Kutafuta mke mtandaoni...

Gates

Member
Jan 18, 2011
48
4
Limekuwa jambo la kawaida sasa kwa vijana kujitafutia wake kupitia mitandao ya kijamii. Inawezekana wapo wanaobahatika kupata wake wema lakini binafsi nadhani si jambo jema sana. Asilimia kubwa ya wanaotafuta wake kupitia mitandao huishia kudumbukia katika matatizo lukuki na hivyo hujuta kwanini alimuoa aliyemuoa. Nashauri vijana tumtegee Mungu katika swala la kutafuta mchumba kwani ni muhimu ukapata mtu mnayeendana kwa mambo mengi. Vijana tumrudie Mungu, tumtangulize Mungu katika maisha yetu kwani yeye ndiye jibu la mahitaji yetu yote ya kimwili na kiroho. Ameni.
 
Hata hao wamitandaon ni wa Mungu, suala n kumsoma mtu tabia before marriage, all n all mapenz yanatokea popote, haijalishi n wapi.
 
Mchumba/mume/mke anapatikana popote unaweza kumwomba Mungu na akakukutanisha na mtu wa kwenye mtandao na maisha yakaenda shwari. Kumbuka Mungu ni Roho zaidi. Kumbuka kuna watu wanasoana ambao walikuwa wanafahamiana tangu watoto tena wametokea eneo moja na wameoana na ndoa haidumu hivyo kufahamiana kwao siyo sababu. Isaka alitwaliwa mke ambaye hakumfahamu kabisa lakini waliishi vizuri. Kwani unayekutana nae kwenye gari, kanisani au kwenye public yoyote unakuwa unafahamiana nae ndo useme wa mtandaoni hawafai hivyohivyo unaweza fahamiana nae mtandaoni then mkaonana mkiridhiana mnaendelea kuwasiliana kujuana tabia n.k. Mími naamini mtandaoni kuna watu wastaarabu kuna watu wanadhani mtandaoni hakuna watu wastaarabu labda niwaulize wanaodhani hivyo wao siyo wastaarabu? Maana kama wao ni wastaarabu kwa nini wasidhani kuwa kwenye mitandao kuna watu na heshima zao na siyo wote mambulula? Watu walio mitandaoni ndo walewale walioko kwenye jamii zetu ambapo tunamwona mtu mwingine ana tabia za ajabu mwingine ana tabia nzuri hadi unatamani ukatake ushauri kwake. Tatizo mtandaoni huwezi wafahamu ila kupitia comment unawajua.
 
Back
Top Bottom