Uwezo Tunao
JF-Expert Member
- Nov 14, 2010
- 6,942
- 1,190
KAMA HATA MHE MBUNGE HAYUKO SALAMA WANANCHI TUKIMBILIE WAPI???
Kwa kitendo hiki cha ajabu (Askari Polisi Kumpiga Mh Mbunge) sana kuwahi kufanywa nchini mwetu, WAZIRI WA MAMBO YA NDANI PAMOJA NA SAID MWEMA WOTE WAJIUZULU mara moja kwa kuzingatia MSINGI WA UWAJIBIKAJI katika dhana zima ya Utawala bora na huyo askari awajibishwe kwa Maslahi ya Umma!!
Hili la askari kumpiga mbele ya hadhara Mhe Mbunge mbele ya wananchi anaowaongoza kamwe HAIKUBALIKI na wala HAIVUMILIKI hata kidogo. Katika hili hakuna kiwango chochote cha MAELEZO WALA VISINGIZIO vitakavyoweza kutolewa kuhalalisha CHOMBO CHOCOTE KUMDHALILISHA KIONGOZI kiasi hicho.
Chombo chetu cha jeshi la polisi KIKATIBA ni chombo USALAMA NA UTULIVU kumshambuliwa kiongozi yeyote bila kujali itikadi yake ya kisiasa nchini. Kitendo hiki hakina tofauti sana na kitendo cha KUMPIGA BABA AU MAMA MZAZI mbele ya watoto wake.
Msononeko kwa watoto hautokaa ufutike kiurahisi kwenye kumbukumbu zao na hata kusadikiwa jambo kama hili kusababisha madhara makubwa kisaikolojia katika jamii. Ni kutokana na ukweli huu ndio MAANA SHERIA KOKOTE DUNIANI HUTOA ADHABU KALI MNO kwa wadhalilishaji wa aina ya askari polisi huyu wa Arusha.
Siku zote watoto pale nyumbani huamini kwama ama BABA AU MAMA NDIO WATU WENYE NGUVU KULIKO WOTE DUNIANI kiasi kwamba wanapoona mashujaa wao hawa wakipigwa hadharani basi ujue moja kwa moja kwamba mpaka hapo Ulimwengu wao unakua umefunikwa juu kutazama chini.
Kitendo cha KUSHAMBULIWA KWA MANENO NA KIWILI NA KUJERUHIWA kwa mwakilishi halali wa raia bungeni akiwa katika eneo lake ya kazi jimboni kwake Arusha ni kitendo UDHALILISHAJI MKUBWA mbele ya macho ya umma wa Tanzania.
Kama hilo halitoshi na tunaiomba Bunge letu la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kamati zake za (i) Kamati ya Maadili na (ii) Kamati ya Ulinzi na Usalama kukutana mara moja na KUSHUGHULIKIA KWA NAMNA ITAKAVYOTURIDHISHA WANANCHI JUU YA HUU UTOVU MKUBWA WA NIDHAMU uliofanywa na askari wetu kwa kiongozi wa ngazi ya juu wa ngazi ya ubunge kama alivyofanyiwa Mhe Lema.
Hili ni jambo zito lisilohitaji hiyana hata kidogo. Nani analo jibu atakayepigwa kesho au kesho kutwa kati ya viongozi wetu. Huwezi kujua kesho huenda akapigwa Waziri, Waziri Mkuu au hata Raisi wetu. Japo Rais katukashirisha sana alilolifanyia taifa kwenye uchaguzi mkuu lisilokubalika lakini mtu kumpiga hatuwezi kukubali hata kidogo.
Kwa kitendo hiki cha ajabu (Askari Polisi Kumpiga Mh Mbunge) sana kuwahi kufanywa nchini mwetu, WAZIRI WA MAMBO YA NDANI PAMOJA NA SAID MWEMA WOTE WAJIUZULU mara moja kwa kuzingatia MSINGI WA UWAJIBIKAJI katika dhana zima ya Utawala bora na huyo askari awajibishwe kwa Maslahi ya Umma!!
Hili la askari kumpiga mbele ya hadhara Mhe Mbunge mbele ya wananchi anaowaongoza kamwe HAIKUBALIKI na wala HAIVUMILIKI hata kidogo. Katika hili hakuna kiwango chochote cha MAELEZO WALA VISINGIZIO vitakavyoweza kutolewa kuhalalisha CHOMBO CHOCOTE KUMDHALILISHA KIONGOZI kiasi hicho.
Chombo chetu cha jeshi la polisi KIKATIBA ni chombo USALAMA NA UTULIVU kumshambuliwa kiongozi yeyote bila kujali itikadi yake ya kisiasa nchini. Kitendo hiki hakina tofauti sana na kitendo cha KUMPIGA BABA AU MAMA MZAZI mbele ya watoto wake.
Msononeko kwa watoto hautokaa ufutike kiurahisi kwenye kumbukumbu zao na hata kusadikiwa jambo kama hili kusababisha madhara makubwa kisaikolojia katika jamii. Ni kutokana na ukweli huu ndio MAANA SHERIA KOKOTE DUNIANI HUTOA ADHABU KALI MNO kwa wadhalilishaji wa aina ya askari polisi huyu wa Arusha.
Siku zote watoto pale nyumbani huamini kwama ama BABA AU MAMA NDIO WATU WENYE NGUVU KULIKO WOTE DUNIANI kiasi kwamba wanapoona mashujaa wao hawa wakipigwa hadharani basi ujue moja kwa moja kwamba mpaka hapo Ulimwengu wao unakua umefunikwa juu kutazama chini.
Kitendo cha KUSHAMBULIWA KWA MANENO NA KIWILI NA KUJERUHIWA kwa mwakilishi halali wa raia bungeni akiwa katika eneo lake ya kazi jimboni kwake Arusha ni kitendo UDHALILISHAJI MKUBWA mbele ya macho ya umma wa Tanzania.
Kama hilo halitoshi na tunaiomba Bunge letu la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kamati zake za (i) Kamati ya Maadili na (ii) Kamati ya Ulinzi na Usalama kukutana mara moja na KUSHUGHULIKIA KWA NAMNA ITAKAVYOTURIDHISHA WANANCHI JUU YA HUU UTOVU MKUBWA WA NIDHAMU uliofanywa na askari wetu kwa kiongozi wa ngazi ya juu wa ngazi ya ubunge kama alivyofanyiwa Mhe Lema.
Hili ni jambo zito lisilohitaji hiyana hata kidogo. Nani analo jibu atakayepigwa kesho au kesho kutwa kati ya viongozi wetu. Huwezi kujua kesho huenda akapigwa Waziri, Waziri Mkuu au hata Raisi wetu. Japo Rais katukashirisha sana alilolifanyia taifa kwenye uchaguzi mkuu lisilokubalika lakini mtu kumpiga hatuwezi kukubali hata kidogo.