Kipimo unachotumia wewe ni cha mwisho kabisa kukitumia kupima maendeleo, pima maendeleo kwa kuangalia kiwango cha miundombinu na namna inavyotumiwa, serikali inawajibika kuweka miundombinu kwa ajili ya maendeleo..binadamu tunatofautiana watu wengine hawapendi kuwa na vitu vizuri..nyumba nzuri, gari nk mtu kama huyo utamlazimisha apate vitu unavyotaka wewe?Kuna kitu kimoja mnapaswa kuelewa. Pamoja na kwamba Kagame yuko very strict, huwezi kulinganisha Rwanda na Tanzania. Udogo wa Rwanda unafanya iwe rahisi sana kuiendeleza na kuifanya iwe hiyo world class unayoisema.
Magufuli, pamoja na ubaya wake, alitaka kuifanya Dar es Salaam iwe kama ulaya, lakini asingeweza kuifanya Tanzania yote iwe kama ulaya.
Ndio maana hata Singapore, kwa infrastructure na usafi na uzuri hata ulaya hawaifikii, kwa sababu ni ka nchi kadogo sana, imeendelea kwa kutumia bandari tu. Hata Norway ni hiyo hivyo. Sasa utamlaumuje mtu mwenye eka 20 kuwa shamba lake sio safi kama yule mwenye eka moja?
Nenda South Africa, pamoja na uchumi wao mkubwa, ukitoka nje ya jiji kilometa 50 tu utaona maisha ya rural areas Tanzania tunawaacha kwa mbali sana.
Hata China, wanapendeza mijini tu. Kuna sehemu za vijijini China wako hoi sana.
Kwa hiyo usimsifie sana Kagame kuwa ameifanya Rwanda kuwa nchi ya kuigwa, wakati ka-nchi kadogo. Ukitaka kumsifia Kagame basi mlinganishe na Zanzibar, sio Tanzania bara
Haya Rwanda ni nchi ndogo, ilinganishe na Zanzibar basi..zinalingana?
Ukubwa wa nchi na uwingi wa watu una faida nyingi na nafasi nzuri ya kupata maendeleo kuliko nchi ndogo yenye watu wachache.