Kutoka Mbagala Market hadi African Lyon

Kibunango

Platinum Member
Aug 29, 2006
8,420
2,271
Mkurugenzi wa Mohamed Enterprises, Mohamed Dewji ameamua kujitosa kupimana ubavu na Bakhresa katika ligi kuu ya Tanzania kwa kuamua kuinunua timu ya Mbagala Market ambayo imepanda ligi kuu.

Baada ya kampuni ya Bakhresa kuibuka na timu ya Azam katika ligi kuu ya Tanzania, mkurugenzi wa Mohamed Enterprises Tanzania LTD, Mohamed Dewji au maarufu kama Mo ambaye pia ni Mbunge wa Singida mjini, amejitambulisha rasmi kuimiliki timu ya African Lyon ambayo awali ilikuwa ikijulikana kwa jina la Mbagala Market.

Utambulisho huo ulifanyika katika Hotel ya Corasseum iliyoko Oysterbay Dar es Salaam.

Utambulisho huo uliambatana na kutunikiwa nishani wachezaji waliofanikiwa kuifikisha timu hiyo ligi kuu.

Mbwana Samaki ambaye ni mfungaji bora wa ligi daraja la kwanza alizawadiwa kikombe cha ufungaji bora.

Mmiliki huyo mpya aliwataka wachezaji hao kujituma ili kufanikisha timu hiyo inasonga mbele zaidi na kutwaa ubingwa wa ligi kuu msimu ujao.

Kwa upande wake Mo alisema kuwa atahakikisha timu hiyo haitakabiliwa na masuala ya ukata wa fedha au matatizo yoyote yale.

Kwa kuanzia tayari Dewji ameishanunua kiwanja ambacho anategemea kujenga kiwanja cha kisasa cha soka kitakachokuwa na viwanja vya michezo mingine kama vile sehemu ya gym ,maduka na hosteli za kulala wachezaji.

Uwanja huo upo eneo la Mbagala jijini Dar es Salaam.


Source: Nifahamishe
 
Hii ni habari njema kwa akina sie wapenzi wa Man U, Liverpool, Arsenal, Chelsea nk.
Zamani tuliweza kuona timu kama Mwadui, Pamba, Pilsner, Sigara, Ndovu, RTCs (Biasharas) na nyingine nyingi zilizokuwa zifanya vizuri na kupewa'tafu' na makampuni hayo. Baada ya mabadiliko makubwa ya kisera hasa kwenye uchumi timu hizo ziliishia kutemwa na kupotea. Ninawapongeza Mohamed Enterprises, Bakhressa, Viwanda vya Mtibwa na Kagera kwa kujitolea kuchangia maendeleo ya soka hapa Tanzania.

Ombi langu kubwa ni kuwa timu hizi ambazo zinaonekana kuwa na mfumo unaoeleweka katika uendeshaji soka, wahakikishe kuwa wanajenga base nzuri ya kukuza vipaji kwa kuwa na timu 'B' (timu B hasa, kama ilivyokuwa miaka ya nyuma pale Yanga na Simba) na zile za watoto wadogo. Mkifanikiwa kufanya hivyo basi hamtakuwa na matatizo ya usajili katika timu zenu.

Nawatakia kila la kheri
 
Hongera african Lyon, Nawaomba sana mlete chachu mpya ya soka hapa Tanzania. Vilabu vya mitaani (vya wanachama uchwara) vimepitwa na wakati na ndio maana wenzetu kama Kenya, Zambia n.k. vinapotea kabisa. na sasa unaweza kuona wanasoka wengi kutoka club kama Mathare utd wanacheza soka la kulipwa nje ya Kenya.

Sisi pia tungepanda kuwaona vijana wakifanya maajabu na vilabu vya kulipwa huko mbali sana...........Tafadhali jengeni msingi mzuri na endelevu..
 
Habari njema kwa wapenda michezo, lakini hawa jamaa (matajiri) hii tabia ya kusubiri vijana wahangaike huko underground then wakichomoza kuwadaka si nzuri labda iwe hasa kwa manufaa ya Club na si kujinufaisha kibiashara zaidi!

Pia tungependa kuona timu hii inapewa support consistently sio anaenda nayo weee then ikifika wakati kuona haimufaishi akaamua kuitelekeza.....akifanya hivyo ni kuvunja moya waanzilishi huko uswazi!
 


Ombi langu kubwa ni kuwa timu hizi ambazo zinaonekana kuwa na mfumo unaoeleweka katika uendeshaji soka, wahakikishe kuwa wanajenga base nzuri ya kukuza vipaji kwa kuwa na timu 'B' (timu B hasa, kama ilivyokuwa miaka ya nyuma pale Yanga na Simba) na zile za watoto wadogo. Mkifanikiwa kufanya hivyo basi hamtakuwa na matatizo ya usajili katika timu zenu.

Nawatakia kila la kheri

Ombi lako naona limeshafikiliwa, kwani pamoja na mambo mengine timu hiyo itakuwa na uwanja wake na hii itasaidia kuondoa timu za Dar kubanana uwanja wa Taifa...

Ila jina lao sio la kizalendo kabisa, na sijui nini kiliwasukuma kuchagua jina hilo.
Kwa kuanzia tayari Dewji ameishanunua kiwanja ambacho anategemea kujenga kiwanja cha kisasa cha soka kitakachokuwa na viwanja vya michezo mingine kama vile sehemu ya gym ,maduka na hosteli za kulala wachezaji.

Uwanja huo upo eneo la Mbagala jijini Dar es Salaam.
 
...hivi soka la kitanzania (premier league) ni tayari officially la kulipwa, au bado la ridhaa?

wachezaji wote wana mikataba ya kulipwa? kuna kiwango cha mishahara, bima ya wachezaji, na katika hayo?
 
Ombi lako naona limeshafikiliwa, kwani pamoja na mambo mengine timu hiyo itakuwa na uwanja wake na hii itasaidia kuondoa timu za Dar kubanana uwanja wa Taifa...

Ila jina lao sio la kizalendo kabisa, na sijui nini kiliwasukuma kuchagua jina hilo.

...kaka, hata Young Africans jina lao la kimazabe mazabe, usileweshwe na wazaramo kutamka kwao YANGA (younger!) :D
 
...hivi soka la kitanzania (premier league) ni tayari officially la kulipwa, au bado la ridhaa?

wachezaji wote wana mikataba ya kulipwa? kuna kiwango cha mishahara, bima ya wachezaji, na katika hayo?

Kwa timu zingine sijui ila nachojua kuhusu African Lyon (pronounced as in English, "lion") ni kwamba wanalipwa mshahara minimum 350,000 (it may be not much but what are the alternatives?), wamekatiwa bima wachezaji na 4 members of their families, na wengine ambao wapo shule wanalipiwa ada zao. The average age ya timu is 18 years and I think they are in a streak of 18 games without defeat, if I am not mistaken.

Good thing is that uongozi umebaki uleule wa Mbagala Market to most extent na mmoja wa wafadhili ni Meddy Rehmtulla, the Fifa and TFF approved soccer agent who recently took Simba players Henry Joseph and Ime Izechukwu for tryouts in Norway. Mo provided the plot which was the former Korosho complex in Mbagala/Temeke area. Check out their website: African Lyon FC

If you ask me, they would be going places! Watch!!!
 
Mkurugenzi wa Mohamed Enterprises, Mohamed Dewji ameamua kujitosa kupimana ubavu na Bakhresa katika ligi kuu ya Tanzania kwa kuamua kuinunua timu ya Mbagala Market ambayo imepanda ligi kuu.

Baada ya kampuni ya Bakhresa kuibuka na timu ya Azam katika ligi kuu ya Tanzania, mkurugenzi wa Mohamed Enterprises Tanzania LTD, Mohamed Dewji au maarufu kama Mo ambaye pia ni Mbunge wa Singida mjini, amejitambulisha rasmi kuimiliki timu ya African Lyon ambayo awali ilikuwa ikijulikana kwa jina la Mbagala Market.

Utambulisho huo ulifanyika katika Hotel ya Corasseum iliyoko Oysterbay Dar es Salaam.

Utambulisho huo uliambatana na kutunikiwa nishani wachezaji waliofanikiwa kuifikisha timu hiyo ligi kuu.

Mbwana Samaki ambaye ni mfungaji bora wa ligi daraja la kwanza alizawadiwa kikombe cha ufungaji bora.

Mmiliki huyo mpya aliwataka wachezaji hao kujituma ili kufanikisha timu hiyo inasonga mbele zaidi na kutwaa ubingwa wa ligi kuu msimu ujao.

Kwa upande wake Mo alisema kuwa atahakikisha timu hiyo haitakabiliwa na masuala ya ukata wa fedha au matatizo yoyote yale.

Kwa kuanzia tayari Dewji ameishanunua kiwanja ambacho anategemea kujenga kiwanja cha kisasa cha soka kitakachokuwa na viwanja vya michezo mingine kama vile sehemu ya gym ,maduka na hosteli za kulala wachezaji.

Uwanja huo upo eneo la Mbagala jijini Dar es Salaam.


Source: Nifahamishe

Habari ya zamani kidogo hii, hoja yangu ipo hapo pekundu. Bado huu uwanja upo? Timu imeshauzwa kwa wamiliki wawili tofauti, hii rasilmali bado ipo pamoja na umiliki wa timu? Na kama ipo inaendelezwaje? Na kama haipo kwanini wanunuzi wa timu hawakuidai kama sehemu ya timu waliyoinunua?
 
Kwani hii ni mara ya kwanza kwa Mohamed Enterprise kumiliki timu ya mpira hapa nchini? Kama aliwahi kumiliki timu huko nyuma nini ilikuwa hatima ya hiyo timu? Tafuteni historia ili mjue mpo wapi na mnaelekea wapi na sio kuswagwa kama mbuzi!!
 
Hii ndo ya Mo sijui iliishia wapi? Na huo uwanja maendeleo yake yakoje?
 
Habari ya zamani kidogo hii, hoja yangu ipo hapo pekundu. Bado huu uwanja upo? Timu imeshauzwa kwa wamiliki wawili tofauti, hii rasilmali bado ipo pamoja na umiliki wa timu? Na kama ipo inaendelezwaje? Na kama haipo kwanini wanunuzi wa timu hawakuidai kama sehemu ya timu waliyoinunua?
Kwa ufupi sina updates za hii issue kwa sasa.
 
Habari njema kwa wapenda michezo, lakini hawa jamaa (matajiri) hii tabia ya kusubiri vijana wahangaike huko underground then wakichomoza kuwadaka si nzuri labda iwe hasa kwa manufaa ya Club na si kujinufaisha kibiashara zaidi!

Pia tungependa kuona timu hii inapewa support consistently sio anaenda nayo weee then ikifika wakati kuona haimufaishi akaamua kuitelekeza.....akifanya hivyo ni kuvunja moya waanzilishi huko uswazi!
Ujumbe haukufanyiwa kazi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom