Inawezekana ila wasomi hata wale waliosomea kilimo hawataki kulima. Wanataka kazi za maofisini. Wakulima wa vijijini hawana elimu ya kutosha kuhusu kilimo cha kisasa. Gharama nacho ni kizuizi kikubwa. Ili kuotesha bustani kama hiyo hapo juu unahitaji mbegu bora, madawa ya kuua wadudu, mbolea na maji ya kumwagilia. Mkulima mdogo wa kijijini hana mtaji huo. Halafu akipeleka mazao yake sokoni bei anayoikuta haiwezi kurudisha gharama zake. Kilimo cha mkulima mdogo Tanzania kinachukuliwa kama hobby na siyo biashara. Lakini mkulima mwenyewe anayo akili na uzoefu wa kujua kuwa kilimo haklilipi. Serikali yetu inatambua kilimo cha wawekezaji (wapora ardhi) lakini inadiliki kumlazimisha mkulima mdogo mzalendo kuiuza mazao yake kwa bei ya hasara. Kilimo Kwanza ati.
Uvivu pia unachangia hapa. Mtu yeyote mwenye bidii na nia anaweza kufanya bustani ya mboga mboga na kuuza kwa beii nzuri kumwendeshea maisha. Lakini kila mmoja wetu ni bingwa wa siasa na maneno meeeeengi. vitendo = sufuri.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.