Ngahekapahi
JF-Expert Member
- May 8, 2012
- 553
- 366
Ndugu zangu wanajamvi mimi hii kitu sielewi inalenga nini,na kwa upande wangu naona kama serikali imeshindwa kabisa kutekeleza wajibu wake.Kila leo unasikia gharama za huduma mbalimbali zikipanda mfano DAWASA kuanzia july wanapandisha gharama za maji,ambapo maji hayo hayapatikani sehemu zote kama inavyopaswa hapa Dar.TANESCO wakaongeza gharama za umeme,watu wa DALADALA na wenyewe wakata ongezeko la 150%,Vyakula bei juu.Wakati huo haya yote yanamkuta mtanzania mshahara wake au pato lake liko palepale.Sasa hii ni kumkomoa Mtanzania au nini ndugu zangu.Naomba kuwasilisha.