu huyo wa shule alinambia naweza kusaidiwa kwa kulipiwa ada nusu ikiwa nitafanya mtihani wao vizuri, Basi niliomba niufanye na nilipelekwa kwenye chumba Cha darasa nikiwa mwenyewe Somo la kwanza likiwa ni hesabu na baada ya kuuona mtihani kwa sababu hesabu pia ilichangia Mimi kupangiwa Tabora school niliuona mtihani wa kawaida sana nilipewa Lisa na nusu lakini ndani ya dakika 45 nikaufuta , nikaletewa tena wa Lugha nao kidogo nikamaliza nikatolewa nje kupata chakula nikapewa chakula na mwl El huyu ni mdada alikuwa anajitolea.
Baada ya kurudi kwenye paper la maarifa nalo mda kidogo nikalifuta na ikawa mwisho nikaenda kusubiri matokeo na baada ya kuitwa kwanza mkuu wa shule alifurahi sana na kunipongeza nikiwa nimepata hesabu zote pamoja na mitihani wa maarifa nao nimepata zote, Lugha tu ndio Kati ya maswali 50 nilipata 46 nikiwaachia 4 tu.
Baada ya matokeo hayo nikapewa barua yangu ya kuchaguliwa na kuibeba kwa furaha na ahadi ya kulipiwa ada nusu nikijua kiasi kilichobaki naweza kuwashawishi wazazi na kaka zangu kunisaidia, nikarudi home nilifika nyumbani saa 5 usiku pamoja na kupata lifti ya baiskeli baba aliniuliza ulikuwa wapi mpaka mda huu nikamwambia nilikuwa kwa rafiki zangu nikajikuta nimechelewa so sikutaka kumwambia ukweli maana alikuwa ameonja kidogo hivyo nikaona nitamweleza kesho.
Itaendeleaa..........
Leo nimependa kushare kidogo kuhusu historia ya maisha yangu inaweza kuwa funzo kwa mwingine pia.
Mara baada ya kumaliza darasa la Saba katika shule moja ya msingi mkoa wa Singida dc nilibahatika kuchaguliwa kujiunga na shule ya sekondari ya wavulana Tabora school, kwa bahati mbaya nilizaliwa katika familia ambayo bado haikuwa inatambua umuhimu wa elimu pamoja na ilikuwa na uwezo wa kunisomesha lakini haikuwa hivyo.
Mimi ni mtoto wa mwisho Kati ya watoto Tisa kutoka kwa baba mmoja na Mama mmoja hivyo nilikuwa napendwa sana kama mtoto wa mwisho na ndugu zangu wengine wapatao wanne walifaulu vizuri kwenye shule nzuri ambazo leo zinaitwa special school lakini wazazi waligoma kabisa kuwasomesha wakiwa na Imani wataenda kupotea, hivyo nami nikaunganishwa kwenye kundi hilo kuwa nitaenda kupotea na hivi ikizingatiwa Mimi ni mtoto wa mwisho na wazee wananipenda sana.
Baada ya kuomba ushauri kwa kaka zangu nao pia waligoma kabisa kunipa ushauri wowote na zaidi ya kuniambia kaa nyumbani wewe ndio utawalea wazazi na kuwatunza, nahisi kwa wale mliokulia Singida mnajua vizuri mtoto wa mwisho ndio mwenye jukumu la kubaki na wazazi kwa kipindi hicho,
Basi baada ya majibu hayo moyoni mwangu palikuwa na wingu zito la mawazo huku nikishuhudia wale tuliosoma wakiwa kwenye haraki za kujiandaa kuripoti shuleni na hasa marafiki tuliokuwa karibu sana na wengine walikuwa wa shule jirani na tulikuwa tukifanya mitihani ya ujirani mwema na kushindana kwa nguvu kubwa, pamoja na yote hayo sikuwa na njia nyingine ya kufanya.
Kuna siku nikiwa nachunga nikajiwa na wazo kwanini nisitafute shule za mashirika ya kidini niende kujieleza naweza pia kupata msaada wa kusomeshwa na ndugu wakiona juhudi zangu wanaweza kuamua kuanza kunipa msaada,
baada ya kupata wazo Hilo huku siku mbili nyuma nilisikia story kuhusu shule moja ya sekondari inamilikiwa kanisa la kilutheri Tanzania na huwa inatoa msaada hasa kwa watoto yatima na washio katika mazingira magumu.
Baada ya kupata wazo Hilo nilipanga safari ya miguu kwenda shule ya sekondari Iambi na mfukoni nikiwa na hela ya kula Kama elfu tatu nilitoka asubuhi bila kuaga kwa mtu yeyote na nilifanikiwa kufika shuleni hapo saa 6 hivi mchana na nikapokelewa na mwalimu Mpuni nikamweleza sababu ya Mimi kuja hapo, akanichukua na kunipeleka kwa mkuu wa shule hiyo Mchungaji Elirehema Nkungu.
Mkuu huyo wa shule alinambia naweza kusaidiwa kwa kulipiwa ada nusu ikiwa nitafanya mtihani wao vizuri, Basi niliomba niufanye na nilipelekwa kwenye chumba Cha darasa nikiwa mwenyewe Somo la kwanza likiwa ni hesabu na baada ya kuuona mtihani kwa sababu hesabu pia ilichangia Mimi kupangiwa Tabora school niliuona mtihani wa kawaida sana nilipewa Lisa na nusu lakini ndani ya dakika 45 nikaufuta , nikaletewa tena wa Lugha nao kidogo nikamaliza nikatolewa nje kupata chakula nikapewa chakula na mwl El huyu ni mdada alikuwa anajitolea.
Baada ya kurudi kwenye paper la maarifa nalo mda kidogo nikalifuta na ikawa mwisho nikaenda kusubiri matokeo na baada ya kuitwa kwanza mkuu wa shule alifurahi sana na kunipongeza nikiwa nimepata hesabu zote pamoja na mitihani wa maarifa nao nimepata zote, Lugha tu ndio Kati ya maswali 50 nilipata 46 nikiwaachia 4 tu.
Baada ya matokeo hayo nikapewa barua yangu ya kuchaguliwa na kuibeba kwa furaha na ahadi ya kulipiwa ada nusu nikijua kiasi kilichobaki naweza kuwashawishi wazazi na kaka zangu kunisaidia, nikarudi home nilifika nyumbani saa 5 usiku pamoja na kupata lifti ya baiskeli baba aliniuliza ulikuwa wapi mpaka mda huu nikamwambia nilikuwa kwa rafiki zangu nikajikuta nimechelewa so sikutaka kumwambia ukweli maana alikuwa ameonja kidogo hivyo nikaona nitamweleza kesho.
Itaendeleaa..........