Ironbutterfly
JF-Expert Member
- Feb 5, 2023
- 3,044
- 8,165
Habari za mida hii wakuu,
Mida ya saa 7 mchana nilikuwa natokea Nzega kwenda Singida, ila kwakuwa kuna kijiji hapo kati nilitakiwa kuonana na mdau mmoja wa bomba la mafuta anipatie documents fulani hivi, so nilipanda usafiri wa daladala/hiace.
Tumefika maeneo ya Nkinga Hospital kituo cha bus mbele yake kidogo kama kilometa 1, traffic mmoja akasimamisha hiace nilopanda, akaenda upande wa dereva, wakateta kidogo, then akapanda mzee mmoja na vijana wawili walofungwa pingu pamoja, wakaketi. Traffic akarudi upande wake.
Safari ikaendelea na konda akaendelea kujaza abiria hadi kubanana vya kutosha, akawasimamisha wale walofungwa pingu na yule mzee kupisha abiria wengine waketi.
Basi Safari ikaendelea huku hiace ikiwa imejaza nyomi. Mie nilipofika Kijiji nilichokuwa namkuta jamaa, nikashuka, hiace ikaendelea na Safari zake. Ila imenistaajabisha sana, utaratibu wa kusafirisha watuhumiwa ukoje?
Wajuzi mje mtufungue macho, nawasilisha.
Mida ya saa 7 mchana nilikuwa natokea Nzega kwenda Singida, ila kwakuwa kuna kijiji hapo kati nilitakiwa kuonana na mdau mmoja wa bomba la mafuta anipatie documents fulani hivi, so nilipanda usafiri wa daladala/hiace.
Tumefika maeneo ya Nkinga Hospital kituo cha bus mbele yake kidogo kama kilometa 1, traffic mmoja akasimamisha hiace nilopanda, akaenda upande wa dereva, wakateta kidogo, then akapanda mzee mmoja na vijana wawili walofungwa pingu pamoja, wakaketi. Traffic akarudi upande wake.
Safari ikaendelea na konda akaendelea kujaza abiria hadi kubanana vya kutosha, akawasimamisha wale walofungwa pingu na yule mzee kupisha abiria wengine waketi.
Basi Safari ikaendelea huku hiace ikiwa imejaza nyomi. Mie nilipofika Kijiji nilichokuwa namkuta jamaa, nikashuka, hiace ikaendelea na Safari zake. Ila imenistaajabisha sana, utaratibu wa kusafirisha watuhumiwa ukoje?
Wajuzi mje mtufungue macho, nawasilisha.