Kusimamishwa kazi kwa wakuu wa shule jiji la Arusha

godmasai

Senior Member
Apr 9, 2013
102
47
Wasalam wana jamvi,

Takribanni wiki moja imepita tangu tangazo kwa vyombo vya habari ilipotolewa na ofisi ya mkurugenzi wa jiji la Arusha kuhusu kuwasimamisha kazi wakuu wa shule, kwa kuwa imesemekana kuwa katika shule hizo wamo wanafunzi hewa.

Sasa maswali ya kujiuliza...

Je, ni uchunguzi gani wa kisayansi umefanyika hata ukathibitisha taarifa hizo za uwepo wa hao wanafunzi hewa?

Je, ni kweli fedha zilizotumwa na serikali zimetafunwa na hao wakuu wa shule?

Je, bodi za shule hizo pia si zingetakiwa kuwajibishwa kwa kuvunjwa kwa kuwa zinahusika moja kwa moja kupitisha matumizi ya fedha zinazotumwa na serikali.

Je, suala la wanafunzi wanaohamia shule nyingine kama za serikali au binafsi limeangaliwa vipi, na vile vile wanafunzi wanaoacha shule kwa kupata ujauzito, utoro kifo na kadhalika limetolewa muongozo gani ili fedha zao zinazotumwa zirudishwe serikali?

Je, Serikali imetuma auditing team kuthibitisha kuwa kuna fedha zinazosemekana za wanafunzi hewa kuwa zimetafunwa?

Mambo ni mengi ya kujiuliza, lakini inaonekana uamuzi umefanyika kwa uonevu ili baadhi ya kundi fulani waonekane wamefanya kazi ya maana kumbe ni kutafuta umaarufu kwa uonevu.

Pia maamuzi haya yatasabisha kikubwa kuyumba kwa maendeleo ya elimu ususani jiji la Arusha.

Mtazamo wangu, taarifa za mwaka jana zilizotumika kuwahukumu na kuwasimamisha kazi wakuu wa shule ni za kiuonevu.
 
Tatizo la wakuu wa shule wanafanya kaz kwa mazoea, kwa mfano

i. Unakuta mwanafunzi ameacha shule ila rekodi zake zinaonekana ktk daftari la mahudhurio kwa miezi hata 6.

ii. Kila mwezi wanatuma taarifa za utoro sugu bila ya kuonyesha hatua zilizochukuliwa dhidi yao(kisheria mwanafunzi akikaa bila kuja shule kwa miezi 3 mfululizo anafukuzwa shule ).

iii. Serikali ilpoanza kutoa fedha za elimu bure wakuu wengi wa shule sidhani kama wametoa taarifa zozote kuhusu idadi ya mwanafunzi kuwa imeshuka au imeongezeka ili fedha iongezwe au ipunguzwe.
 
Tatizo la wakuu wa shule wanafanya kaz kwa mazoea, kwa mfano i. unakuta mwanafunzi ameacha shule ila rekodi zake zinaonekana ktk daftari la mahudhurio kwa miez hata 6. ii. Kila mwezi wanatuma taarifa za utoro sugu bila ya kuonyesha hatua zilizochukuliwa zidi yao(kisheria mwanafunzi akikaa bla kuja shule kwa miez 3 mfululizo anafukuzwa shule ). iii. Serikali ilpoanza kutoa fedha za elm bure wakuu wengi wa shule sidhani kama wametoa taarfa zozote kuhusu idadi y mwanafunzi kuwa imeshuka au imeongezeka ili fedha iongezwe au ipunguzwe.
Hayo maandishi yako yanaonyesha kama vile na wewe ulikuwa mtoro shuleni
 
Acheni kulalamika hovyo kwani lazima kuwa mkuu?tToka juzi naona hizi post za hovyohovyo,kwanza kazi zenyewe this time hazithaminiwi kabisa
 
Tatizo la wakuu wa shule wanafanya kaz kwa mazoea, kwa mfano

i. Unakuta mwanafunzi ameacha shule ila rekodi zake zinaonekana ktk daftari la mahudhurio kwa miezi hata 6.

ii. Kila mwezi wanatuma taarifa za utoro sugu bila ya kuonyesha hatua zilizochukuliwa dhidi yao(kisheria mwanafunzi akikaa bila kuja shule kwa miezi 3 mfululizo anafukuzwa shule ).

iii. Serikali ilpoanza kutoa fedha za elimu bure wakuu wengi wa shule sidhani kama wametoa taarifa zozote kuhusu idadi ya mwanafunzi kuwa imeshuka au imeongezeka ili fedha iongezwe au ipunguzwe.
Kwa muongozo upi mkuu, je serikali imesenaje kuhusu hayo hapo juu; bado kuna changamoto lukuki kwenye elimu msingi bila malipo
 
Back
Top Bottom