Kutaifisha mabenki Marekani

Boma

Senior Member
Apr 5, 2008
189
8
Sasa hivi Serikali ya Marekani inataifisha Mabenki sita ambayo yalikuwa yanamilikiwa na watu binafsi. Serikali imelazimika kutaifisha mabenki hayo ili kuokoa uchumi wa nchi usiendelee kudidimia .

Mwaka 1967 Mwl JK Nyerere Rais wa Tanzania alitaifisha mabenki na Viwanda n.k akiwa na nia ya kujenga uchumia ambao aliona hauwezi kukuwa kwa haraka mikononi mwa watu binafsi.

Watu wengi walilaani sana jambo hilo, lakini kumbe ili kuokoa uchumi hali ikiwa mbaya serikali inatakiwa iendeshe mabenki kuweka mambo sawa, pengine tofauti ni uwezo wa ku-manage, dhamira kwa uongozi wote.

So far, kila nchi inaona hatua hiyo ya Marekani ni sawa na sioni wa kulaani, sasa Kwanini mzee wetu alipigwa madongo hata na watu wake . Mzee wa watu alijua nchi haiwezi kuendelea bila viwanda akajenga viwanda vya kila aina katika dhamira yake ilele ya kujenga uchumi, watu wake ambao hawakuwa na msaada sana kwake na hawaelewi nchi haiendelei bila VIWANDA wameviuza vyote sasa hivi, hivyo kuzungumza economical take off itachukua muda mrefu sana.
 
Hivi hii bail out Tanzania in work vipi kwani nakumbuka hivi karibum wali bail out TRC kwa kuwapa pesa za kuendeshea shughuli je sasa watgawana faida au vipi
 
Sasa hivi Serikali ya Marekani inataifisha Mabenki sita ambayo yalikuwa yanamilikiwa na watu binafsi. Serikali imelazimika kutaifisha mabenki hayo ili kuokoa uchumi wa nchi usiendelee kudidimia .

Mwaka 1967 Mwl JK Nyerere Rais wa Tanzania alitaifisha mabenki na Viwanda n.k akiwa na nia ya kujenga uchumia ambao aliona hauwezi kukuwa kwa haraka mikononi mwa watu binafsi.

Watu wengi walilaani sana jambo hilo, lakini kumbe ili kuokoa uchumi hali ikiwa mbaya serikali inatakiwa iendeshe mabenki kuweka mambo sawa, pengine tofauti ni uwezo wa ku-manage, dhamira kwa uongozi wote.

So far, kila nchi inaona hatua hiyo ya Marekani ni sawa na sioni wa kulaani, sasa Kwanini mzee wetu alipigwa madongo hata na watu wake . Mzee wa watu alijua nchi haiwezi kuendelea bila viwanda akajenga viwanda vya kila aina katika dhamira yake ilele ya kujenga uchumi, watu wake ambao hawakuwa na msaada sana kwake na hawaelewi nchi haiendelei bila VIWANDA wameviuza vyote sasa hivi, hivyo kuzungumza economical take off itachukua muda mrefu sana.

Hivi kinachafanyika Marekani ni kutaifisha au kununua mabenki.Ukitaifisha haulipi haulipi chochote lakini ukinunua unatakikana kulipa.Ukweli ni kuwa si Tanzania tu waliingilia kati kama Kampuni inakuwa hijiendeshi vizuri na hii tumeiona ina work ata ktk dunia ya kwanza.
 
Back
Top Bottom