Kumtoa mtoto!!

Mvaa Tai

JF-Expert Member
Aug 11, 2009
6,159
4,443
Wana Jamvi weekend hii nimepata kadi ya mchango ambayo sijawahi kuchangia mchango wa aina hiyo, kadi yenyewe ina heading isemayo "Mchango wa Maulidi" inaendelea kusema Bwana na Bi xxx wanaratajia kumtoa mtoto wao kipenzi mwanzoni mwa mwezi December, hivyo mimi kama rafiki, Ndugu au jamaa wa karibu wananiomba mchango wa hali na mali ili kufanikisha jambo hilo muhimu.

Kwasababu ni watu wa imani tofauti na mimi na nilifahamiana nao nikiwa nanunua Shamba huko bagamoyo, nimehisi pengine kumtoa mtoto si kitu kigeni ila ni mimi tu sifahamu na nikiwauliza wao wanaweza kuhisi nina dharau ilihali wao wameniheshimu kwa kunishirikisha jambo(Hivyo nimekubali kushiriki bila kujua 'kumtoa mtoto' ni nini). Sijajua wanamaanisha nini je wanataka kumfanyia mtoto Sendoff au Harusi? Naombeni anayefahamu mchango wa maulidi ni nini, na kumtoa mtoto ni nini anisaidie kabla sijachangia ili nifahamu uzito wa jambo lenyewe maana naamini humu wanapitia watu wa aina mbalimbali na exposure tofauti tofauti.
 
Hakuna kitu kinanibo na kurudisha nyuma maendeleo na mambo muhimu kama michango!!! Nisamehewe ila sipendi na huwa sichangi, nachanga kwa vitu important na watu important, tena kile nilichonacho sio kile watakacho. Nways cjui maana, ngoja wenyeji waje!
 
Mkuu ulivyotaja tu bagamoyo kilichonijia akilini ni mambo mawili kuhusu hiyo kadi ya mchango uliyopewa;

1. Kumtoa mtoto yaweza kuwa kwamba aliyekupa kadi mke wake au mwanamke alijifungua mtoto siku kadhaa zilizopita hivyo huyo mtoto baada ya kuzaliwa then anahitajika kufanyiwa kasherehe ambapo sasa atakuwa anaweza kuchanganyika na other members of the community. Sijui ni watu wa itikadi gani lakini kama ni waislam hiyo kitu huitwa siku 40 baada ya mtoto kuzaliwa ambapo huendana na kisomo ( maulidi) watu hula na kunywa na kufurahi na ndipo hata huyo mtoto hunyolewa zile nywele wanazoita za utotoni yaani alizozaliwa nazo.

2. Huenda huyo aliyekupa kadi ana binti yake aliyevunja ungo na kwa mila zao huwekwa ndani kwa muda fulani akifundishwa mambo yanayoendana na majukumu ya mwanamke then baada ya huo muda hufanyika sherehe ya kumtoa huyo binti. Hii mara nyingi huendana na sherehe ya ngoma zaidi sijawahi kuona maulid ikifanyika zaidi ya watu kula, kunywa na kucheza.....Nina uhakika moja kati ya haya mawili linahisika hapo!
 
Mkuu ulivyotaja tu bagamoyo kilichonijia akilini ni mambo mawili kuhusu hiyo kadi ya mchango uliyopewa;

1. Kumtoa mtoto yaweza kuwa kwamba aliyekupa kadi mke wake au mwanamke alijifungua mtoto siku kadhaa zilizopita hivyo huyo mtoto baada ya kuzaliwa then anahitajika kufanyiwa kasherehe ambapo sasa atakuwa anaweza kuchanganyika na other members of the community. Sijui ni watu wa itikadi gani lakini kama ni waislam hiyo kitu huitwa siku 40 baada ya mtoto kuzaliwa ambapo huendana na kisomo ( maulidi) watu hula na kunywa na kufurahi na ndipo hata huyo mtoto hunyolewa zile nywele wanazoita za utotoni yaani alizozaliwa nazo.

2. Huenda huyo aliyekupa kadi ana binti yake aliyevunja ungo na kwa mila zao huwekwa ndani kwa muda fulani akifundishwa mambo yanayoendana na majukumu ya mwanamke then baada ya huo muda hufanyika sherehe ya kumtoa huyo binti. Hii mara nyingi huendana na sherehe ya ngoma zaidi sijawahi kuona maulid ikifanyika zaidi ya watu kula, kunywa na kucheza.....Nina uhakika moja kati ya haya mawili linahisika hapo!

Thanks mkuu ngoja nisubiria wengine kama wana maana zaidi ya hii, lakini mpaka hapa sijaona kama natakiwa kuchangia hasa katika kipindi hiki kigumu
 
Hakuna kitu kinanibo na kurudisha nyuma maendeleo na mambo muhimu kama michango!!! Nisamehewe ila sipendi na huwa sichangi, nachanga kwa vitu important na watu important, tena kile nilichonacho sio kile watakacho. Nways cjui maana, ngoja wenyeji waje!
Tatizo dada yangu ni definition ya vitu important ni vipi hivyo? ndiyo maana hata hili swala wamenisisitiza kwamba nitoe mchango ili kufanikisha "swala hili muhimu"
 
Kutoa ni moyo na si utajiri. Kumbuka huyo ni jirani yako, leo kwake, kesho kwako!
 
Tatizo dada yangu ni definition ya vitu important ni vipi hivyo? ndiyo maana hata hili swala wamenisisitiza kwamba nitoe mchango ili kufanikisha "swala hili muhimu"
..Mkuu haya mambo ukiyaangalia kwa undani utagundua ni kamtindo kamezoeleka ndani ya jamii kuchangiana kwa yale mambo ambayo yanahusisha jamii husika. lakini kiukweli hayana tija hata kidogo. Niliwahi wakati fulani kusababisha manung'uniko na mtafaruku kwenye familia yetu. Tulikuwa na mtoto wa sister wetu amepata admission CBE kusoma Advanced Diploma (Self sponsorship) at the same time tulikuwa na mtoto wa baba yetu mkubwa anataka kuoa. Utakuta yote yalikuwa yanatutegemea cc kuchangia mambo yote. Nikatoa wazo baada ya kuona hali kwa mambo yote mawili hayaendi. Kwa nini tusielekeze nguvu kumchangia huyu mwanafunzi aende chuo then huyu anayetaka kuoa achukue tu mke wake kwa a very simple sherehe...Weeeeeeh!!!!! Yalitoka maneno hapo acha tu sitaki kukumbuka hiyo siku...Kwa hiyo ili ku-maintain mahusiano na ujirani mwema we changia tu ulichonacho....
 
Mambo ya makabwela wa Buguruni hayo. Huko masaka na chuo kikuu nakoishi mtaalam hakuna mambo ya kumtoa mtoto wala kumuingiza.

Baada ya hilo, kaa tayari kwani muda si mrefu utaambiwa mchango mwingine wa mtoto kuingizwa suna.

Hapo kigodoro lazima kiwepo
 
..Mkuu haya mambo ukiyaangalia kwa undani utagundua ni kamtindo kamezoeleka ndani ya jamii kuchangiana kwa yale mambo ambayo yanahusisha jamii husika. lakini kiukweli hayana tija hata kidogo. Niliwahi wakati fulani kusababisha manung'uniko na mtafaruku kwenye familia yetu. Tulikuwa na mtoto wa sister wetu amepata admission CBE kusoma Advanced Diploma (Self sponsorship) at the same time tulikuwa na mtoto wa baba yetu mkubwa anataka kuoa. Utakuta yote yalikuwa yanatutegemea cc kuchangia mambo yote. Nikatoa wazo baada ya kuona hali kwa mambo yote mawili hayaendi. Kwa nini tusielekeze nguvu kumchangia huyu mwanafunzi aende chuo then huyu anayetaka kuoa achukue tu mke wake kwa a very simple sherehe...Weeeeeeh!!!!! Yalitoka maneno hapo acha tu sitaki kukumbuka hiyo siku...Kwa hiyo ili ku-maintain mahusiano na ujirani mwema we changia tu ulichonacho....
Inauma sana kufanya kitu kinafiki any way nitafanya hivyo kinafiki lakini huwa sifurahishwi na vimichango vya aina hii
 
Kutoa ni moyo na si utajiri. Kumbuka huyo ni jirani yako, leo kwake, kesho kwako!

Tatizo siyo kutoa ishu unatoa kwasababu gani? unajua watu wamezoea kuchangisha imefikia mahala watu wana changisha hata Birthdays au graduations
 
I bet mumber 1 suits to your question...by the way kuna haja sana ya kujitathmini na hizi mila zinazokomba kila

senti tunayosevu...manake michango mingi ya sisi makabwela ni ya starehe za muda mfupi zisizo na tija..lolest!
...1. Kumtoa mtoto yaweza kuwa kwamba aliyekupa kadi mke wake au mwanamke alijifungua mtoto siku kadhaa zilizopita hivyo huyo mtoto baada ya kuzaliwa then anahitajika kufanyiwa kasherehe ambapo sasa atakuwa anaweza kuchanganyika na other members of the community. Sijui ni watu wa itikadi gani lakini kama ni waislam hiyo kitu huitwa siku 40 baada ya mtoto kuzaliwa ambapo huendana na kisomo ( maulidi) watu hula na kunywa na kufurahi na ndipo hata huyo mtoto hunyolewa zile nywele wanazoita za utotoni yaani alizozaliwa nazo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom