Kupandishana vyeo kijanja kunatuumiza kata ya Kyengege Iramba Singida

Luushu

JF-Expert Member
Apr 8, 2012
812
468
Habari Wana jamvi,

Huku kwetu kumekuwa na ka staili ka KUPANDISHANA VYEO KIJANJA, kwenye kata yetu tulikuwa na weo mwenye Degree na kazi alikuwa anachapa ipasavyo akahamishwa kapelekwa kata jirani ya ulemo na kyengege akaletwa veo mwenye certificate kutoka Kijiji Cha kidaru kuja kuwa kaimu weo Sasa ni mwaka wa pili na nusu

Swali kwa mamlaka husika ni kweli hakuna waajiriwa wenye sifa mpaka akaimishwe huyu,hapa katani wapo veo Wana diploma kwa Nini hawakukaimishwa kakaimishwa veo Makala wa kidaru?

Pia mwaka huu mwezi wa pili alihamishwa mwalimu mkuu mwenye degree kutoka shule ya msingi Mugundu,akaletwa mwalimu mwenye certificate kutoka shule jirani ya kyengege kuja kukaimu ualimu mkuu wakati hapo shuleni wapo walimu wenye diploma ambao kwa uelewa wangu ndio walifa kukaimu kitu ambacho kimeleta mfarakano mkubwa Kati ya walimu.

Swali afisa elimu,mkurugenzi mmeridhika haya yanayotokea au mnapewa vi memo na mwenyekiti wa halmashauri ambae ndie diwani wa kata hii, au mnapewa vimemo na waziri wa fedha ambae ametoka kwenye kata hii na mnashindwa kukataa kwa kutetea kibarua chenu?

Kama ni hivyo basi tunaomba mamlaka za juu zaidi zije zitusaidie ikiwemo takukuru mkoa ichunguze harufu ya rushwa inayo sababisha kushuka kwa maendeleo kata ya kyengege na kushuka kiwango Cha elimu shule ya msingi Mugundu
 
Mkuu inabidi utwambie kwanza kama hayo madaraka kama yanahitaji vigezo vya ngazi ya elimu uliyoitaja.
Mfano labda ili uwe veo ni mpaka uwe na degree,kama sio basi mnajilisha upepo tu.

Zipo kazi uzoefu na uwezo kazini ndio unaongea na sio elimu za darasani.

Hii kasumba ya kuamini vyeti kila sehemu ndio imefanya tuna maprofesa wa uchumi wa trab na trat.
 
Mkuu inabidi utwambie kwanza kama hayo madaraka kama yanahitaji vigezo vya ngazi ya elimu uliyoitaja.
Mfano labda ili uwe veo ni mpaka uwe na degree,kama sio basi mnajilisha upepo tu.

Zipo kazi uzoefu na uwezo kazini ndio unaongea na sio elimu za darasani.

Hii kasumba ya kuamini vyeti kila sehemu ndio imefanya tuna maprofesa wa uchumi wa trab na trat.
Mwongozo unasema walimu wakuu waanzie diploma kwenda degree Sasa wakiwepo wengi ndio tuanaangalia nani ana uwezo kuwazidi wengine,Hali kadhalika ma weo nao mwongozo ni huo huo

Pointi yako ya uzoefu ni sawa Ila Sasa ungekuwepo katani ungejionea mwenyewe uwezo wao ni hafifu wale walio hamishwa uwezo wao ulikuwa juu sana ukiachilia mbali degree zao
Kama shuleni tangu mwezi wa tatu shule Haina kamati ya shule hii haihitaji uwe na degree ndio ujue shule ni lazima iwe na kamati sijui wenzangu mwongozo uko vipi hapo waliopitia wizara ya elimu tupeni mwongozo
 
Back
Top Bottom