Mjomba wa taifa
JF-Expert Member
- Apr 20, 2012
- 231
- 161
Taarifa zilizo rasmi kutoka kwa baadhi vya viongozi waandamizi wa NIDA ni kuwa zoezi lililofanyika la uandikishaji vitambulisho vya uraia jijini DSM litarudiwa upya kutokana na kuvurunda kwa waandikishaji. Taarifa hizo zinasema katika vituo vingi vya uandikishaji wahusika waliopewa jukumu hilo hawakuwa na uwezo licha ya kupewa mafunzo elekezi kabla ya Zoezi hilo.
Imebainika kuwa waandikishaji wengi walipewa nafasi hizo kishikaji (as usual) pasipo kuwa na sifa za kutosha, walikuwa na elimu ya darasa la saba na kidato cha nne.
Gharama zilizotumika katika zoezi lililoharibika zinafidiwa vipi? Muda uliotumiwa kutokwenda kazini na kupanga foleni utafidiwa vipi? Ni nani aliyehusika kutoa nafasi za kazi kwa watu wasio na sifa hata kufikia kuvurunda kwa zoezi zima?
Madhara haya yataendelea kuumiza watanzania WENYE HATIA ya kuchagua viongozi vipofu na hatimae kuletewa viongozi/watendaji KISHIKAJI katika ngazi zote.
Imebainika kuwa waandikishaji wengi walipewa nafasi hizo kishikaji (as usual) pasipo kuwa na sifa za kutosha, walikuwa na elimu ya darasa la saba na kidato cha nne.
Gharama zilizotumika katika zoezi lililoharibika zinafidiwa vipi? Muda uliotumiwa kutokwenda kazini na kupanga foleni utafidiwa vipi? Ni nani aliyehusika kutoa nafasi za kazi kwa watu wasio na sifa hata kufikia kuvurunda kwa zoezi zima?
Madhara haya yataendelea kuumiza watanzania WENYE HATIA ya kuchagua viongozi vipofu na hatimae kuletewa viongozi/watendaji KISHIKAJI katika ngazi zote.