Kuna haja ya TCRA kuendelea kuwepo?

HKBW

JF-Expert Member
Aug 4, 2009
468
342
Nimejaribu kuelewa kile TCRA walichokieleza kwa waandishi wa habari na nimebakia na swali kama bado wana haja ya kuwepo au lah!

Malalamiko ya wananchi na majibu waliotoa ni tofauti kabisa. Najiuliza ni kwa nini hasa wanafanya hivi, kwakuwa wanatudharau na kujua hatuna cha kufanya. Au kuna kitu zaidi wanapata toka kwa hao watoa huduma.

Sioni namna nchi hii tunaweza kuendelea kama upatikanaji wa internet unakuwa ghari kwa wananchi wa kawaida.

Katika karne hii ya 21 kuna mtu anapanga bei kulingana na MB, halafu hapo hapo anasema quality picha imeongezeka, applokesheni zipo nyingi na spidi imeongezeka. Hili pekee ni sababu ya kuwafanya wao wawalazimishe watoa huduma kushusha bei kutokana na mahitaji kuongezeka.

Halafu wanatufanya wajinga kwa kufaninisha bei na nchi nyingine, hizi bei wanazozilinganisha ni za mobile data kitu ambacho tunapaswa kuwa tumeachananacho. Hilo ni mbali na hizo data kuwa za uongo.

Ule mkongo wa TAIFA unatunufaishaje sisi wananchi, mbona hatuoni nafuu ya kuwa nao. Ikiwa TCRA wameshindwa kuusimamia ili utunufaishe kwa kusambaza mtandao majumbani na kwenye ofisi kuna haja ya kuwa na hii mamlaka?

Mi naona kodi zetu zinapotea bure kwa watu wasiokuwa na maslahi na sisi wala taifa letu.
 
Binafsi sioni faida ya TCRA kwa wananchi. Unyonyaji wa makampuni ya simu uko palepale na wala hawana utetezi wowote!
 
Sasa ambacho huelewi ni nini?

wamejibu thought za wananchi.

watu wanalalamika Voda wanaiba MBs, ndo unaambiwa MBs haziibiwibila kuna updates za simu, Speed ya mtandao kuwa kubwa nk.

Imagine uneingia Youtube umefungua video ya Dkk 10 ambayo ina mbs 350 kwa 4k

hiyo video ukiifungua tuu ndani ya Dkk 1 ukiwa na 4G ya Voda unakuta youtube App imeipakua yote,

wewe ukiskip ukisema sio hii ujue Mbs zako 350 zimeenda,

Hivi ndio vitu watanzania wanajuliswa.

Huwa nashangaa unakuta Mtu anasema Voda wanaiba Mbs, Shaaaaaaame kabisa, Voda wakuigi mbs???


Na kuhusu mkongo wa taifa upo nchi nzima, hakuna wilayabhaina mkongo nchi hii, labda kama imeanzishwa Juzi, Ongea na TTcL uvute mkongo kwako,
 
Halafu wanatufanya wajinga kwa kufaninisha bei na nchi nyingine, hizi bei wanazozilinganisha ni za mobile data kitu ambacho tunapaswa kuwa tumeachananacho. Hilo ni mbali na hizo data kuwa za uongo.
Walidhani watakaoona kipindi ni wananchi wa vijiji vya mwambao wa ziwa Tanganyika
 
Ule mkongo wa TAIFA unatunufaishaje sisi wananchi, mbona hatuoni nafuu ya kuwa nao. Ikiwa TCRA wameshindwa kuusimamia ili utunufaishe kwa kusambaza mtandao majumbani na kwenye ofisi kuna haja ya kuwa na hii mamlaka?
Ni kama yule checkbob alivyotufanyia kwenye gas na kwenye mkongo vivyohivyo
 
Sasa ambacho huelewi ni nini?

wamejibu thought za wananchi.

watu wanalalamika Voda wanaiba MBs, ndo unaambiwa MBs haziibiwibila kuna updates za simu, Speed ya mtandao kuwa kubwa nk.

Imagine uneingia Youtube umefungua video ya Dkk 10 ambayo ina mbs 350 kwa 4k

hiyo video ukiifungua tuu ndani ya Dkk 1 ukiwa na 4G ya Voda unakuta youtube App imeipakua yote,

wewe ukiskip ukisema sio hii ujue Mbs zako 350 zimeenda,

Hivi ndio vitu watanzania wanajuliswa.

Huwa nashangaa unakuta Mtu anasema Voda wanaiba Mbs, Shaaaaaaame kabisa, Voda wakuigi mbs???


Na kuhusu mkongo wa taifa upo nchi nzima, hakuna wilayabhaina mkongo nchi hii, labda kama imeanzishwa Juzi, Ongea na TTcL uvute mkongo kwako,
Kuna haja gani ya kuwa na mtandao unaotembea 5mb/s wakati mb 500 ni buku?
 
Mimi mwenyewe siungagi voda maana kitu cha kufungua kwa mb 5 voda itatumia mb 30
 
Back
Top Bottom